Kuhusu Afrika Kusini na xenophobic attacks.

bahati93

JF-Expert Member
Aug 6, 2015
1,129
2,002
Lengo la uzi huu ni kufafanua kwa kisanyansi nguvu zinazowasukuma wasauzi kufanyia fujo watu ambao sio wa jamii yao huko nchini kwao south afrika. Hizo force ni kama ifuatavyo.

UTANDAWAZI. Kwa dunia ya sasa kuna mwingiliano mkubwa sana wa jamii za watu mbalimbali dunia nzima, ni asili ya wenyeji kutaka kuzuia wageni kuingia makwao ( hii inatokana na jinsi binadamu alivyo evolve kutoka vikundi vidogo dogo ( darwin theory of evolutional) hapo kale kulikuwa na mipaka na iliheshimiwa) na kila jamii hapa duniani ina lugha ambayo inatambulisha wote kwa ujumla { sisi , wao} so hapa tunachoshuhudia ni vita kati ya sisi na wao ambapo sisi ni wasauthi na wao ni wageni

KUTOKUWAJIBIKA. Hili ni jambo ambalo na hakika kila mtu ana kiasi chake cha kukwepa kubeba lawama. Hii point ni muhimu sana kwani imekuwa chanzo kikubwa sana katika kuleta chuki baina ya jamii ya wenyeji na wageni pale ambako wageni wataonekana wana maisha mazuri kuliko wenyeji baathi ya mifano hai ni GERMANY pale ambako waliona kama wayahudi ndio wamefanya maisha yao yawe magumu, pia wakasemwa wao ndio waliosababisha wao kushindwa vita ya kwanza ya dunia hiii yote kutokana na kutokutaka kukubali kwamba makosa yamefanyika na ni wote kubeba lawama. Na hapa wasauth wamenasa kwenye mtego huo huo wa kifrika Badala ya kuchunguza kwa nini watu wao hawana elimu kuwafanya kushindana kwenye soko la ajira wanabaki kurusha lawama kwa wageni.

HUMAN BRAIN. Matendo ya binadamu yote yanaratibiwa na mawazo yalio katika mbongo zetu sasa. Hapa nataka kusema ni kwamba kitalaam kutokana na evolution a human brain imekuwa ikibadilika ili kukidhi mahitaji sasa kilichotokea ni kwamba our frontal lobe ( ubongo wa mbele ) umeadvance sana na kuweza kufikiri na kuwa rational ( ni irrational kwa wanachofanya wasauth ) but imekuaje mpaka maamuzi haya wakayaona ni rational, primary brain ( lizard brain) ni responsible huu ni mfumo wa faham ambao wanadamu wote tumeridhi from our common ancestral way back sasa hii brain ndo inadirect out instinct of survivor hii brain inatake over pale ambako inahisi uhai umehatarishwa (self defense) angalia viumbe vyote vinajihami kupigania uhai wao automatic.

So hawa wasouth hii brain imetake over couse they sense maisha yao yapo hatarini.

MOB PSYCHOLOGY. This ni crazy situation ni kwamba katika mob watu hawafanyi maamuzi yao bali wanafuata maamuzi ya kiongozi wao. Huyu kiongozi anachokuwa anafanya ni kuongea maneno ya kuwatia hasira watu na kisha kutoa suggestion of how outlet their anger. Hapa ndipo wata direct either kwa mtu au mali.

Bado wanadamu tunaevolve haya yanayotokea ni kama case studies ili jamii nyingine zijifunze zisije fanya makosa ambayo yanafanyika. In time wasauth watapona madonda ambayo yapo kwa jamii zao since wamepitia mengi sana. Plus ukiweka na umaskin na ujinga ambao unawakabili.
 
Immigration policy zao zina semaje hata US huwezi kuingia tu kizembe. Nchi yeyote ikitaka iendelee kubali watu wanaofanya kazi kwa juhudi alafu tax them more
 
Pia karibu nchi karibu zote za Africa Hazina mipango ya nchi inayoeleweka, na hata hiyo isiyoeleweka haisimamiwi.
 
Pia karibu nchi karibu zote za Africa Hazina mipango ya nchi inayoeleweka, na hata hiyo isiyoeleweka haisimamiwi.
Nikweli huwezi kuingia nchi ya watu na kufanya kazi ambayo mzawa anaweza fanya, ila sijui huko SA wana ruhusu vipi alafu baadae wana waua wageni
 
WaSauzi sio wabaguzi....stori ya ubaguzi ni siasa za mitandaoni....wageni wanauawa kwa sababu wanafanya ujambazi,wizi,uporaji. Sisi ndo tunafanya mauaji yaonekane ni ubaguzi
 
Nikweli huwezi kuingia nchi ya watu na kufanya kazi ambayo mzawa anaweza fanya, ila sijui huko SA wana ruhusu vipi alafu baadae wana waua wageni
wazawa hawapo skilled enough, na pia nasikia hawapendi kufanya kazi
 
WaSauzi sio wabaguzi....stori ya ubaguzi ni siasa za mitandaoni....wageni wanauawa kwa sababu wanafanya ujambazi,wizi,uporaji. Sisi ndo tunafanya mauaji yaonekane ni ubaguzi
Ndio maana nimesema nchi za Africa hazijiwekei mipango na kusimamia.
 
Immigration policy zao zina semaje hata US huwezi kuingia tu kizembe. Nchi yeyote ikitaka iendelee kubali watu wanaofanya kazi kwa juhudi alafu tax them more
Hiyo ndio policy za wenzetu, na wako makini sana kufuatilia.
 
WaSauzi sio wabaguzi....stori ya ubaguzi ni siasa za mitandaoni....wageni wanauawa kwa sababu wanafanya ujambazi,wizi,uporaji. Sisi ndo tunafanya mauaji yaonekane ni ubaguzi
Mungu anakuona kwa uongo huu, Wasouth ndio wanaongoza kwa uvivu na kutafuta short cut kwa wizi na ujambazi...Wao wenye national ID ndio wanaoongoza kwa kuuziwa silaha kama bidhaa nyingine tu.
 
Nikweli huwezi kuingia nchi ya watu na kufanya kazi ambayo mzawa anaweza fanya, ila sijui huko SA wana ruhusu vipi alafu baadae wana waua wageni
Mkuu! Wa South ni Wavivu sijawahi kuona...
Nikupe mfano mmoja!

SA ikifika Msimu wa baridi Raia hawaendi kazini kabisa, na Viwanda vinahitaji kufanya productions inabidi Viajiri Wageni ili kazi ziende coz Wageni hawana longolongo.

Raia akipata mshahara tu, haendi kazini, pombe starehe kwenda Mbele mpaka pesa ikiisha ndo anarudi kazini.

Kwa mazingira Kama haya mgeni always Ana nafasi kupata kazi kuliko Raia.

Shule wamekataa, kazi hawataki.
 
Kuongezea kidogo wazuru hawajatahiriwa ,wanawake wa kizuru wanapenda waliotahiriwa hapo chuki ingine inaanzia. 🤣 🤣
 
Nani kasema kwanza weusi ndo roho mbaya kupitiliza nimekaa nje south Africans siyo watu nafikiri sijui kwa walitoyapitia ndugu zao.kwanza neno ahsante ni gumu sana kwao kulitamka niliishii Kule mwaka nikakimbia zangu
WaSauzi sio wabaguzi....stori ya ubaguzi ni siasa za mitandaoni....wageni wanauawa kwa sababu wanafanya ujambazi,wizi,uporaji. Sisi ndo tunafanya mauaji yaonekane ni ubaguzi
 
Back
Top Bottom