Kufungwa kwa kiwanda cha nyanya cha Dangote: Je, kuna kitu cha kujifunza Tanzania ya Viwanda?

mitale na midimu

JF-Expert Member
Aug 26, 2015
10,420
17,701
Dangote-Tomato-NAN.jpg

tomato.png

Dangote anafunga kiwanda cha nyanya baada ya kukosa malighafi.
Sasa anafanya mazungumzo na kampuni ya Kiitaliano ili ije Nigeria kulima nyanya kwa wingi ili apate uhakika wa malighafi za kiwanda chake cha Tomato paste.

Kwa nini Alifungua hicho kiwanda?
Kuna kipindi hapo nyuma kama ilivyotokea hapa nchini nyanya nigeria zilikuwa nyingi kupita kiasi na bei kushuka saana. Wito ukaja watu wajitokeze kwenye kuwekeza katika usindikaji wa nyanya ili zisioze na ziuzwe mahala mbalimbali.

Dangote alipoiona hiyo fursa, iliyochochewa na wanasiasa aliamua kuwekeza kiwanda kikubwa sana cha kuchakata nyanya. Akafikilia plan B ikitokea kuna upungufu akaajiri wakulima wadogowadogo walime nyanya zisaidie.

Baada ya kiwanda kufunguliwa nyanya zilizokuwepo ziliweza kutosha kulisha kiwanda hicho kwa wiki kadhaa tu, baadae zikawa hadimu.

Wakati hayo yakiendelea, Umbali kidogo tu na nigeria Ipo nchi ya Hispania ambayo nyanya ni bei che kiasi cha kutumiwa kwenye michezo ya kupondana. Hawezi kuagiza nyanya nje ya nchi kutokana na sheria ngumu, lkn jamaa wa ndani uwezo wao ni mdogo kuzalisha kulisha nyanya kiwanda hicho jamaa amejikuta kastack inabidi atafute muwekezaji wake aje amlimie.

Chanzo:Why Dangote Closed his Tomato Factory and Lessons you can Learn from It | Opinions.ng

Najaribu kuwaza kwa nia nyororo...

1:Je hii case tumejipangaje katika kukabili changamoto zetu ili viwanda vyetu viwe endelevu?
2:Nguvu kiasi gani tumeiweka kuimarisha wakulima ili viwanda vichanue na kudumu?
3:Je, Kuna somo lolote la kujifunza au mambo yako vizuri hadi sasa?


Wataalam wa mambo karibuni katika kutoa michango nufaishi.


Mitale na midimu
Katika tafakari njema ya viwanda japo ni muumini sugu wa Kilimo na teknohama.
 
Africa tunapenda kushushana tu sijui ni laana gani hii?
Anyway ushauri ktk namna ya sisi kujipanga ni km ifuatavyo ;

Kwanza kabisa serikali itenge bajeti ya kutosha ktk Kilimo tofauti na sasa hali ilivyo mbaya ,lengo ni kutoa ruzuku kwa wakulima ikibidi na pia kupunguza bei za bembejeo.

Pili elimu iwepo kuhusu fursa za Kilimo na mazingira yawe friendly ktk Kilimo ili vijana wengi wajiajiri huko.

Tatu serikali iweke kipaumbele ktk kukopesha wakulima kwa riba nafuu.

Nne masharti na sheria za uagizaji bidhaa ziendane na mazingira ya wakati husika ili kurahisisha uagizaji wa malighafi yasiyitoshereza.

TANO serikali iwekeze ZAIDI ktk Kilimo na sio miundo mbinu pekee.
Mwisho suala la kodi ktk sekta ya Kilimo na viwanda iwe ya kulipika kuliko kukomoana kulivyo sasa maana Kilimo na viwanda vinategemeana sana ktk kuimarika, thanks.
 
Sekta hii ingeimarishwa na wakulima wakapata warsha kadhaa ingekuwa suluhisho kubwa kwenye mambo ya ajira.
Kilimo ni ngumu kweli pale mkulima akishaivisha mazao yake naye hana uwezo wa kuuza atakako..vibano vinaanza huruhusiwi kuuza mazao nje. Bei ya ndani ndio hiyo, wakulima wamejikatia tamaa huko vijijini.
 
Sekta hii ingeimarishwa na wakulima wakapata warsha kadhaa ingekuwa suluhisho kubwa kwenye mambo ya ajira.
Kilimo ni ngumu kweli pale mkulima akishaivisha mazao yake naye hana uwezo wa kuuza atakako..vibano vinaanza huruhusiwi kuuza mazao nje. Bei ya ndani ndio hiyo, wakulima wamejikatia tamaa huko vijijini.
Kweli mkuu kuna ombwe kati ya mkulima na soko. Viwanda ambavyo vinategemea rasilimali za mashambani vikiimarika bila kuwepo na changamoto za upatikanaji wa hizo rasilimali na continuity ya upatikanaji wakulima watakuwa pazuri.
Kusingekuwa na kilio cha kuuza nje kama ndani pako vizuri.
 
Inawezekana pale bajeti kubwa ukipeleka kwnye kilimo ukachana na bobandia ambayo haina uwezo wakunufaisha hata 2%ya watanzania
 
Usiongelew viwanda vya tanzania ni ushuzi mtupu.
Wewe mbunge anakubia saloni ni kiwanda huyo mbunge au akili yake kaweka kwene masaburi.
Its a big joke.
 
Wachangiaji wengi wa hii thread naona mko bomba sana nami naongezea tu kwamba serikali ikiweke kilimo kama kipaumbele namba moja.

Iachane kwanza na hizi "White Elephant Projects" za kutafutia political kicks, ijali kwanza maendeleo ya watu kabla ya vitu.
 
Kilimo kitengewe bajeti kubwa na wataalamu wa kilimo wafanye kazi,sio kushinda ofisini wanachat wasap
Pumbavu wewe nawe unaongea nini? Li chama lenu si ndio linasema KILIMO siyo kipaumbele choke? Yaani nilivyo na hasira na ma CCM Mimi, naweza kuyaua yote!! Yanataka tuanze kwanza na viwanda malighafi itakuja yenyewe kwa kuangalia kiwanda kikichopo!
 
Pumbavu wewe nawe unaongea nini? Li chama lenu si ndio linasema KILIMO siyo kipaumbele choke? Yaani nilivyo na hasira na ma CCM Mimi, naweza kuyaua yote!! Yanataka tuanze kwanza na viwanda malighafi itakuja yenyewe kwa kuangalia kiwanda kikichopo!
ha ha ha,naona mkuu una frasteshen....
Vipi sementi haziuziki nini,maana nasikia kinjia cha kwenda msalani hapoi kwako kimeota nyasi....
 
ha ha ha,naona mkuu una frasteshen....
Vipi sementi haziuziki nini,maana nasikia kinjia cha kwenda msalani hapoi kwako kimeota nyasi....
Ngoja nimmalizie kumparura dadako aende akisafishe yuko hapa!!
 
Dangote-Tomato-NAN.jpg

tomato.png

Dangote anafunga kiwanda cha nyanya baada ya kukosa malighafi.
Sasa anafanya mazungumzo na kampuni ya Kiitaliano ili ije Nigeria kulima nyanya kwa wingi ili apate uhakika wa malighafi za kiwanda chake cha Tomato paste.

Kwa nini Alifungua hicho kiwanda?
Kuna kipindi hapo nyuma kama ilivyotokea hapa nchini nyanya nigeria zilikuwa nyingi kupita kiasi na bei kushuka saana. Wito ukaja watu wajitokeze kwenye kuwekeza katika usindikaji wa nyanya ili zisioze na ziuzwe mahala mbalimbali.

Dangote alipoiona hiyo fursa, iliyochochewa na wanasiasa aliamua kuwekeza kiwanda kikubwa sana cha kuchakata nyanya. Akafikilia plan B ikitokea kuna upungufu akaajiri wakulima wadogowadogo walime nyanya zisaidie.

Baada ya kiwanda kufunguliwa nyanya zilizokuwepo ziliweza kutosha kulisha kiwanda hicho kwa wiki kadhaa tu, baadae zikawa hadimu.

Wakati hayo yakiendelea, Umbali kidogo tu na nigeria Ipo nchi ya Hispania ambayo nyanya ni bei che kiasi cha kutumiwa kwenye michezo ya kupondana. Hawezi kuagiza nyanya nje ya nchi kutokana na sheria ngumu, lkn jamaa wa ndani uwezo wao ni mdogo kuzalisha kulisha nyanya kiwanda hicho jamaa amejikuta kastack inabidi atafute muwekezaji wake aje amlimie.

Chanzo:Why Dangote Closed his Tomato Factory and Lessons you can Learn from It | Opinions.ng

Najaribu kuwaza kwa nia nyororo...

1:Je hii case tumejipangaje katika kukabili changamoto zetu ili viwanda vyetu viwe endelevu?
2:Nguvu kiasi gani tumeiweka kuimarisha wakulima ili viwanda vichanue na kudumu?
3:Je, Kuna somo lolote la kujifunza au mambo yako vizuri hadi sasa?


Wataalam wa mambo karibuni katika kutoa michango nufaishi.


Mitale na midimu
Katika tafakari njema ya viwanda japo ni muumini sugu wa Kilimo na teknohama.
Kulaga uhangame nyanda chovaga ubhalange abhangi
 
Back
Top Bottom