Kufunguliwa kwa tawi la kiwanda cha Sino-Truck nchini Tanzania kutatatua changamoto ya usafirishaji wa mizigo

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
VCG111304600215.jpg

Fadhili Mpunji

Mwanzoni mwa mwezi Machi mwaka huu kampuni ya serikali ya China inayotengeneza malori aina ya Sino-Truck, imetangaza kufungua tawi la kiwanda chake nchini Tanzania, likianza kwa uwekezaji wenye thamani ya dola za kimarekani milioni 20, na kutoa ajira kwa watu 500. Hatua hii sio kama ni mwendelezo wa ushirikiano kati ya China na nchi za Afrika kwenye kuhamishia teknolojia barani Afrika, bali pia ni uwekezaji ambao manufaa yake yanasambaa kwenye maeneo mengi.

Kwa muda mrefu sasa malori yanayotumiwa nchini Tanzania ni yale yaliyotengenezwa barani Ulaya, na mengine machache ni yake yanayotoka nchini Japan. Katika miaka ya hivi karibuni malori kutoka China yameanza kuonekana barabarani yakisafirisha mizigo kutoka bandarini Dar es salaam kwenye katika mikoa ya mbalimbali, na hata nchi za jirani. Mwanzoni baadhi ya wamiliki wa malori walikuwa na wasiwasi kuhusu ubora wa malori hayo, lakini baada ya kuyatumia na kuona ubora wake malori hayo sasa yamekuwa na soko. Kwa hiyo kufunguliwa kwa kiwanda cha malori hayo nchini Tanzania, kutakuwa na manufaa mengi.

Kwanza, watanzania wanaolazimika kutumia fedha nyingi za kigeni kuagiza malori hayo kutoka nje, na kulipia fedha nyingi za usafirishaji na ushuru wa forodha, sasa wataweza kununua malori hayo nchini Tanzania. Hali hii sio tu kama itaisaidia Tanzania kuokoa fedha za kigeni, bali pia itawawezesha watanzania kuwa na njia mbalimbali za ununuzi wa malori hayo kwa msaada wa mabenki ya Tanzania, tofauti na kama malori hayo yangeagizwa kutoka nje.

Pili, katika hatua ya mwanzo, kampuni hiyo imetangaza kuanza kwa kuajiri watu 500. Pamoja na kuwa idadi hii ni ndogo, lakini ni wazi kuwa ajira kubwa kama hizi zinazotolewa na viwanda vikubwa mara nyingi huambatana na malipo mazuri, na huwa zinazalisha ajira nyingine nyingi ndogo ndogo. Bila shaka watakaoajiriwa kwenye kampuni hiyo wanaweza kuwa wateja wa biashara nyingine, wanaweza kuajiri watu wengine kama vile watumishi wa nyumbani na hata kuwa chanzo ya mapato kwa wengine, na pia kulipa kodi ya mapato kwa serikali. Kwa hiyo uwekezaji wa kampuni hii ni sawa na kinachoitwa kwa kiingereza ajira zenye “spillover effect”, yaani manufaa yake yanawagusa wengi na sekta nyingi.

Tatu, kuanzishwa kwa kampuni hii kunajibu kilio cha muda mrefu cha uwepo wa urari mbaya wa biashara kati ya China na Tanzania. Hadi sasa Tanzania inaagiza zaidi bidhaa kuliko inazouza China, na moja ya bidhaa hizo ni malori. Moja ya faida kubwa za kampuni hii kuanzisha kiwanda nchini Tanzania, ni kuwa urari mbaya wa biashara kwa Tanzania utapungua. Hili ni jambo lenye afya kwa uchumi wa Tanzania, na hata kwenye ushirikiano wa kidiplomasia na kiuchumi kati ya China na Tanzania.

Nne, tukumbuke kuwa kwa sasa serikali ya Tanzania inajitahidi kuhimiza utekelezaji wa sera ya viwanda, na kinachofanywa na kampuni hiyo ya China ni kuunga mkono sera ya ndani za Tanzania. Bila shaka mambo yanayoendana na utekelezaji wa sera hii, kama vile uhamishaji wa teknolojia na ujuzi kwa watu wa Afrika, vitapatikana kwenye uwekezaji huo.

Hali kama hii sio kama tu inaonekana nchini Tanzania, Uganda kupitia mpango wake wa BUBU, yaani Buy Ugandan, Build Uganda, tayari imeanzisha kiwanda cha magari kwa kushirikiana na kampuni ya China, magari ambayo tayari yanauzwa na kutumika. Mara zote China imekuwa inasema tunatakiwa kujenga dunia ya binadamu yenye hatma ya pamoja. Uwekezaji kama huu ukiendelea, bila shaka kutakuwa na mabadiliko makubwa sio tu kwenye sekta ya usafirishaji barani Afrika, bali pia kwenye maisha ya watu wa Afrika.
 
Hapo China imejitengenezea soko jipya ya kila kidude cha hilo Lori, hakuna kitakachotoka Tz, na mishahara, tutasikia kama si ya kiunyonyaji, na raia wa China wakijazwa kila idara.
Afrika ni ya kuliwa tu, hakuna urari wa biashara mpaka Waafrika tuzalishe wenyewe Kwa asilimia 100 na kuwauzia wa nje ya Afrika, sio ubia.
 
Safi
Mjapani ka dominate soko la Magari kadogo Afrika naona mchina kaamua kuteka soko la magari makubwa

Kwenye Magari naona Ulaya wameshindwa kuteka soko la Afrika

Mchina na Mjapani wamedhamiria
 
Hata matrekta ya kichina nayo yana ubora waanze kuyaasemble watapata pesa nyingi Sana
 
Nikisikia tu neno wachina mwili unasisimka. Nawaza tu hapo tumepigwa.

Pia hiyo Sino china wamewahi kunipiga kwenye Bima hamna kampuni hapo. Hao wachina wametege kwenye udhaifu. Wanaiibia tu serikali kupitia viongozi wasiowaaminifu
 
Safi
Mjapani ka dominate soko la Magari kadogo Afrika naona mchina kaamua kuteka soko la magari makubwa

Kwenye Magari naona Ulaya wameshindwa kuteka soko la Afrika

Mchina na Mjapani wamedhamiria
Wote ni ujinga.

Kwanini hatuwezi kutengeneza magari yetu wenyewe hadi tusubiri Mchina au Mjapani atuletee ya kwake?

Nyumbu iko wapi?
 

Fadhili Mpunji

Mwanzoni mwa mwezi Machi mwaka huu kampuni ya serikali ya China inayotengeneza malori aina ya Sino-Truck, imetangaza kufungua tawi la kiwanda chake nchini Tanzania, likianza kwa uwekezaji wenye thamani ya dola za kimarekani milioni 20, na kutoa ajira kwa watu 500. Hatua hii sio kama ni mwendelezo wa ushirikiano kati ya China na nchi za Afrika kwenye kuhamishia teknolojia barani Afrika, bali pia ni uwekezaji ambao manufaa yake yanasambaa kwenye maeneo mengi.

Kwa muda mrefu sasa malori yanayotumiwa nchini Tanzania ni yale yaliyotengenezwa barani Ulaya, na mengine machache ni yake yanayotoka nchini Japan. Katika miaka ya hivi karibuni malori kutoka China yameanza kuonekana barabarani yakisafirisha mizigo kutoka bandarini Dar es salaam kwenye katika mikoa ya mbalimbali, na hata nchi za jirani. Mwanzoni baadhi ya wamiliki wa malori walikuwa na wasiwasi kuhusu ubora wa malori hayo, lakini baada ya kuyatumia na kuona ubora wake malori hayo sasa yamekuwa na soko. Kwa hiyo kufunguliwa kwa kiwanda cha malori hayo nchini Tanzania, kutakuwa na manufaa mengi.

Kwanza, watanzania wanaolazimika kutumia fedha nyingi za kigeni kuagiza malori hayo kutoka nje, na kulipia fedha nyingi za usafirishaji na ushuru wa forodha, sasa wataweza kununua malori hayo nchini Tanzania. Hali hii sio tu kama itaisaidia Tanzania kuokoa fedha za kigeni, bali pia itawawezesha watanzania kuwa na njia mbalimbali za ununuzi wa malori hayo kwa msaada wa mabenki ya Tanzania, tofauti na kama malori hayo yangeagizwa kutoka nje.

Pili, katika hatua ya mwanzo, kampuni hiyo imetangaza kuanza kwa kuajiri watu 500. Pamoja na kuwa idadi hii ni ndogo, lakini ni wazi kuwa ajira kubwa kama hizi zinazotolewa na viwanda vikubwa mara nyingi huambatana na malipo mazuri, na huwa zinazalisha ajira nyingine nyingi ndogo ndogo. Bila shaka watakaoajiriwa kwenye kampuni hiyo wanaweza kuwa wateja wa biashara nyingine, wanaweza kuajiri watu wengine kama vile watumishi wa nyumbani na hata kuwa chanzo ya mapato kwa wengine, na pia kulipa kodi ya mapato kwa serikali. Kwa hiyo uwekezaji wa kampuni hii ni sawa na kinachoitwa kwa kiingereza ajira zenye “spillover effect”, yaani manufaa yake yanawagusa wengi na sekta nyingi.

Tatu, kuanzishwa kwa kampuni hii kunajibu kilio cha muda mrefu cha uwepo wa urari mbaya wa biashara kati ya China na Tanzania. Hadi sasa Tanzania inaagiza zaidi bidhaa kuliko inazouza China, na moja ya bidhaa hizo ni malori. Moja ya faida kubwa za kampuni hii kuanzisha kiwanda nchini Tanzania, ni kuwa urari mbaya wa biashara kwa Tanzania utapungua. Hili ni jambo lenye afya kwa uchumi wa Tanzania, na hata kwenye ushirikiano wa kidiplomasia na kiuchumi kati ya China na Tanzania.

Nne, tukumbuke kuwa kwa sasa serikali ya Tanzania inajitahidi kuhimiza utekelezaji wa sera ya viwanda, na kinachofanywa na kampuni hiyo ya China ni kuunga mkono sera ya ndani za Tanzania. Bila shaka mambo yanayoendana na utekelezaji wa sera hii, kama vile uhamishaji wa teknolojia na ujuzi kwa watu wa Afrika, vitapatikana kwenye uwekezaji huo.

Hali kama hii sio kama tu inaonekana nchini Tanzania, Uganda kupitia mpango wake wa BUBU, yaani Buy Ugandan, Build Uganda, tayari imeanzisha kiwanda cha magari kwa kushirikiana na kampuni ya China, magari ambayo tayari yanauzwa na kutumika. Mara zote China imekuwa inasema tunatakiwa kujenga dunia ya binadamu yenye hatma ya pamoja. Uwekezaji kama huu ukiendelea, bila shaka kutakuwa na mabadiliko makubwa sio tu kwenye sekta ya usafirishaji barani Afrika, bali pia kwenye maisha ya watu wa Afrika.

Sino-Truck ili kufahamu uimara wake kopesheni wateja na wekeni bei hadharani mwisho vipuri tengeneseeni hapa TZ na sio kuunganisha magari tu​

 
I like that. Ila wasije kutuuzia malori hayo bei sawa na ukiagiza china.
 
Hapo China imejitengenezea soko jipya ya kila kidude cha hilo Lori, hakuna kitakachotoka Tz, na mishahara, tutasikia kama si ya kiunyonyaji, na raia wa China wakijazwa kila idara.
Afrika ni ya kuliwa tu, hakuna urari wa biashara mpaka Waafrika tuzalishe wenyewe Kwa asilimia 100 na kuwauzia wa nje ya Afrika, sio ubia.
Sasa kama vitambaa vya kufuta jasho bado mnaagiza ng'ambo waacheni wenye akili wawanyonye
 
Sasa kama vitambaa vya kufuta jasho bado mnaagiza ng'ambo waacheni wenye akili wawanyonye
Kabisa! Na cha ajabu, kuna kipindi, hasa cha Nyerere, tulijaribu na angalau tukawa na viwanda, sijui ujasiri ulee uliishia wapi?
 
Back
Top Bottom