Freestyler
Senior Member
- Dec 15, 2010
- 198
- 9
Mara sehemu ya kwanza ya makala haya ilipotoka wiki iliyopita, nilipata taarifa ya mshtuko. Nilinasa sherehe za watu wanaochekelea. Wanadai vurugu za Arusha zimefanikiwa kuwaweka juu.
Ni ile ile falsafa ya siasa za majitaka. Kwamba baadhi ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wanaona Arusha ni mtaji wa kuwaweka hai kisiasa. Kufa kufaana!
Sidhani kama nchi inastahili kuendelea kuwavumilia wanasiasa wa aina hii.
Wapo radhi kuona damu inamwagika, watu wanakufa ili kutimiza matakwa yao kisiasa. Serikali ikigoma kumuadhibu, wewe mwananchi chukua hatua kwa kumchukia moja kwa moja.
Nasikitika kwamba kura yangu kwenye Uchaguzi Mkuu 2010 niliitumbukiza pasipostahili. Nilimpa aliyekuwa Mgombea Urais wa CHADEMA, Willibrod Slaa (pichani)ambaye nimebaini kuwa hafai hata kidogo.
Slaa ni chanzo cha mauaji ya Arusha. Najiuliza ujasiri wa kuichimba mkwara serikali kaupata wapi! Nastaajabu kuona kwamba mtu huyo, eti aliwahi kusimama kwenye mimbari na kuhubiri Neno la Mungu.
Ni padri gani anayeweza kuwa mchochezi. Anayewatuma watu wakauawe! Nasikitika kuona kwamba mpaka leo, bado kuna wananchi hawajataka kukubali ukweli.
Slaa aliwatuma vijana wa Arusha wakauawe kwa sababu alijua polisi kuna nini. Anafahamu kwamba vituo vya polisi, hasa vikubwa vina zana za kila namna kukabiliana na wahalifu. Unauliza bunduki polisi?
Akifahamu hilo, yeye aliwaamrisha vijana kwenda kuvamia kituo cha polisi na kuwatorosha, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema. Alitegemea nini?
Je, polisi wangekubali kuvamiwa, wapigwe, wauawe? Ni dhahiri Slaa alijua kwamba vijana wangekabiliana na jibu la kijeshi ambalo lingegharimu maisha yao. Hicho ndicho kilichotokea. Alifanya makusudi.
Alitamani watu wafe ili ajiongezee mtaji wa kisiasa. Alikosea kupita kiasi. Damu za wahanga wa Arusha itazunguka kwenye kichwa chake. Aliwatuma yeye, basi kama si duniani, mbinguni atahukumiwa.
Kama nilivyouliza wiki iliyopita, kwa nini Slaa hakusimama mstari wa mbele kwenda kuwatorosha Mbowe na Lema? Aliagiza tu, yaani yake ndiyo roho, za wale vijana ni nini? Ni kama msemo risasi kwa tembo, binadamu aah!
Alijifanya mshika rimoti na kubonyeza, akaagiza, nendeni kituo cha polisi, mumlete Mbowe na Lema kabla sijaondoka hapa. Inawezekana serikali inamlea kwa sababu ya kuhofia kelele za jumuiya ya kimataifa.
Je, tunastahili kuwalea watu wa aina hii kwa sababu ya woga wa jumuiya za kimataifa? Watanzania tuepuke, tujifunze hulka za wanasiasa, tutambue kuwa wao ni sosi ya migogoro ya nchi nyingi na mauaji ya wenyewe kwa wenyewe.
Ni busara kila Mtanzania akawa macho, aepuke kutumiwa na wanasiasa. Tuchuje maneno ya jukwaani kisha tuyaweke mbele yale yenye masilahi kwa taifa, yenye rangi mbaya tuyapuuze kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho.
Wanasiasa maskini wa hoja hawafai. Hao ni rahisi kutupeleka kwenye machafuko. Wakigundua hawana ajenda ya kuwafanya watengeneze vichwa vya habari, wanakosa amani, hivyo wanaamua kufanya uchochezi na kuyaweka rehani maisha ya wananchi.
Ajenda ya katiba mpya ilipomezwa na Rais Jakaya Kikwete, wakaamua kugeukia Arusha. Ni vizuri wanasiasa wakawa wakweli kwa wananchi, si kusema uongo ili kujipa ushindi wa mezani. Propaganda zilizopitwa na wakati.
CCM na Chadema wote wamecheza rafu Arusha. Ni kama aliyeuziwa cheni ya bandia naye akatoa fedha feki. Ajabu ni kwamba makosa yao, mauti yanawaangukia wananchi. Ni kama nyasi kusiginwa wakati wa mechi ya watani wa jadi.
Kama Chadema walidanganya kwa Rebecca Mngodo (Mbunge Viti Maalum), CCM nao walicheza faulo kwa Mary Chatanda ambaye inadaiwa uwakilishi wake ni Tanga lakini alipelekwa Arusha makusudi kuongeza kura.
Chadema hawaelezi ukweli kwamba Arusha, CCM ina madiwani wengi kuliko wao. Wanataka uchaguzi wa Meya urudiwe ilhali hata wakifanya hivyo, bado chama tawala kina nafasi kubwa ya kutetea. Kina wapiga kura wengi ndani ya halmashauri ya jiji.
Tatizo hapa ni kwamba wanawatumia wananchi kama mitaji yao, kwa hiyo wanaendelea kuwazuga kwa hoja za kizamani. Wamechagua kuwa wapinzani, kwa hiyo wanapinga kila kitu. Mtu kashindwa anadai kachakachuliwa, anaambiwa athibitishe madai yake, anashindwa.
Nasikitika kwamba uchaguzi ulishapita na kura nilishaitumbukiza pasipostahili. La kujifunza ni kwamba siku nyingine kabla sijachagua, nitachanganua vilivyo aina ya mtu ninayemtaka.
Nashukuru Mungu hakushinda, maana leo ningejuta zaidi.
Source
Ni ile ile falsafa ya siasa za majitaka. Kwamba baadhi ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wanaona Arusha ni mtaji wa kuwaweka hai kisiasa. Kufa kufaana!
Sidhani kama nchi inastahili kuendelea kuwavumilia wanasiasa wa aina hii.
Wapo radhi kuona damu inamwagika, watu wanakufa ili kutimiza matakwa yao kisiasa. Serikali ikigoma kumuadhibu, wewe mwananchi chukua hatua kwa kumchukia moja kwa moja.
Nasikitika kwamba kura yangu kwenye Uchaguzi Mkuu 2010 niliitumbukiza pasipostahili. Nilimpa aliyekuwa Mgombea Urais wa CHADEMA, Willibrod Slaa (pichani)ambaye nimebaini kuwa hafai hata kidogo.
Slaa ni chanzo cha mauaji ya Arusha. Najiuliza ujasiri wa kuichimba mkwara serikali kaupata wapi! Nastaajabu kuona kwamba mtu huyo, eti aliwahi kusimama kwenye mimbari na kuhubiri Neno la Mungu.
Ni padri gani anayeweza kuwa mchochezi. Anayewatuma watu wakauawe! Nasikitika kuona kwamba mpaka leo, bado kuna wananchi hawajataka kukubali ukweli.
Slaa aliwatuma vijana wa Arusha wakauawe kwa sababu alijua polisi kuna nini. Anafahamu kwamba vituo vya polisi, hasa vikubwa vina zana za kila namna kukabiliana na wahalifu. Unauliza bunduki polisi?
Akifahamu hilo, yeye aliwaamrisha vijana kwenda kuvamia kituo cha polisi na kuwatorosha, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema. Alitegemea nini?
Je, polisi wangekubali kuvamiwa, wapigwe, wauawe? Ni dhahiri Slaa alijua kwamba vijana wangekabiliana na jibu la kijeshi ambalo lingegharimu maisha yao. Hicho ndicho kilichotokea. Alifanya makusudi.
Alitamani watu wafe ili ajiongezee mtaji wa kisiasa. Alikosea kupita kiasi. Damu za wahanga wa Arusha itazunguka kwenye kichwa chake. Aliwatuma yeye, basi kama si duniani, mbinguni atahukumiwa.
Kama nilivyouliza wiki iliyopita, kwa nini Slaa hakusimama mstari wa mbele kwenda kuwatorosha Mbowe na Lema? Aliagiza tu, yaani yake ndiyo roho, za wale vijana ni nini? Ni kama msemo risasi kwa tembo, binadamu aah!
Alijifanya mshika rimoti na kubonyeza, akaagiza, nendeni kituo cha polisi, mumlete Mbowe na Lema kabla sijaondoka hapa. Inawezekana serikali inamlea kwa sababu ya kuhofia kelele za jumuiya ya kimataifa.
Je, tunastahili kuwalea watu wa aina hii kwa sababu ya woga wa jumuiya za kimataifa? Watanzania tuepuke, tujifunze hulka za wanasiasa, tutambue kuwa wao ni sosi ya migogoro ya nchi nyingi na mauaji ya wenyewe kwa wenyewe.
Ni busara kila Mtanzania akawa macho, aepuke kutumiwa na wanasiasa. Tuchuje maneno ya jukwaani kisha tuyaweke mbele yale yenye masilahi kwa taifa, yenye rangi mbaya tuyapuuze kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho.
Wanasiasa maskini wa hoja hawafai. Hao ni rahisi kutupeleka kwenye machafuko. Wakigundua hawana ajenda ya kuwafanya watengeneze vichwa vya habari, wanakosa amani, hivyo wanaamua kufanya uchochezi na kuyaweka rehani maisha ya wananchi.
Ajenda ya katiba mpya ilipomezwa na Rais Jakaya Kikwete, wakaamua kugeukia Arusha. Ni vizuri wanasiasa wakawa wakweli kwa wananchi, si kusema uongo ili kujipa ushindi wa mezani. Propaganda zilizopitwa na wakati.
CCM na Chadema wote wamecheza rafu Arusha. Ni kama aliyeuziwa cheni ya bandia naye akatoa fedha feki. Ajabu ni kwamba makosa yao, mauti yanawaangukia wananchi. Ni kama nyasi kusiginwa wakati wa mechi ya watani wa jadi.
Kama Chadema walidanganya kwa Rebecca Mngodo (Mbunge Viti Maalum), CCM nao walicheza faulo kwa Mary Chatanda ambaye inadaiwa uwakilishi wake ni Tanga lakini alipelekwa Arusha makusudi kuongeza kura.
Chadema hawaelezi ukweli kwamba Arusha, CCM ina madiwani wengi kuliko wao. Wanataka uchaguzi wa Meya urudiwe ilhali hata wakifanya hivyo, bado chama tawala kina nafasi kubwa ya kutetea. Kina wapiga kura wengi ndani ya halmashauri ya jiji.
Tatizo hapa ni kwamba wanawatumia wananchi kama mitaji yao, kwa hiyo wanaendelea kuwazuga kwa hoja za kizamani. Wamechagua kuwa wapinzani, kwa hiyo wanapinga kila kitu. Mtu kashindwa anadai kachakachuliwa, anaambiwa athibitishe madai yake, anashindwa.
Nasikitika kwamba uchaguzi ulishapita na kura nilishaitumbukiza pasipostahili. La kujifunza ni kwamba siku nyingine kabla sijachagua, nitachanganua vilivyo aina ya mtu ninayemtaka.
Nashukuru Mungu hakushinda, maana leo ningejuta zaidi.
Source