Sungi
Senior Member
- Apr 29, 2009
- 149
- 47
Vyama vya siasa Tanzania vimekuwa vikifukuza wanachama wao wa ngazi mbalimbali pale viongozi hawa wanapokaidi au kwenda kinyume na itikadi ya chama husika. Lakini nadhani swali la msingi hapa ni kwamba, hawa viongozi, hasa wabunge, wanakuwa wamechaguliwa na wananchi na pengine sio tu na wanachama wa vyama wanavyotoka. Utaratibu huu wa kufukuza uachama viongozi, eti kwa kwenda kinyume na itikadi ya vyama unaendelea kudidimiza democrasia na kuwafanya viongozi wawe watumwa kwa vyama vya siasa na ukiritimba na "wakubwa" wa vyama kwa kuhamisha nguvu ya wananchi kuchagua viongozi wanaowafaa. Hii ni sababu nyingine, katiba yetu mpya iwe na vipengere vya "right to recall" kurudisha nguvu ya kuwaondoa wabunge ambao wananchi hawaridhiki na utendaji wao wa kazi. Kutoa haki ya wagombea huru (binafsi) kuweza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi pia itasaidia kuwapa wabunge uwezo wa kutetea maslahi ya wananchi wao bila ya kuwa na woga wa kufukuzwa chamani na hatimaye kupoteza nafasi zao za uongozi na hasa bungeni.