Kufuta ushuru wa saruji: Changamoto za utekelezaji wake

HAPA tunaongelea USHURU WA SARUJI KUFUTWA, na serikali imefanya utafiti wa KINA kabla ya kusaini ITIFAKI YA UMOJA WA FORODHA WA AFRIKA MASHARIKI.

Hayo masuala mengine sio pahala pake; tunaweza kuanzisha Thread nyengine na kila moja ina majibu yake.

Net group solution, Deep Green, Meremeta, RITES, Richmond, Buzwagi, Ushirika wa Celtel na TTCL, na ubinafsishaji wa viwanda vya ngozi, nguo, mahoteli ya serikali, uuzaji wa nyumba za serikali zilikuwa na utafiti wa kina?
 
Kwa heshima na taadhima kubwa.

1. Hapa tunazungumzia SARUJI na Kuhusu ushuru wa Saruji kufutwa kwenye bidhaa hio.
2. Suala la TTCL, TRC, ATC, TICTS, TBL, TDL, NBC and what ever case you may know of; ni out of the THREAD. Ukitaka kuyazungumzia hayo, anzisha thread nyengine; tusitoke nje ya mada. Aidha, kila moja ya hizo ni different case scenario na kuna maelezo yake.
3.Mtu anapofanya maamuzi huwa hafanyi kwa kufanya OVERVIEW ANALYSIS ya mambo, kinachotakiwa ni INDEPTH ANALYSIS. Sasa kama kuna safari ndefu, ni kweli; hilo silikatai. Na Inapaswa ianze kwa watu wenye kubwabwaja kuthamini ANALYSIS, ambazo zinapelekea waamuzi kufanya maamuzi yalikuwa informed.
4. Mimi wala sijajiaibisha, kwani I have made my case; you want to encounter that; go ahead; ila iwe kwa HOJA. USIKURUPUKE TU; au ndio unafanya mambo KIJESHI JESHI [IDDI AMIN] kwa hiyo Uniform kwenye profile?

Umezungumzia indepth analysis wenzako wanakuuliza hayo maamuzi mabovu yalifanyiwa indepth analysis? unataka thread nyingine.

Jibu hoja, huna unaweza ukanyamaza, unaruhusiwa tu.
 
Makame,acha Boot licking isiyo na aibu. Acha kuonyesha sura yako ya kifisadi hadharani. unasema Bei ya simenti ni 50% ya 20,000/=? Naomba niambie duka linalouza Bei hiyo haraka ili nikanunue maana huku Kasulu bei ni zaidi sana ya hiyo. Hivi hamwoni aibu kujikomba? Kama Dr. Slaa alikuwa akiwadanganya watanzania basi msingezichakachua kura zake ili mwone kama angeshindwa kutekeleza hilo. Msitufanye watanzania wote ni wajinga na wajanja ni nyinyi tu wachakachuaji wakuu. Aibu kwenu na komeni kuwadhihaki watanzania wenye uchungu wa dhati na umasikini wa watanzania katikati ya utajiri uliotekwa nyara na manyang'au.
Mungu ibariki Tanzania.
 
USHURU WA SARUJI IAGIZWAYO KUTOKA NJE KWA SASA NI 25%; na VAt ni 18%.

ushuru umewekwa kwenye saruji ili kulinda uzalishaji wa viwanda vyetu vya ndani; kwani Saruji kutoka nje inaingia kwenye soko letu katika mazingiza ya ushindani usio halali. Nasema hivyo kwa sababu saruji izalishwayo nje na kuletwa kwenye soko letu inapata ruzuku huko itokako. Endapo Serikali itaruhusu saruji hio kuingia nchini bila ya kutozwa ushuru itakua na athari zifuatazo.

Mkuu unatambua ya kwamba hata sisi Tanzania tunatoa ruzuku katika malighafi mbalimbali kuanzia kwenye sekta ya kilimo mpaka viwanda na biashara. Kinadharia unachozungumza ni sahihi ila ni lazima utumie mzani, je faida za kufuta kodi na ushuru zinazidi hasara ya kufanya hivyo?


1. Uzalishaji wa ndani utadumaa na hatimaye kufa.
2. Ajira za ndani zitapotea.
3. Mapato ya serikali yatapotea (Both ya Ushuru na mapato ya ndani kutoka kwenye uzalishaji wa ndani).
4. Uzalishaji wa ndani ukifa; saruji iagizwayo kutoka nje itapandishwa bei; kwa kuwa itakuwa ishaua uzalishaji wa ndani; hivyo watakuwa na ukiritimba.

Huo ni upande mmoja wa shilingi. Upande mwingine unaweza kusema ya kwamba kuondolewa kwa ushuru na VAT kunaweza kuleta changamoto kwa wazalishaji wetu wa hapa nchini na kuwalazimu kufanya kazi kwa ufanisi zaidi ili waweze kupunguza gharama zao za uzalishaji na kuongeza uzalishaji wakati huo huo.

Pili, ni ajira kiasi gani ambazo zimetengezwa na viwanda vyetu? Angalia supply chain yote na pia katika mauzo ya mwisho.Je ajira hizi no bora? Kwa hapa ninamaanisha kwanza ni za muda (vibarua) au la, je zinafuata sheria za kazi za nchi hii? maslahi yake yakoje?
Kwa kutumia hoja hiyo hiyo ya kugeuza upande wa shilingi, je ni ajira ngapi ambazo zinaweza kutengenezwa kwa kufanya ujenzi uwe wa bei nafuu? Fikiria mafundi wote?, viwanda, maghala, majumba ya hudumu, makazi ya kudumu ambayo yote yanaweza kutengeneza ajira maradufu ya hivi viwanda "vyetu" vya Wazo Hill, Tanga na Mbeya.


KIMSINGI KUFUTA USHURU HAKUWEZI KUSHUSHA BEI YA SARUJI; bali kutaangamiza uzalishaji wa ndani, ajira, mapato na hatimaye kujengea mabepari wanaoagiza saruji kutoka nje MONOPOLY.

Kivipi? Kufuta ushuru kutapunguza gharama za uzalishaji na markup za wazalishaji zitapungua na hence bei ya saruji itashuka. Uzalishaji wa ndani utaangamia pale tu utakaposhindwa kuhimili vishindo vya kibiashara. Katika nyakati za utandawazi kama huu viwanda legelege kufa ni kitu cha kawaida kabisa na god forbid, kama vitakufa havitokuwa vya kwanza.

Usitumie misamiati bila ya kuifahamu, uwepo wa viwanda vichache vya saruji nchini ni classic case ya nguvu ya soko kuwepo kwa wazalishaji. Hawa mabwana maadam wako wachache wanaweza kukaa chini na kupanga bei wazitakazo (collusion) na kuishia kubehave kama wamoja (monopolist). Kwenye uagizaji wa saruji kutoka nje ikiwa taratibu na mikakati madhubuti itawekwa na kufuatwa then sioni ni jinsi gani wachache tu watavyofaidika, kwani hata hivyo hivi sasa ni wachache tu wanaofaidika kutokana na ownership ya viwanda vya saruji nchini.

Unajua pia majengo bora husaidia kukuza miji. Na kuna kitu kinaitwa property tax huku mijini ambacho kinatozwa mara baada ya tathmini ya thamani ya jengo na ukiwa na tembe hii ni sifuri. Kodi ya majengo itasaidia kuongeza mapato ya serikali


AIDHA

kufuta ushuru wa saruji ni kuenda kinyume na utekelezaji wa Itifaki ya Umoja wa Forodha ya Jumuiya ya Afrika Mashariki; hivyo kimsingi maanake ni kuelekea kujitoa kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Siyo rahisi kama unavyofikiri wewe ndugu yangu. Ni kweli itakiuka vipengele vya ushuru wa pamoja ila kumbuka ya kwamba hili bado ni zoezi linaloendelea kufanywa na sio kila kitu kiko cast in stone. Tunaweza kujenga hoja na kubadilisha matakwa ya vipengele vya Ushuru wa forodha.
Pia nitashangaa sana kama nchi za EAC zitaitenga Tanzania kwa sababu imeamua kuondoa ushuru kwenye saruji


Kwa kuhitimisha ndugu yangu, Slaa alivyosema kuondoa ushuru hakumaanisha kufunga milango kwa saruji kutoka nje. Azma yake kuu ilikuwa ni kupunguza gharama za uzalishaji wa saruji hapa nchini na hivyo kutoa unafuu kwenye bei ya mauzo.
 
Back
Top Bottom