Kufuta matokeo ya Mitihani ya Darasa la Saba ni matokeo ya kuwa na Chaguzi Feki

Ndg yangu hapa sikuungi mkono hata kidg!!!!

Historia ya udanganyifu ktk mitihani hapa nchini halijaanza Leo ña tunakosea saña kulihalalisha na kutoa lawama kwa Rais.. Rejea matokeo ya form four 2012
Je kwa Hoja yenu inamashiko???? Kwani mwaka huu pekee ndo haya yametokea??? Mbona tunasahau ya 2012 ambayo yalitikisa nchi na vijana wengi walijiua!!!

Hapa sababu ni nyingi sana huenda hii mnayoitetea ikawa ni maelezo tu kwenye Hoja kubwa tusijifanye ati ndo leo udnganyifu umeanza,,,, fuatiia historia tangu tujiondoe kwenye EALA educacional council mwaka 1971 tukaamua kuanzisha NECTA mwaka 1973 hebu jaribu kuona kama tangu miaka hyo je hatujawahi kushuhudia wizi wa mitihani!!! Ña je kma tulishuhudia chanzo ña sababu zilikuwa hizi mnazozisema Leo?????
Inawezekana una rekodi nzuri zaidi kuhusiana na wizi wa mitihani. Kwangu mimi, siwezi nikasema kama ni jambo ambalo nimewahi kufuatilia kwa umakini.

Ninachokumbuka kwa siku za nyuma, kumekuwepo kufutiwa mitihani kwa shule moja moja au hata baadhi ya wanafunzi. Sababu kubwa ilikuwa ni walimu wa shule kutaka shule zao zijenge majina mazuri na wakati fulani rushwa iliyokuwa ikitolewa na wazazi ili watoto wao wafaulu mitihani.

Sina uhakika, mama imewahi kutokea wilaya nzima kufutiwa mitihani yao! Kama wilaya nzima au karibu wilaya nzima inahusishwa na wizi wa mitihani, yawezekana kwa sasa, sababu siyo kama zile za zamani.

Ujumbe ulio mujimu ni kuwa kila mmoja aheshimu na kutii taratibu za kazi yake na siyo mtu.
 
Acha siasa zakipumbavu yani watu wavujishe mitihani alafu usingizie kua nikwasababu ya raisi magufuli tuache siasa zaajabu jpm chapa kaz watz wengi tunakuelewa unatupeleka pazur
Muda utaamua, wala usiwe na haraka
 
Kuhusu kulinganisha na ulichokisema cha chaguzi mbali mbali kwa upande Wa sekta ya elimu sizani kama Hoja yako inamashiko hapa ila tatzo hapo ni kulinda matumbo ya viongozi wakiwemo wakuu Wa shule,,, maofsa elimu ili wasifukuzwe ña pia kutafuta sifa hasa kuvutia wazaz kupeleka watt kwenye shule hzo hasa shule za private

Ktk hili walimu na viongozi wanatakiwa wazingatie saña ethics zao ktk taaluma husika pia walimu wanawajibu mkubwa saña Wa kuepukana na mambo kama hayo endapo watatimiza wajibu wao ña kutojikita kutegemea kuwaibia Mitihani watt wao.
Jamii nzima inahitaji iwe pamoja Ktk hili kwani walimu na viongozi wengne wanakimbia aibu ya kufanya vibaya hvyo wanajikuta wanaiba mitihani wakat wangeungana na jamii kuwaandaa watoto kufaulu rejea alichokifanya Rc Mtaka Wa Simiyu na wazazi Huwezi ukategemea mambo kama hayo kutokea
Kimsingi umekubaliana indirectly na mleta mada. Unaposema maofisa elimu wanogopa kufukuzwa (tena siku hizi unafukuzwa jukwaani kwenye mkutano wa kisiasa) huoni kwamba ndio msingi wa kauli ya mleta mada kwamba kiini cha yote haya ni utawala wa kibabe usio zingatia weledi wa kutaka kufanya analysis na assessment za vyanzo halisi vya wanafunzi na shule kwa ujumla kutokufanya vizuri?

Walimu, na maofisa elimu wajikite kutimiza wajibu wao kivipi wakati kuna suala la sera ambalo ni suala la kisiasa ndio linakua chanzo cha kuvuruga sio tu mifumo na taratibu za elimu bali kuvuruga taratibu nyingi za kiutumishi kwa kutaka matokeo mazuri ya haraka ili kupata political mileage?
 
Ndg yangu hapa sikuungi mkono hata kidg!!!!

Historia ya udanganyifu ktk mitihani hapa nchini halijaanza Leo ña tunakosea saña kulihalalisha na kutoa lawama kwa Rais.. Rejea matokeo ya form four 2012
Je kwa Hoja yenu inamashiko???? Kwani mwaka huu pekee ndo haya yametokea??? Mbona tunasahau ya 2012 ambayo yalitikisa nchi na vijana wengi walijiua!!!

Hapa sababu ni nyingi sana huenda hii mnayoitetea ikawa ni maelezo tu kwenye Hoja kubwa tusijifanye ati ndo leo udnganyifu umeanza,,,, fuatiia historia tangu tujiondoe kwenye EALA educacional council mwaka 1971 tukaamua kuanzisha NECTA mwaka 1973 hebu jaribu kuona kama tangu miaka hyo je hatujawahi kushuhudia wizi wa mitihani!!! Ña je kma tulishuhudia chanzo ña sababu zilikuwa hizi mnazozisema Leo?????
Inapofikia maafisa wa wilaya nzima kushirikiana kuiba mitihani unafikiri ni kwa sababu gani!?? Wana hofu nini juu ya matokeo...!!!? Je serikali kuu imeweka mazingira mazuri na maafisa hao wameshindwa kutekeleza wajibu wao wa kuwapatia elimu bora?? Au hali ni tete wanafunzi hawajui kusoma wala kuandika mahudhurio ni mabaya kutokana na sababu mbalimba na wakawa na hofu ya wilaya zao kushika mikia na kinachofata ni kutumbuliwa watumishi wote bila kuangalia sababu kwa kina!?? Mkuu waza zaidi ya hapa! Ndio maana mtoa mada kalinganisha matukio mengine ikiwa ni pamoja na ya uchaguzi...!!! Kwani hiyo miaka ya 2012 wakurugenzi na wasimamizi wa uchaguzi walikuwa wakikataa kupokea fomu za wagombea wa uchaguzi!????? Mawakala walikuwa wakizuiliwa waziwazi kama siku hizi....!!!! Kama maafisa hawa wanashangiliwa kwa ukiukwaji wa taratibu unadhani ni kipi kitafanyika kwa sekta nyingine!???
 
Ndg yangu hapa sikuungi mkono hata kidg!!!!

Historia ya udanganyifu ktk mitihani hapa nchini halijaanza Leo ña tunakosea saña kulihalalisha na kutoa lawama kwa Rais.. Rejea matokeo ya form four 2012
Je kwa Hoja yenu inamashiko???? Kwani mwaka huu pekee ndo haya yametokea??? Mbona tunasahau ya 2012 ambayo yalitikisa nchi na vijana wengi walijiua!!!

Hapa sababu ni nyingi sana huenda hii mnayoitetea ikawa ni maelezo tu kwenye Hoja kubwa tusijifanye ati ndo leo udnganyifu umeanza,,,, fuatiia historia tangu tujiondoe kwenye EALA educacional council mwaka 1971 tukaamua kuanzisha NECTA mwaka 1973 hebu jaribu kuona kama tangu miaka hyo je hatujawahi kushuhudia wizi wa mitihani!!! Ña je kma tulishuhudia chanzo ña sababu zilikuwa hizi mnazozisema Leo?????
Ni kweli udanganyifu umeanza siku nyingi. udanganyifu ni sehemu ya maisha ya baadhi ya binadamu katika jamii. Ndio maana ni wajibu wa serikali makini kuweka mifumo ambayo itawakatisha tamaa wadanganyifu waliopo, na kuwajenga wale ambao wangeweza kuwa wadanganyifu, na kuwaelekeza kwenye ukweli. kujenga utamaduni wa watu kuwajibika ipasavyo.

Hoja kubwa hapa ni kwamba haya yaliyofanyika yanaingia katika mfumo wa kiserikali zaidi, badala ya kuwa ni watu fulani mmoja mmoja. kimsingi haya mambo yalikuwa yanaishia kwa waalimu na waalimu wakuu, wasimamizi, na wanafunzi. sasa hivi mpaka yanafika kwa maafisa elimu? huo ni upande mmoja.

sisi hatuhalalishi kitu hapa, tunajenga hoja kutokana na uovu unaotokea katika sekta moja unavyoweza kuibukia katika sekta nyingine. kama unadhania kwamba yale yanayofanywa na serikali katika chaguzi, uhuni wa makusudi, yanaishia hapo hapo, basi tafakri upya.
 
waliopaswa kuwajibishwa.sio wale tu. chakushangaza yule profesa hadi muda huu yupp ofisini anadunda.
kwanza ni suala la motivation: unapo mpa motisha mwalimu mkuu tu na kuwaacha wengine tegemea malalamiko kwa hawa waliobaki mana nao ni binadamu kama huyo uliyempa "posho " ya madaraka. hawajitumi.
nidhamu kazin: tunaambiwa kila siku nidhamu imerejea hko makazini sawa na hilo ni la kinidhamu mbona mitihani yavuja na hao watumishi wenye nidhamu?
mwaka wa tatu bila kupandishwa mishahara wala posho?
 
Unasumbuliwa na Utapiamlo wewe.
Wahi Hospitali upewe orodha ya vyakula vya kurutubisha afya mwili wako ukikaidi Mirembe inakuita.
Ukitaka kuangamiza taifa lolote duniani huhitaji kutumia silaha za nuklia wala mabomu ya atomic. Njia nzuri ya kuangamiza taifa ni kuhariby mfumo wa elimu. Ruhusu "mbumbumbu" waonekane wamefaulu na wasonge mbele. Matokeo yyatajionyesha baada ya muda mbumbumbu hao wakishahitimu. Wagonjwa watawafia mikononi, majengo yataanguka mikononi mwa wahandisi, pesa zitapotea mikononi mwa wachumi, utu utapotea mikononi mwa viongozi wa dini, na haki itapotea mikononi mwa mahakimu. Kuchezea elimu ni kuangamiza taifa!.
 
Hii ndio point ya msingi ya mwanzisha uzi.
Tunatengeneza taifa la uongo,wizi,unafiki na utapeli.
Udanganyifu unaoratibiwa, kutekelezwa na kusimamiwa kwenye taasisi mbalimbali unatujengea misingi imara ya uhalifu unakaodumu kwenye jamii kwa muda mrefu sana!
 
Viongozi wetu ni wa kuwaangalia sana nimesikitika kusikia ofisa ambaye si ajabu alowahi kuwa mwalimu akisema lurudia mitihani bila kiwaandaa hakutawaathiri watoto eti kwa sababu wamesoma miaka saba. Hapo hapo nikasikia mtoto akisema amekuwa so frustrated kwa sababu alikaa kambi kabla ya mitihani .wote tunajua psychological preparation ilivyo muhimu tofauti na mkurugenzi anayotulisha he is supposed to know this kwani nae alipita huko. Jamani kabla ya mitihani huwa tunakesha ila si kwamba tunayosoma kwenye mkesha yanatokea kwenye exam ila mkesha ni muhimu sana kwa mtahiniwa
 
Back
Top Bottom