Kuhatarisha usalama wa Taifa? Give me a Break!

JamiiForums

Official JF Response
Nov 9, 2006
6,200
4,984
Baija Bolobi said:
Madudu mengi na ya hatari yanayotokea katika siasa za nchi yetu yanaashiria kuwa idara yetu ya Usalama wa Taifa imefika mwisho kiutendaji. Ebu ona:-

-Rais akamteua Chenge baada ya kuvunjwa kwa Baraza la mawaziri. Watu wakapiga kelele, yeye akakaidi. Baada ya muda mfupi akalazimika kumwondoa kwa aibu!

-Nape na Malisa wakavutana kuhusu uongozi wa UVCCM; Rais akawatosa wote na kumchukua Masauni. Amegundulika alifoji umri, akaondoka, lakini aibu ikabaki kwa Rais. Hakuna aliyewajibishwa katika idara ya Usalama.

-Sasa tunaambiwa Bashe si raia. Amekuwa katika nafasi nyingi ikiwamo NEC. Chiligati anasema walipitiwa tu. Wamepitiwa mangapi?

La kujiuliza, hivi tuna ile Idara ya Usalama wa Taifa au sasa ni Idara ya Uhasama wa Taifa? Kinachoonekana kujengeka sasa ni kuwa uhasama katika mahusiano ya watawala ni mkubwa sana. Leteni maoni ya nini mwisho wa uhasama huu.

Kwa wasiojua majukumu ya taasisi hii wa-download attachment hii:


Kazi ya Usalama wa Taifa pia imegawika katika mafungu haya:
1. Kulinda Viongozi Wakuu- Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, na Viongozi wa staafu wa ngazi hizo, (pamoja na kulinda viongozi wakuu wa UWT km mkurugenzi wake mkuu).
2. Kukusanya taarifa za usalama kwa lengo la kujua mood ya wananchi kuhusiana na kila tukio linalotokea ama lisilotokea nchini ili kuiwezesha serikali kufanya maamuzi sahihi, na mara zote kulinda maslahi ya taifa.
3. Kutafuta intelligensia kutoka nje ya mipaka zenye kuiwezesha nchi kujua siri za ndani za nchi nyingine, rafiki ama shindani, ama hasimu, ili ziweze kuisaidia kufikia maamuzi sahihi (informed decisions) kuhusiana na mambo mbalimbali ya kitaifa na kimataifa.
Kufanya mauaji ni sehemu ya kazi ya TISS na idara yoyote ile ya kijasusi katika nchi mbalimbali ila haiwi wazi inaweza kufanyika kwa kuwekewa sumu ambayo mtu anaweza kufa hapohapo au baada ya siku tatu au hata zaidi kutegemea na aina ya sumu na kiwango chake na pia kuna ajali ya gari ambayo inaweza kuonekana kama ya kawaida kabisa au ya kusababishwa na aina ya hila yoyote ile kama ilivyotokea kwa Diana ionekane alikuwa anawakimbia wapiga picha na kuna ambayo wengi wamezoea ambayo ni ya kumfuata mlengwa na kumpiga risasi mahali popote nyumbani kwake, kwenye mkutano au sehemu yoyote inapopatikana nafasi hiyo.

Ni kweli kuwa kazi ya usalama wa Taifa ni kulinda masilahi ya Taifa lakini na raia wakeila kuna nyakati huwa ni kwaajili ya kulinda wakubwa wachache au serikali husika na masilahi yake na hapa inaweza kufikia hata kuua kiongozi mkubwa na mwandamizi au hata kundi la watu kwa mfano aliyekua waziri mkuu wa Israel Yitzak Rabin huyu alipigwa risasi na ikasemekana ni raia ila ukweli ulivyo yule hakuwa raia wa kawaida alikuwa alinda kile ambacho Waisrael wanakiamini siku zote na PM. Yeyote anapochukua nchi ile anatakiwa akifuate akikiuka siyo mwenzao tena atatolewa kafara kwa namna yoyote ile kuhakikisha Israel inabaki kuwa ilivyo kama wanavyoamini wayahudi na ni wakatili mawako tayari kuona mwarabu anapata anachokitaka okay basi tufanye hivi kule midle east kuna waarabu kibao tena ambao ni wazaliwa Israel kwa nini asitumwe kwenda kufanya yale mauaji lakini yakafanywa na myahudi mwenzake? Angalia wengine kama Rafik Harir wa Syria, na hata marehemu Kombe aliuawa na Polisi wakimtuhumu kuwa ni Jambazi pamoja na kuwa alijitambulisha kuwa yeye ni nani!

Ngoja nikupe mfano mwingine ambao huu utawachanganya wengi na wavivu wa kusoma na kuchunguza tutawaacha mbali sana WTC huko New York ambapo walikufa zaidi ya watu 3000 na kuwasingizia magaidi na kuzua vita ambavyo vimedhulumu maisha ya wanyonge wengi bila kujali aina ya dini kabila au hata utaifa maana walikufa wamarekani na waisilamu wa Iraq na kwingineko duniani na hata kumnyonga Sadam na hali ikawa mbaya Iraq kuliko alivyokuwepo Sadam Hussein na pia kubadilisha mambo mengi duniani ikiwemo kuvujiana heshima na kutuhumiana ugaidi kwa kumpima mtu kwa itikadi yake tu na hata kumdhalilisha

Ni matumain yangu humu JF. Kuna wakandarasi ambao wanaweza kutoa ufafanuzi wa jinsi gorofa linaweza kujengwa namna gani halafu ligongwe na ndege lishuke kama ice cream juani na kuwa vumbi na wanahabari watoe picha ambazo nyingi zinafanana na hasa ukizingatia kwa wenzetu suala TEKNOHAMA wako mbali wana vyombo vingi vya kudugundua mambo mengi HEBU WANAJF.TUSIWE WATU WA MALUMBANO MENGI HUMU NDANI TUPATE MUDA WA KUSOMA NA KUCHUNGUZA MAMBO KWA KINA UTANIELEWA NASEMA NINI HAYA NINAYOYANGEA HUMU

ANGALIZO: Hapa simaanishi magaidi hawapo laa ila magaidi wapo na wanafanya kazi zao na wengine kibao tunao hata hapa kwetu tena wanajishikamanisha vizuri sana wakubwa wa serikali zetu kwa kuifadhili na kutoa michango mbalimbali kwenye serikali na jamii kwa ujumla na ukijidai kuwafuatilia yaweza kukuta makubwa maana baadhi ya wakubwa wana masilahi yao huko.

Hivyo basi moja ya kazi ya idara yoyote ya ujajusi ni kufanya ujasusi na project za siri katika nchi mbalimbali tatizo ni kuwa hapa kwetu na baadhi ya nchi nyingi zinatumia vibaya Idara hizo badala ya kujiletea maendeleo kama Nchi za urusi na Asia na hivyo sehemu kubwa kuishia kulinda kundi la watu wachache na madaraka yao maana hao ndiyo wenye uwezo wa kumpoint mkurugenzi na wengine katika kazi nyeti za serikali iliyoko madarakani.

Idara hii ina watu wengi sana tena wengine hawathaminiki katika jamii kabisa na wanafanya kazi kizalendo zaidi na kutanguliza masilahi ya Taifa mbele lakini wanakwamishwa na urasimu na kutokuchukuliwa hatua kwa wahusika (watu hatarishi wa usalama) na ikumbukwe kuwa idara hizi kwenye nchi nyingi huingia maeneo mengi sana mbalimbali unaweza kumkuta waziri,Mchungaji, sheikhe, mhadhiri,mwana habari, mfagiaji, dereva wa dalala au tax, fundi viatu, mwalimu, padre,mwanamuziki, makahaba na kwa hapa Dsm. Hata muuza samaki (pweza) kwenye sinia anaweza akawa na akafanya kazi kwa ufanisi mzuri kabisa ila mwana usalama wa kweli hana na habebi bango la kujitangaza waziwazi kuwa yeye ni mwana usalama na ndiyo maana ukimwona mtu anajigamba sana ujue huyo ni feki na ana masilahi yake binafsi ukiacha wale ambao wanafanya kazi za wazi za kuwalinda viongozi Top5 kingine kazi ya kukamata wahalifu mara nyingi huwa ni kazi ya polisi na kama kuna ofisa usalam akitaka kukamata anaweza kukamata kama raia mwingine yeyote kulingana na sheria za nchi MZISOME! raia anaweza kumkamata mhalifu ila ikiwa ni lazima sana kwa mwanausalama kufanya hivyo kimabavu anaweza kufanya hivyo akishirikiana na polisi na vyombo vingine vya dola kama vile PCCB, Uhamiaji, TFDA, Jeshi nk. TENA IKUMBUKWE KUWA OFISA WA IDARA YA USALAMA WA TAIFA HAKAMATI MVUTA BANGI MARA NYINGI ATAKUWA RAFIKI YAKE ILI AWEZE KUJUA BANGI INALIMWA WAPI NA KUPELEKWA KUUZWA WAPI HAWAKURUPUKI TU. Lakini sio mbwembwe ambazo watu wengi wanapenda kujionyesha nazo kuwa wao ni wana usalama na kuwakera wengine.

Kwa kwa kuongezea ni kuwa hakuna jambo lolote la hasara na aibu ambalo linaipata nchi hii ambalo vyombo husika na Rais mwenyewe hana Taarifa nalo kila kitu kinajulikana na kutolewa ufanunuzi na hasra zake LAKINI KIKUBWA NI KWAMBA HUPUZWA KWANI WASIKA WENGI HUWA NI MASWAIHIBA WA RAIS AU WAZIRI MHUSIKA NA HATA VIONGOZI WAANDAMIZI Na ndiyo maana mara nyingi Rais anashindwa kuchukua maamuzi magumu maana yanaweza kumgusa yeye mwaneyewe au yalianzia kwake mwenyewe. Lakini idara ina heshima zake na kukusanya taarifa mbalimbali za kiulinzi na usalama na hata kiuchumi lakini hazitiliwi maanani zinawekwa kapuni na kama unabisha mtafute rafiki yako yeyote wa karibu muulize kiundani kama hawahui mambo yanyoendela nchi hii lakini hana namna ya kufanya.

OMBI NA TAHADHARI:
IDARA HII ISIBEZWE NA KULAUMIWA KWA KUWABEBA WANASIASA NA KUTOKUFANYA KAZI YAKE IPASAVYO NI KWA SABABU YA MFUMO WENYEWE ULIVYO KAMA NDANI YA JESHI NA IKUBUKWE KWA WALE WALIOPITIA HOJA ZANGU ZA MWANZO NILIONYESHA JINSI WANAVYOTOA KAZI KUANZIA NATIONAL SERVICE KWA MAANA HIYO IDARA HII NI PARAMILITARY NA KUNA CHAN OF COMMAND AMBAYO KILA MTU ANAIFUTA KULINGA NA ORDER ALIYOPEWA NA AMIRI JESHI MKUU WA MAJESHI NI RAIS MWENYEWE WA JMT.

ILA NA WAO WAMECHOKA NA UOVO UNAOENDELEA SERIKALINI MPAKA HUKO KWENYE MAJESHI NA HII NI HATARI SANA INAWEZA KUJA KULETA MACHUFUKO SIKU ZA USONI KAMA IVORY COAST NA KWINGINEKO MAANA HAWANA UHAKIKA NA MAISHA YAO YA BAADAYE YA WATOTO WAO NA NDUGU ZAO MAANA KILA KITU KIZURI NA CHENYE MASILAHI KIMESHIKWA NA WAKUBWA NA WAJANJA WACHACHE.
 
Hii ndo Tanzania bwana. Baadae tutatafuta mwekezaji atusaidia kusimamia usalama wa taifa. Yaani kila kitu kimebinafsishwa - hadi kufikiri. Kama kweli Chiligati amesema walipitiwa basi iko siku hii nchi tutakuwa na rais asiye mtanzania. Tatizo letu ni kulindana na kuogopa kufanya un-popular tough decision. Watu wanajua hata wasipotimiza majukumu yao nyeti hakuna atakayewawajibisha.

More to come...let us wait and see
 
Baija, ni muda mrefu tume-conclude humu jamvini kwamba Usalama wa Taifa ((UWT) ile wing ya CCM ya kinamama should be UW-CCM)nchi hii ni kama hakuna. Kimsingi wao wamekuwa kama Security & Intelligence wing ya CCM katika kupambana na upinzani wowote dhidi ya maslahi ya chama.

Mgeni yeyote toka popote wa rangi yoyote ya ngozi anaweza kuingia Tanzania akafanya anachotaka kisha ama akaondoka zake au akaendelea kudunda nchini raha mustarehe. Nchi inavyoyumbishwa kiuchumu, kiutamaduni na kimaadili ni hatari kwa usalama wake.

Ni jukumu la UWT ku-rectify issues kama hizo lakini hapa Tanzania, CCM wanachakachua kila kitu yet wao (UWT) wanakenua meno as long as akaunti zao zinanona.
 
Sidhani kama U/Taifa ni wazembe kwa kiasi hiki.

Ninachokiona mimi tatizo ni Ubishi na kupenda misifa kwa viongozi wetu wakubwa.

Kwa mfano swala la Masauni na hata lile la Chenge kurudishwa barazani lilibezi kwenye mbwembwe na ubishi tu.

Ni mambo ambayo yalikuwa wazi wazi.
 
kuna haja ya badiliko katika ofisi hiii, kunapotokea mabadiliko makubwa kwama yetu kutoka mfumo wa chama kimoja kwenda vyama vingi ilikuwa lazima ofisi hii ifumuliwe na iundwe upya, sasa sisi wamefanya kimya kimya......, anajua mkapa na wenzake
 
Madudu mengi na ya hatari yanayotokea katika siasa za nchi yetu yanaashiria kuwa idara yetu ya Usalama wa Taifa imefika mwisho kiutendaji. Ebu ona:-

-Rais akamteua Chenge baada ya kuvunjwa kwa Baraza la mawaziri. Watu wakapiga kelele, yeye akakaidi. Baada ya muda mfupi akalazimika kumwondoa kwa aibu!

-Nape na Malisa wakavutana kuhusu uongozi wa UVCCM; Rais akawatosa wote na kumchukua Masauni. Amegundulika alifoji umri, akaondoka, lakini aibu ikabaki kwa Rais. Hakuna aliyewajibishwa katika idara ya Usalama.

-Sasa tunaambiwa Bashe si raia. Amekuwa katika nafasi nyingi ikiwamo NEC. Chiligati anasema walipitiwa tu. Wamepitiwa mangapi?

La kujiuliza, hivi tuna ile Idara ya Usalama wa Taifa au sasa ni Idara ya Uhasama wa Taifa? Kinachoonekana kujengeka sasa ni kuwa uhasama katika mahusiano ya watawala ni mkubwa sana. Leteni maoni ya nini mwisho wa uhasama huu.

Kuna siku Hassy Kitine alisema haya alionekana mjinga. Alisema mawaziri wanaoteuliwa na rais wengi hawastahuli kuwepo kwenye nafasi ile, kwa kuwa usalama wa taifa haushirikishwi na wenyewe hautaki kujishirikisha. Kila siku watu wanasema usalama wa taifa wa sasa si kwa jili ya usalama wa taifa, ni usalama wa CCM, sasa naona hata usalama wa CCM inadhindwa kuulinda.

Kama maamuzi makubwa ya chama yanafanywa na NEC, kama maamuzi makubwa ya NEC yanaihusu Tanzania, na kama yanafanywa na wasio watanzania, how can you trust CCM. It is so stupid kusema eti walitupiwa, so stupid answer ina maana hata CCM haina idara ya usalama. Kama Bashe na wajumbe wengine wa NEC ni Bashe like, what do you expect. Maamuzi yatakuwa kwa manufaa ya Tanzania au ya wageni, au wafanyabiashara waliowaweka madarakani.
 
Kwa kweli usalama wa Taifa, ni moja kati ya Idara ambazo zimekufa kabisa Tanzania, kwa sababu zimebadiliza role zake kabisa. Najua wanasoma hapa Jamii Forums, subiri niwakukumbushe, hawa watu wameacha kulinda maslahi ya taifa, wanalinda viongozi, tena bora wangekua wanawalinda physically, yaani wanawalinda viongozi kwenye kashfa tu, ila physically hamna ulinzi wowote wa maana, sema tu nchi yetu ni ya amani.

Hapa Tanzania, watu toka nchi jirani wanaingia tu bila hata passport, achilia mbali visa. hebu check mikoa ya mipakani yote kuna wageni kibao, ambao wanaenda sehemu yeyote na kufanya chochote. Watu wanaambiwa sio raia wakati walishakua viongozi wakubwa tu, wanasahau kwamba usalama wanadhalilika.

CHANZO CHA TATIZO

Chanzo kikubwa cha tatizo ni Usalama wa Taifa kuwa chini ya executive, yaani wanapelekwapelekwa tu na Rais au hata Waziri, wanafanya kazi kwa maelekezo ya Rais, hii ni hatari sana kwa usalama wa nchi yetu, nchi nyingine nyingi tu ulimwenguni, usalama wa taifa una nguvu kuliko hata Rais, usalama wa Taifa unamuonya na kumkataza Rais kufanya kitu ambacho hakina maslahi ya Taifa. Na ndio maana nchi kama Marekani usalama wa Taifa wanaweza kumuua hata Rais kama anafanya vitu ambavyo havina maslahi ya Taifa. Kwa muundo huo kila mtu ataheshimu usalama wa Taifa.

USALAMA WA TAIFA BONGO? WALISHAFULIA!!!!
 
Madudu mengi na ya hatari yanayotokea katika siasa za nchi yetu yanaashiria kuwa idara yetu ya Usalama wa Taifa imefika mwisho kiutendaji. Ebu ona:-

-Rais akamteua Chenge baada ya kuvunjwa kwa Baraza la mawaziri. Watu wakapiga kelele, yeye akakaidi. Baada ya muda mfupi akalazimika kumwondoa kwa aibu!

-Nape na Malisa wakavutana kuhusu uongozi wa UVCCM; Rais akawatosa wote na kumchukua Masauni. Amegundulika alifoji umri, akaondoka, lakini aibu ikabaki kwa Rais. Hakuna aliyewajibishwa katika idara ya Usalama.

-Sasa tunaambiwa Bashe si raia. Amekuwa katika nafasi nyingi ikiwamo NEC. Chiligati anasema walipitiwa tu. Wamepitiwa mangapi?

La kujiuliza, hivi tuna ile Idara ya Usalama wa Taifa au sasa ni Idara ya Uhasama wa Taifa? Kinachoonekana kujengeka sasa ni kuwa uhasama katika mahusiano ya watawala ni mkubwa sana. Leteni maoni ya nini mwisho wa uhasama huu.
Ukiona tumefikia hapa... basi jua tatizo si la leo, ni la zamani sana na ni sugu

Kwani si tunaona mambo ya akina Upson na Mwakipesile Mbeya??? wale walikua magwiji huko... unakumbuka Kombe???

Kwahiyo ndugu yangu mimi sioni kama tunaelekea pabaya... tulikua pabaya na nio tuko kwenye mpito....
 
Usalama wa Taifa ni waajiriwa wa serikali.

Je nini majukumu ya chombo hiki na mipaka yake? Kiko chini ya Idara au taasisi gani na kinawajibika kwa nani? Kama alivyowahi kusema Hans Kitine kuwa chombo hiki hakisikilizwi na hao wanaotoa maamuzi.

Imefika wakati wa wahusika kuwaondoa dukuduku wananchi kuhusu chombo hiki. Kama ni kukiboresha au kukiunda upya kukidhi mahitaji ya karne hii,yetu macho.
 
Kwa kweli usalama wa Taifa, ni moja kati ya Idara ambazo zimekufa kabisa Tanzania, kwa sababu zimebadiliza role zake kabisa. Najua wanasoma hapa Jamii Forums, subiri niwakukumbushe, hawa watu wameacha kulinda maslahi ya taifa, wanalinda viongozi, tena bora wangekua wanawalinda physically, yaani wanawalinda viongozi kwenye kashfa tu, ila physically hamna ulinzi wowote wa maana, sema tu nchi yetu ni ya amani.

Hapa Tanzania, watu toka nchi jirani wanaingia tu bila hata passport, achilia mbali visa. hebu check mikoa ya mipakani yote kuna wageni kibao, ambao wanaenda sehemu yeyote na kufanya chochote. Watu wanaambiwa sio raia wakati walishakua viongozi wakubwa tu, wanasahau kwamba usalama wanadhalilika.

CHANZO CHA TATIZO

Chanzo kikubwa cha tatizo ni Usalama wa Taifa kuwa chini ya executive, yaani wanapelekwapelekwa tu na Rais au hata Waziri, wanafanya kazi kwa maelekezo ya Rais, hii ni hatari sana kwa usalama wa nchi yetu, nchi nyingine nyingi tu ulimwenguni, usalama wa taifa una nguvu kuliko hata Rais, usalama wa Taifa unamuonya na kumkataza Rais kufanya kitu ambacho hakina maslahi ya Taifa. Na ndio maana nchi kama Marekani usalama wa Taifa wanaweza kumuua hata Rais kama anafanya vitu ambavyo havina maslahi ya Taifa. Kwa muundo huo kila mtu ataheshimu usalama wa Taifa.

USALAMA WA TAIFA BONGO? WALISHAFULIA!!!!

Mkuu ukisikia jinsi jamaa wanavyofanya kazi hata huwezi kuamini.

Kuna wengine wanajua a-z na ripoti zinawafikia wanasiasa, lakini wanasiasa wetu hawana uwezo wa ku act on intel reports, isipokuwa wana uwezo sana wa kuzipoliticize. Tulifanya ujinga pale tulipopeleka maamuzi yote chini ya wanasiasa ambao hawana uwezo, can you believe Sofia Simba ndio mmoja wa wakuu wa kisiasa wa idara hiyo, angalia rekodi yake kama kweli anastahili kuwa pale.
 
Hata tulete UWT toka wapi, kama kuna kiongozi wa hovyo 'hapo juu' kama ilivyo sasa hakuna jipya.

UWT wanajua mengi sana na wangeweza kusafisha hii nchi.

Ni mabingwa wa chabo, nani kalala na nani wapi hiyo ndio kazi waliyobaki nayo. Yanayobumburuka sasa hivi ni matokeo ya ujinga na upuuzi wa watawala wa Tz.

Walioharibu UWT ndio wako madarakani sasa hivi. Waliiharibu iwasaidie kuwachafua wengine. Sasa jamaa walishazoea 'kula nyama za watu', wanaendelea
 
shida ni kua Rais kazungukwa na watu ambao Jenerali Ulimwengu amewaita wapuuzi katika makala yake ya wiki iliopita.
Fikiri juu ya wasaidizi wafuatao wa MH.Kikwete.
Mzee Makamba Yusuph
TAMBWE Hiza
John Chiligati
Sophia Simba
kulikua na Kingunge Ngombare Mwiru
Mtoto wake Ridhwan
mkewe Mama Salma
...hao ndio wasaidizi na washauri wa Rais ,mkama mwenyekiti wa chama pia.
...Orodha ni ndefu mnaweza kuendelea, katika hali hiyo ya uteuzi wa Rais, UWT , wafanye nini ? wanaangalia tu, by the way wao kazi yao sikusaidia kazi za uteuzi za CCM, Kazi yao ni usalama wa Taifa na sikufuatilia mambo yao ndani ya chama, Bashe , MALISA, hao wote walikua na wajibu waKichama zaidi.
labda uteuzi wa Chenge.
 
shida ni kua Rais kazungukwa na watu ambao Jenerali Ulimwengu amewaita wapuuzi katika makala yake ya wiki iliopita.
Fikiri juu ya wasaidizi wafuatao wa MH.Kikwete.
Mzee Makamba Yusuph
TAMBWE Hiza
John Chiligati
Sophia Simba
kulikua na Kingunge Ngombare Mwiru
Mtoto wake Ridhwan
mkewe Mama Salma
...hao ndio wasaidizi na washauri wa Rais ,mkama mwenyekiti wa chama pia.
...Orodha ni ndefu mnaweza kuendelea, katika hali hiyo ya uteuzi wa Rais, UWT , wafanye nini ? wanaangalia tu, by the way wao kazi yao sikusaidia kazi za uteuzi za CCM, Kazi yao ni usalama wa Taifa na sikufuatilia mambo yao ndani ya chama, Bashe , MALISA, hao wote walikua na wajibu waKichama zaidi.
labda uteuzi wa Chenge.

Umemsahau February, BumbuliOne
 
One of the techniques that the Kikwete government is using to neutralize the legislature is to fill it with intelligence operatives masquarading as MPs!Do you know how many intelligence officers were MPs in the just concluded parliament? You guessed right.! kazi yao ni kulinda maslahi ya viongozi na sio ya Taifa.
 
One of the techniques that the Kikwete government is using to neutralize the legislature is to fill it with intelligence operatives masquarading as MPs!Do you know how many intelligence officers were MPs in the just concluded parliament? You guessed right.! kazi yao ni kulinda maslahi ya viongozi na sio ya Taifa.
========

Hakuna nchi iliyowahi kufanikiwa kwa kuwafanya wana usalama kuwa wanasiasa. Hawa watu kama wameelemishwa vizuri huwa wanaharibiwa akili zao za kawaida na kuvishwa fikira zisizokuwapo ili waweze kufanya kazi yao vizuri. Sasa ukiwafanya wanasiasa, unategemea nini?

Nimewaona wakituhumiana humo bungeni na serikalini na sasa tusubiri watakavyoanza kuripuana kwa risasi. Undumila kuwili umewatawala kila wakati - mara hao kwa Lowassa, asubuhi wako kwa JK, keshikutwa kwa Sitta. Na hakuna hata mara moja utawasikia wakizungumza juu ya maslahi ya wananchi. Lugha yao ni maslahi ya kundi lao na kiongozi wao. Tumeliwa.
 
Madudu mengi na ya hatari yanayotokea katika siasa za nchi yetu yanaashiria kuwa idara yetu ya Usalama wa Taifa imefika mwisho kiutendaji. Ebu ona:-

-Rais akamteua Chenge baada ya kuvunjwa kwa Baraza la mawaziri. Watu wakapiga kelele, yeye akakaidi. Baada ya muda mfupi akalazimika kumwondoa kwa aibu!

-Nape na Malisa wakavutana kuhusu uongozi wa UVCCM; Rais akawatosa wote na kumchukua Masauni. Amegundulika alifoji umri, akaondoka, lakini aibu ikabaki kwa Rais. Hakuna aliyewajibishwa katika idara ya Usalama.

-Sasa tunaambiwa Bashe si raia. Amekuwa katika nafasi nyingi ikiwamo NEC. Chiligati anasema walipitiwa tu. Wamepitiwa mangapi?

La kujiuliza, hivi tuna ile Idara ya Usalama wa Taifa au sasa ni Idara ya Uhasama wa Taifa? Kinachoonekana kujengeka sasa ni kuwa uhasama katika mahusiano ya watawala ni mkubwa sana. Leteni maoni ya nini mwisho wa uhasama huu.

Issue ya chenge na idara ya usalama wa taifa ina uhusiano gani?
Kufoji umri na idara usalama wa taifa vina uhusiano gaini?
Na suala la kutokuwa uraia lina uhusiano gani na idrara ya usalama wa taifa? Kwa nini huzungumzii idara ya uhamiaji ambayo ndio imepewa jukumu la masuala yote ya uhamiaji?

Should we please try to analyse things instead of jumping to conclusions?
 
Issue ya chenge na idara ya usalama wa taifa ina uhusiano gani?
Kufoji umri na idara usalama wa taifa vina uhusiano gaini?
Na suala la kutokuwa uraia lina uhusiano gani na idrara ya usalama wa taifa? Kwa nini huzungumzii idara ya uhamiaji ambayo ndio imepewa jukumu la masuala yote ya uhamiaji?

Should we please try to analyse things instead of jumping to conclusions?
========

Alah

Tumegusa kitumbua! Basi tupe Job Description ya Idara ya usalama wa Taifa.

Kwangu, kabla Rais hajateua mtu kwa nafasi kubwa kama ya Waziri Chenge au kabla hajapendekeza mtu kama Masauni kuingia kwenye Cental Committee, ilibidi Idara ya Usalama impe clearance kuwa watu hawa ni safi. Hata Idara iliposhindwa kufanya hivyo, vyombo vya habari vilipiga kelele (at least kwa case ya Chenge), na hapo bado idara ya Usalama iliendelea kulala usingizi mpaka Chenge mwenyewe alipoamua kujiuzuru. Kwa kuwa wewe waonekana ni upo idara hiyo, tuelimishe sisi wajinga tujue ni nini kazi ya idara hiyo ya usalama.
 
========

Alah

Tumegusa kitumbua! Basi tupe Job Description ya Idara ya usalama wa Taifa.

Kwangu, kabla Rais hajateua mtu kwa nafasi kubwa kama ya Waziri Chenge au kabla hajapendekeza mtu kama Masauni kuingia kwenye Cental Committee, ilibidi Idara ya Usalama impe clearance kuwa watu hawa ni safi. Hata Idara iliposhindwa kufanya hivyo, vyombo vya habari vilipiga kelele (at least kwa case ya Chenge), na hapo bado idara ya Usalama iliendelea kulala usingizi mpaka Chenge mwenyewe alipoamua kujiuzuru. Kwa kuwa wewe waonekana ni upo idara hiyo, tuelimishe sisi wajinga tujue ni nini kazi ya idara hiyo ya usalama.

Unaona sasa? Kwako wewe ndio unavyoona hivyo. Under what basis? can you support your argument au unaongea tuu. Mdau nakushauri ukasome kwanza Sheria ya Idara ya Usalama wa Taifa Na. 5 ya Mwaka 1996. Baada ya kusoma hiyo sheria ndio utajua mamlaka ya hiyo idara. Tusiongee tuu ili mradi tumeongea.
 
Madudu mengi na ya hatari yanayotokea katika siasa za nchi yetu yanaashiria kuwa idara yetu ya Usalama wa Taifa imefika mwisho kiutendaji. Ebu ona:-

-Rais akamteua Chenge baada ya kuvunjwa kwa Baraza la mawaziri. Watu wakapiga kelele, yeye akakaidi. Baada ya muda mfupi akalazimika kumwondoa kwa aibu!

-Nape na Malisa wakavutana kuhusu uongozi wa UVCCM; Rais akawatosa wote na kumchukua Masauni. Amegundulika alifoji umri, akaondoka, lakini aibu ikabaki kwa Rais. Hakuna aliyewajibishwa katika idara ya Usalama.

-Sasa tunaambiwa Bashe si raia. Amekuwa katika nafasi nyingi ikiwamo NEC. Chiligati anasema walipitiwa tu. Wamepitiwa mangapi?

La kujiuliza, hivi tuna ile Idara ya Usalama wa Taifa au sasa ni Idara ya Uhasama wa Taifa? Kinachoonekana kujengeka sasa ni kuwa uhasama katika mahusiano ya watawala ni mkubwa sana. Leteni maoni ya nini mwisho wa uhasama huu.

Badala ya kuuliza kama Usalama wa Taifa wapo wapi, pengine na sisi wenyewe tujiulize tupo wapi wakati nchi inaelekea pabaya.

Mie ninavyoiona Idara hiyo sio chombo cha kumulika kile kinachotendeka nchini pamoja na ukweli kwamba kama sikosei kazi yake kubwa ni kuhakikisha kwamba Taifa linaendelea kuwepo. Idara hiyo kwa kiwango kikubwa, kama ilivyo kwa vyombo vingine vya polisi, Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Uhamiaji na Magereza, inafanya kazi kwa ushirikiano na wananchi na hasa Wazalendo, kwa bahati mbaya ingawa sijui kama Idara hiyo ina watuimishi wangapi, lakini siamini kama wapo kila mahali.
 
Madudu yanayofanyika ambayo mtoa hoja anasema yangeshughulikiwa na Idara hiyo, yanaweza kuwa hayashughulikiwi kwa sababu ushirikishwaji wa wananchi yawezekana ni mdogo sana au haupo kabisa. Wananchi ambao ni pamoja na mtoa hoja wanakaa kimya pengine wakifikiri kwamba Idara na vyombo vingine vya usalama vitafanya kazi kwa kupiga ramli. Haiwezekani.
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom