Kuna jamaa mmoja namfahamu yeye alianza kwa kuwa na wazo kama wewe! Bahati nzuri yeye alikuwa alianza kwa kufanya home tution, alikuwa anawafuata wanafunzi majumbani kulingana na muda aliowapangia. Baada ya muda mzazi mmoja alijitolea darasa ambalo lilianza kutumika kwa kujumuisha watoto wengine wa majirani. Baada ya muda kupitia network ya wazazi wa watoto aliokuwa akifundisha akabahatika kukodishwa eneo ambalo Tution Centre ilikuja kuzaa shule ya secondary ( Sitapenda kuitaja hiyo seconday kwa sababu watu humu wataanza kashfa huku waki associate na shule za kata). But secondary yake inafanya vizuri na ni ya bweni.
Nafikiri kwa hakika mawazo ya mwana hapo chini ndiyo wengi walioanzisha shule bila mtaji walivyofanya mimi nawafahamu watu zaidi ya wawili walionza na tution sasa ni shule, inategemea tu una malengo gani tena mwingine ninaye mfahamu si mwalimu by profession ila amesoma tu language (english) pale Udsm.
amini unaweza kama nia but also wengine hutafuta wadhamini ambao upenda kuwekeza kwa Elimu kisha wewe wakusanye wataaluma wenzio mpange jinsi ya kuanza
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.