Jagina
JF-Expert Member
- Jan 29, 2019
- 5,413
- 2,263
Mimi mpaka hivi sasa linaniuma suala la kufungiwa Bureau de changes hasa hizi za hapa Zanzibar. Bado nina masuali lukuki najiuliza kichwani mwangu ambayo siyapatii majibu.
Kila nikichunguza Zanzibar itanufaika vipi na ufungaji wa hizi Bureaux de change, sipati jawabu. Ina maana leo hii Serikali ya Muungano inataka dola zinazopatikana Zanzibar kutoka sekta ya utalii ambayo kimsingi si ya Muungano wazidhibiti wao kupitia Bureau de change yao ya posta?
Kwa tuliosoma utalii hili ni kinyume na matakwa ya utalii endelevu, na ni kinyume na Sera yetu ya Zanzibar ya Utalii kwa wote. Serikali yetu ya Mapinduzi ya Zanzíbar ina Sera nzuri ya Utalii kwa wote, sasa ikiwa mjasiriamali wa Bureaux de change anafungiwa duka lake maana yake yeye hatofaidika tena na mapato ya utalii. Katika hali hii ni sawa na kusema kwamba utalii wa Zanzibar hautomnufaisha tena mfanyabiashara huyu? Sasa je hatuoni kwamba tunapingana na Sera yetu ya utalii kwa wote!
Katika Utalii kuna kitu kinaitwa Tourism Leakage. Wataalamu wanaitafsiri “Leakage” kama ni kitu chochote kinachopelekea mapato ya utalii ya nchi moja kutoka nje ya mfumo wa kiuchumi wa nchi husika. Ni wazi kwamba uchumi si suala la Muungano, hivyo kuifanya Tanzania kuwa na chumi mbili tafauti. Sasa je dola inayopatikana Zanzibar kutokana na utalii sekta ambayo kimsingi si ya muungano ikitolewa nje ya mzunguko wa fedha na uchumi wa Zanzibar itaitwaje kama si Leakage hiyo.
Kwa ufupi, katika takwa moja la utalii endelevu ( sustainable tourism) ni kuajiri jamii inayozunguka utalii wenyewe (surrounding community) ili nayo inufaike na shughuli na mapato ya utalii. Sasa hatuoni kwamba kuzifunga bureau de changes za Zanzibar ambazo kimsingi zinamilikiwa na jamii ya kizanzibari ambao walipaswa kufaidika na utalii wa Zanzibar kwa njia moja ama nyengine na kuifuisha bureau de change ya posta ambayo si milki ya jamii ya Kizanzibari si ni kwenda kinyume na Sera yetu utalii kwa wote tu bali pia ni kwenda kinyume na matakwa ya utalii endelevu? Maana yake dola inayotokana na utalii wa Zanzibar kwa mfumo wa sasa itakwenda kuwanufaisha watu walio nje ya Zanzibar badala ya hawa Wazanzibari walio humu ndani.
Mwisho labda nitowe rai kwa Serikali yetu tunayoipenda ya Zanzíbar na kuitanabahisha kwamba si kila sera inayotungwa na Tanganyika ina maslaha na Zanzibar. Mazingira ya kiuchumi ya Zanzibar ni tafauti sana na mazingira ya kiuchumi ya Bara. Basi ifike wakati kila nchi iwe na sera zake za kifedha ( fiscal and monetary policies) pamoja na kuwa na central banks zake ili kila mmoja apange uchumi wake kwa mazingira ya nchi yake.
Kila nikichunguza Zanzibar itanufaika vipi na ufungaji wa hizi Bureaux de change, sipati jawabu. Ina maana leo hii Serikali ya Muungano inataka dola zinazopatikana Zanzibar kutoka sekta ya utalii ambayo kimsingi si ya Muungano wazidhibiti wao kupitia Bureau de change yao ya posta?
Kwa tuliosoma utalii hili ni kinyume na matakwa ya utalii endelevu, na ni kinyume na Sera yetu ya Zanzibar ya Utalii kwa wote. Serikali yetu ya Mapinduzi ya Zanzíbar ina Sera nzuri ya Utalii kwa wote, sasa ikiwa mjasiriamali wa Bureaux de change anafungiwa duka lake maana yake yeye hatofaidika tena na mapato ya utalii. Katika hali hii ni sawa na kusema kwamba utalii wa Zanzibar hautomnufaisha tena mfanyabiashara huyu? Sasa je hatuoni kwamba tunapingana na Sera yetu ya utalii kwa wote!
Katika Utalii kuna kitu kinaitwa Tourism Leakage. Wataalamu wanaitafsiri “Leakage” kama ni kitu chochote kinachopelekea mapato ya utalii ya nchi moja kutoka nje ya mfumo wa kiuchumi wa nchi husika. Ni wazi kwamba uchumi si suala la Muungano, hivyo kuifanya Tanzania kuwa na chumi mbili tafauti. Sasa je dola inayopatikana Zanzibar kutokana na utalii sekta ambayo kimsingi si ya muungano ikitolewa nje ya mzunguko wa fedha na uchumi wa Zanzibar itaitwaje kama si Leakage hiyo.
Kwa ufupi, katika takwa moja la utalii endelevu ( sustainable tourism) ni kuajiri jamii inayozunguka utalii wenyewe (surrounding community) ili nayo inufaike na shughuli na mapato ya utalii. Sasa hatuoni kwamba kuzifunga bureau de changes za Zanzibar ambazo kimsingi zinamilikiwa na jamii ya kizanzibari ambao walipaswa kufaidika na utalii wa Zanzibar kwa njia moja ama nyengine na kuifuisha bureau de change ya posta ambayo si milki ya jamii ya Kizanzibari si ni kwenda kinyume na Sera yetu utalii kwa wote tu bali pia ni kwenda kinyume na matakwa ya utalii endelevu? Maana yake dola inayotokana na utalii wa Zanzibar kwa mfumo wa sasa itakwenda kuwanufaisha watu walio nje ya Zanzibar badala ya hawa Wazanzibari walio humu ndani.
Mwisho labda nitowe rai kwa Serikali yetu tunayoipenda ya Zanzíbar na kuitanabahisha kwamba si kila sera inayotungwa na Tanganyika ina maslaha na Zanzibar. Mazingira ya kiuchumi ya Zanzibar ni tafauti sana na mazingira ya kiuchumi ya Bara. Basi ifike wakati kila nchi iwe na sera zake za kifedha ( fiscal and monetary policies) pamoja na kuwa na central banks zake ili kila mmoja apange uchumi wake kwa mazingira ya nchi yake.