Kuhusu Bandari; Hii ndio ahadi ya CCM Kwa wananchi

jingalao

JF-Expert Member
Oct 12, 2011
35,052
28,242
Usafiri wa Majini

Kwa kushirikiana na sekta binafsi, kuendelea kuboresha
huduma za uchukuzi katika Bandari za mwambao kwa kufanya
yatuatayo:-
(a) Kuanza ujenzi wa gati Na. 13 na 14 katika Bandari ya Dar es
Salaam;
(b) Kukamilisha uboreshaji wa gati Na. 1 – 7 ili kuimarisha
utoaji wa huduma katika Bandari ya Dar es Salaam;
(c) Kuanza ujenzi wa gati la kushusha magari (RoRo) katika
Bandari ya Dar es Salaam;
(d) Kuanza ujenzi wa bandari mpya za Bagamoyo na Mwambani
Tanga;
(e) Kuanza na kukamilisha ujenzi wa magati manne (4) ya
ziada katika Bandari ya Mtwara;
(f) Kukamilisha ujenzi wa Bandari ya Nyamisati ili kuboresha
usafirishaji wa kwenda na kutoka Mafia;
(g) Kuendelea kuboresha Bandari ya Mwanza, upanuzi
wa Bandari ya Musoma na ujenzi wa magati ya Ntama,
Lushamba na Kiyamkwiki;
(h) Kuendelea na uboreshaji wa miundombinu ya bandari
za Ziwa Nyasa na Tanganyika ili kuimarisha huduma
zitolewazo kwa kujenga magati ya Kagunga, Kasanga,
Kibirizi, Itungi na Kiwira;
(i) Kuboresha mfumo wa uondoshaji mizigo katika Bandari ya
Dar es Salaam kwa lengo la kuongeza kiwango cha utendaji
kwa kuweka mfumo wa “electronic window System” na
kufunga mita za kupima mafuta; na
(j) Kujenga na kukamilisha meli mbili za abiria na mizigo
katika Ziwa Tanganyika, meli moja ya abiria na mizigo
katika Ziwa Victoria na meli nyingine ya abiria na mizigo
katika Ziwa Nyasa. 2015-20


Katika miaka mitano ijayo, Chama kitaelekeza Serikali kuendelea
kuwekeza katika miundombinu ya kimkakati. Miundombinu hiyo
inajumuisha ya reli, viwaja vya ndege na bandari. Pia kuboresha huduma
za usafiri wa anga, baharini na kwenye maziwa kwa kununua vyombo
vipya vya usafiri na kukarabati vyombo vilivyopo ili kuimarisha huduma.
Ili kufikia azma hiyo, katika kipindi hicho miradi itayotekelezwa katika
maeneo mbalimbali ni kama ifuatavyo:-

(a) Kuboresha na kuimarisha utendaji wa Mamlaka ya Bandari Tanzania
(TPA), Shirika la Reli Tanzania (TRC) na Shirika la Ndege la Taifa
(ATC) ili yaweze kutoa mchango stahiki katika usafiri na usafirishaji
nchini na nchi jirani. Vilevile, Shirika la Wakala wa Meli Tanzania
(TASAC) litaimarishwa kwa ajili ya kutoa huduma za uwakala wa
meli na kusimamia ulinzi na usalama wa usafiri na mazingira wa
majini;
(b) Maboresho ya Huduma za Bandari
(i) Miradi itakayotekelezwa chini ya Bandari ya
Dar es Salaam
Ujenzi wa matanki ya kuhifadhia Mafuta;
Ujenzi wa gati namba 12-15 kwa ajili ya makasha;
Usimikaji wa mikanda ya kushusha mzigo wa kichele;
Ujenzi wa (central workshop);
Kujenga ofisi jijini Dodoma;
Ujenzi wa gati katika bandari ya Bagamoyo;
Kuboresha miundombinu katika Chuo cha Bandari;
Kupanua na kuchimba lango la kuingilia na eneo la
kugeuzia meli (entrance channel and turning basin);
Ujenzi wa barabara ya Bandari, Mivinjeni na daraja la bandari

2020-2025.



KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!
 
Back
Top Bottom