mkulimamiwa
JF-Expert Member
- Mar 4, 2025
- 2,440
- 4,857
Mwaka huu huwenda ukawa ni mwaka mgumu sana kutekeleza haki zetu za kikatiba za mwananchi kwenda kupiga kura
Nchi nzima imetaharuki, sijawahi kuona wanajeshi na majeshi mengine kufanya mazoezi kama ilivyo sasa tena tu ni kwa ajili ya uchaguzi
Ukweli ni kuwa, magwanda ya wenzetu hawa, yanatosha kabisa kutaharukisha wananchi hasa kwetu sisi wa vijijini huku
Mazoezi yanayofanyika sasa tunapoelekea uchaguzi, binafisi yananifanya niogope hata kwenda kupiga kura yenyewe
Jambo hili si kwangu tuu, kijijini kwetu huku, kila mwananchi anahofia jambo hili, mambo haya mawili, ya majeshi kufanya mazoezi na tishio la maandamano, ki ukweli kabisa, serikali ifikirie namna nzuri ya kutoa elimu zaidi ili kuondoa hofu kwetu wapiga kura
Mi nadhani, Jeshi lingefanya mazoezi ya kificho ili wananchi tusijae hofu kama ilivyo sasa
Kwa namna ilivyo sasa, inakuwa ni vigumu sana kujitokeza kwenda kupiga kura, kwa sababu, hofu ya kwanza ni juu yao hawa wanaofanya mazoezi yaani, (Majeshi) na kwambaa, ikitokea hawa waandamanaji wakajitokeza, wataweza kumtambua mtu mwema na muovu? Au tutapigwa wote bila kujali mimi nilienda kupiga kura?
Nchi nzima imetaharuki, sijawahi kuona wanajeshi na majeshi mengine kufanya mazoezi kama ilivyo sasa tena tu ni kwa ajili ya uchaguzi
Ukweli ni kuwa, magwanda ya wenzetu hawa, yanatosha kabisa kutaharukisha wananchi hasa kwetu sisi wa vijijini huku
Mazoezi yanayofanyika sasa tunapoelekea uchaguzi, binafisi yananifanya niogope hata kwenda kupiga kura yenyewe
Jambo hili si kwangu tuu, kijijini kwetu huku, kila mwananchi anahofia jambo hili, mambo haya mawili, ya majeshi kufanya mazoezi na tishio la maandamano, ki ukweli kabisa, serikali ifikirie namna nzuri ya kutoa elimu zaidi ili kuondoa hofu kwetu wapiga kura
Mi nadhani, Jeshi lingefanya mazoezi ya kificho ili wananchi tusijae hofu kama ilivyo sasa
Kwa namna ilivyo sasa, inakuwa ni vigumu sana kujitokeza kwenda kupiga kura, kwa sababu, hofu ya kwanza ni juu yao hawa wanaofanya mazoezi yaani, (Majeshi) na kwambaa, ikitokea hawa waandamanaji wakajitokeza, wataweza kumtambua mtu mwema na muovu? Au tutapigwa wote bila kujali mimi nilienda kupiga kura?