Kufikiria kwamba kujua kuongea lugha ya kigeni ni ufahari sana, ni aina ya utumwa karne hii

Seif Kazige Mbambizi

Senior Member
May 7, 2016
135
92
Suala la matamshi katika lugha sio jambo tunaloweza kulifanya mjadala katika nchi kama hii ambayo bado inasumbuliwa na shida nyingi. Isitoshe tatizo la kuelewa au kutokuelewa lugha flani ni suala binafsi sana ambalo hatupaswi kulifanya kama mada ya siku au mjadala wa kitaifa kwasababu kiongozi anaeongoza Tanzania ni mswahili na lugha ya taifa ni kiswahili hivyo akitumia lugha ya kigeni kufikisha ujumbe kwa wahusika ni wazi kwamba watauelewa tu kwasababu wanajua watanzania lugha yao kuu ni kiswahili. Ukiacha kiingereza wapo viongozi wengine hawafahamu lugha ya Kiswahili, kichina, kifaransa, kihindi, kiarabu, kigiriki, kihosa, kingoni, kichaga, kizigua, kihaya n.k hata wakija hapa nchini wanajitahidi kuongea kiswahili lakini kwa makosa na bado tunaelewa nini walitaka kutuambia. Tuache fikra potofu kwamba kujua kuandika au kuongea kingereza ni ufahari sana.
Lugha yoyote ya kigeni ni njia tu ya mawasiliano sio sifa ya mtu flani kuwa kiongozi mzuri.
 
Hii mitazamo ndio iliyopelekea kuanzishwa kwa shule za kimataifa...zenye ada za ajabu,
Ilu nyie wenye mitazamo ya lugha ya taifa and sh@#$ msutuharibie watoto wetu....

Endeleeni kuongea kiswahili chenu huko Ulongoni... Na kazi mtasubiria halmashauri ya Bamtumbo

Total Ignorance bliss ....
 
nani alikwambia kuwa kiingeleza ni lugha ya kigeni kwa Tanzania? hiyo ni lugha rasmi kwa Tanzania kutokujua kiingeleza hakuifanyi ionekane ni lugha ya kigeni. ebu pitia hapa uondoe ujinga kidogo.

Tanzania
Bado tumetawaliwa na maneno ya lugha ya kiingereza wakati tunaishi maisha ya kiswahili.
 
Pathetic fool! Maneno ya mtu aliyeshindwa kuongea Kiingereza na sasa anajifariji. Tunapoenda kuomba kazi, moja ya vigezo vinavyoainishwa ni fluency in English. Kama una mtu unataka kumfurahisha, endelea na jukumu lako, ila kama unawapenda watoto wako na hutaki waje kufagia barabara kama mimi, wapeleke shule inayofundisha Kiingereza
 
Hii mitazamo ndio iliyopelekea kuanzishwa kwa shule za kimataifa...zenye ada za ajabu,
Ilu nyie wenye mitazamo ya lugha ya taifa and sh@#$ msutuharibie watoto wetu....

Endeleeni kuongea kiswahili chenu huko Ulongoni... Na kazi mtasubiria halmashauri ya Bamtumbo

Total Ignorance bliss ....
Wanafunzi wahaendi shule kusoma Lugha za kimataifa isipokuwa wanakwenda kupata mbinu na maarifa kwa lengo la kubadilisha fikra zao duni na kuzifanya kuwa fikra za kisasa. Maarifa hayo yanaweza kumfikia mwanafunzi hata kwa lugha ya kizigua na akawa daktari mzuri kama yule ambae maarifa hayo aliyapata kwa lugha ya Kichina, kifaransa ama kiingereza. Lugha ni njia ya kuwasiliana na sio maarifa ya kitaaluma
 
Suala la matamshi katika lugha sio jambo tunaloweza kulifanya mjadala katika nchi kama hii ambayo bado inasumbuliwa na shida nyingi. Isitoshe tatizo la kuelewa au kutokuelewa lugha flani ni suala binafsi sana ambalo hatupaswi kulifanya kama mada ya siku au mjadala wa kitaifa kwasababu kiongozi anaeongoza Tanzania ni mswahili na lugha ya taifa ni kiswahili hivyo akitumia lugha ya kigeni kufikisha ujumbe kwa wahusika ni wazi kwamba watauelewa tu kwasababu wanajua watanzania lugha yao kuu ni kiswahili. Ukiacha kiingereza wapo viongozi wengine hawafahamu lugha ya Kiswahili, kichina, kifaransa, kihindi, kiarabu, kigiriki, kihosa, kingoni, kichaga, kizigua, kihaya n.k hata wakija hapa nchini wanajitahidi kuongea kiswahili lakini kwa makosa na bado tunaelewa nini walitaka kutuambia. Tuache fikra potofu kwamba kujua kuandika au kuongea kingereza ni ufahari sana.
Lugha yoyote ya kigeni ni njia tu ya mawasiliano sio sifa ya mtu flani kuwa kiongozi mzuri.
Hata hiyo simu uliyoyumia kuandika huu upunguani hapa,ni Lugha ya kigeni ndo inakuongoza kilakitu.
 
Kujua Kiingereza ni takwa la lazima katika ulimwengu huu wa sasa.Kama hukijui jitahidi umwone Ras Simba.
 
Pathetic fool! Maneno ya mtu aliyeshindwa kuongea Kiingereza na sasa anajifariji. Tunapoenda kuomba kazi, moja ya vigezo vinavyoainishwa ni fluency in English. Kama una mtu unataka kumfurahisha, endelea na jukumu lako, ila kama unawapenda watoto wako na hutaki waje kufagia barabara kama mimi, wapeleke shule inayofundisha Kiingereza
Bado unawafundisha watoto wako mpaka sasa kwamba wakimaliza shule watakwenda kuajiriwa? Acha kabisa mawazo hayo yakitumwa, wafundishe kwamba watakapo maliza masomo yao watumie maarifa waliyopata kujiajiri na sio kutegemea ajira za kutembea na bahasha
 
Bado unawafundisha watoto wako mpaka sasa kwamba wakimaliza shule watakwenda kuajiriwa? Acha kabisa mawazo hayo yakitumwa, wafundishe kwamba watakapo maliza masomo yao watumie maarifa waliyopata kujiajiri na sio kutegemea ajira za kutembea na bahasha

Wewe una mawazo mafupi mafupi ya ujasiriamali. Ukitaka kuwa mwekezaji huwezi kuwaza matope. Kama umekimbia kutembea na bahasha sababu ya kuogopa lugha, ukiwa mwekezaji wenye bahasha watakutembelea, tafuta mkalimani au ishia kuuza kalimati.
 
Hii yooote ni kumtetea "on behalf of myself"

Anakutieni ujinga, halafu mnawashangaa na kuwadharau waliokuwa wanawabeba wazungu.
 
Wewe una mawazo mafupi mafupi ya ujasiriamali. Ukitaka kuwa mwekezaji huwezi kuwaza matope. Kama umekimbia kutembea na bahasha sababu ya kuogopa lugha, ukiwa mwekezaji wenye bahasha watakutembelea, tafuta mkalimani au ishia kuuza kalimati.
Ukishakuwa umetawaliwa kifikra basi unakuwa mtumwa wewe mpaka vitukuu vyako.
 
Back
Top Bottom