Kufukuzwa kazi kamanda wa meli Marekani na unafiki wa Marekani kuhusu uhuru wa kutoa maoni.

BUSH BIN LADEN

JF-Expert Member
Mar 16, 2019
7,607
17,072
Ilikuwa jana 2/4/2020 ambapo zilizuka taarifa za maambukizi ya Covid19 kwenye meli vita ya kubeba ndege ya jeshi la Marekani USS Theodore Roosevelt iliyoko Pacific.

Taarifa hizi zilitolewa na kamanda wa meli hiyo Kapteni Brett Crozier katika barua aliyoiandika akilishutumu jeshi la wana maji la nchi hiyo kutofanya vya kutosha kuwalinda na kuwaokoa wanajeshi wake wanaokufa wakati hawako vitani.

Banda ya barua yake iliyoandikwa 30/03/2020 kuvuja kwa vyombo cya habari, Thomas Modly anayekaimu uongozi wa jeshi la wanamaji ameamua kumtoa kazini kwa madai kwamba barua ya kapteni Crozier ilijenga picha miongoni mwa wengi kwamba jeshi na serikali ya nchi hiyo haifanyi chochote kuwalinda askari wake.

Hii imezua sintofahamu miongoni mwa wamarekani na mataifa mengine kuhusu uhuru wa maoni na kuweka uwazi taarifa zinazohusu janga hili la Corona.

Marekani na nchi nyingi za magharibi zimekuwa zikiilaumu China kuhusu kutotoa taarifa za kina kuhusu corona na kutowajibika hali iliyosababisha gonjwa hili kuenea sana Ila pia wameilaumu serikali ya China ilipomchukulia hatua za kinidhamu daktari wa China alietoa taarifa za mwanzoni kabisa kuhusu corona.

Swali la kujiuliza ni vipi Marekani waliona kitendo alichofanyiwa daktari wa China hakikuwa sahihi ila wao walichomfanyia kamanda wao ni sahihi.

Za kuambiwa changanya na za kwako, kitu kuwa sahihi au kinyume chake muda mwingine inategemea na hali sio uhalisia.

Naomba kuwasilisha
 
..kisa cha huyo Kapteni hakihusiani na uhuru wa kutoa habari.

..Uhuru wa kutoa habari anao na ndiyo maana hata sisi tulioko Afrika tunajua changamoto alizokutana nazo.

..mimi nadhani suala hili linahusu UZALENDO.

..Je, uzalendo ni kwa NCHI au uzalendo ni kwa serikali au Raisi?

..Kwa maoni yangu Kapteni ameamua kuwa mzalendo kwa NCHI kwa kuwatetea askari ambao amepewa dhamana kuwaongoza.

..Vyombo vya habari navyo viko mstari wa mbele kumtetea Kapteni badala ya kukaa kimya na kumuacha peke yake akisakamwa na serikali.

..Hili ni somo kubwa kwa Watanzania. Tusimame upande wa KWELI. Na uzalendo siyo kwa ccm, raisi, serikali. Uzalendo ni kwa NCHI / TANZANIA.
 
..kisa cha huyo Kapteni hakihusiani na uhuru wa kutoa habari.

..Uhuru wa kutoa habari anao na ndiyo maana hata sisi tulioko Afrika tunajua changamoto alizokutana nazo.

..mimi nadhani suala hili linahusu UZALENDO.

..Je, uzalendo ni kwa NCHI au uzalendo ni kwa serikali au Raisi?

..Kwa maoni yangu Kapteni ameamua kuwa mzalendo kwa NCHI kwa kuwatetea askari ambao amepewa dhamana kuwaongoza.

..Vyombo vya habari navyo viko mstari wa mbele kumtetea Kapteni badala ya kukaa kimya na kumuacha peke yake akisakamwa na serikali.

..Hili ni somo kubwa kwa Watanzania. Tusimame upande wa KWELI. Na uzalendo siyo kwa ccm, raisi, serikali. Uzalendo ni kwa NCHI / TANZANIA.

idd amin aliwahi kusema “naweza kuwahakikishieni kuwa mna uhuru wa kujieleza lakini siwezi wahakikishieni uhuru baada ya kujieleza”


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ilikuwa jana 2/4/2020 ambapo zilizuka taarifa za maambukizi ya Covid19 kwenye meli vita ya kubeba ndege ya jeshi la Marekani USS Theodore Roosevelt iliyoko Pacific.

Taarifa hizi zilitolewa na kamanda wa meli hiyo Kapteni Brett Crozier katika barua aliyoiandika akilishutumu jeshi la wana maji la nchi hiyo kutofanya vya kutosha kuwalinda na kuwaokoa wanajeshi wake wanaokufa wakati hawako vitani.

Banda ya barua yake iliyoandikwa 30/03/2020 kuvuja kwa vyombo cya habari, Thomas Modly anayekaimu uongozi wa jeshi la wanamaji ameamua kumtoa kazini kwa madai kwamba barua ya kapteni Crozier ilijenga picha miongoni mwa wengi kwamba jeshi na serikali ya nchi hiyo haifanyi chochote kuwalinda askari wake.

Hii imezua sintofahamu miongoni mwa wamarekani na mataifa mengine kuhusu uhuru wa maoni na kuweka uwazi taarifa zinazohusu janga hili la Corona.

Marekani na nchi nyingi za magharibi zimekuwa zikiilaumu China kuhusu kutotoa taarifa za kina kuhusu corona na kutowajibika hali iliyosababisha gonjwa hili kuenea sana Ila pia wameilaumu serikali ya China ilipomchukulia hatua za kinidhamu daktari wa China alietoa taarifa za mwanzoni kabisa kuhusu corona.

Swali la kujiuliza ni vipi Marekani waliona kitendo alichofanyiwa daktari wa China hakikuwa sahihi ila wao walichomfanyia kamanda wao ni sahihi.

Za kuambiwa changanya na za kwako, kitu kuwa sahihi au kinyume chake muda mwingine inategemea na hali sio uhalisia.

Naomba kuwasilisha
Capten alifanya jambo jema sema, huyo Ps aliyevujisha barua kwenye Media ndo kamuharibia, ila nachoamini hapo Trump na majenerali wake wamejikaanga maana kamati ya Senate na Bunge zitawahoji tu wahusika
 
Capten alifanya jambo jema sema, huyo Ps aliyevujisha barua kwenye Media ndo kamuharibia, ila nachoamini hapo Trump na majenerali wake wamejikaanga maana kamati ya Senate na Bunge zitawahoji tu wahusika
Yep na ninasikia hadi jamaa kaandika barua askari 100 walikuwa tayari na maambukizi na hamna action yoyote Navy walikuwa wamechukua
 
Back
Top Bottom