Kufanya kazi kwa wahindi bila kujipendekeza na kuwa mnafiki inawezekana kweli?

Kufanya kazi kwa wahindi bila kujipendekeza na kuwa mnafiki inawezekana kweli?

Nashukuru sijawahi kuajiriwa na Wahindi ila kuna ndugu zangu wamefanya kazi na wahindi haki niliapa sitakuja kufanya kazi nao. Bora nikalime mahindi, tikiti maji au nyanya
 
Mh. Inategemea sasa na wahindi wenyewe.. kwasababu watu wanatofautiana... Mimi nilishawahi kufanya kazi kwa muhindi muislam na alikuwa poa kabisa. Anaongea kiswahili kimenyooka anajua ata kiswahili cha mtaani. Ipo siku alipigiwa simu na mteja wake muhindi mbaniyani akaanza kumfokea kwa kihindi. Mm na umbeya wangu nkamuuliza boss wng mm nkajua wahindi wanatufokeaga sisi tu kumbe na nyie mnafokewa.. akanijib kwamba yy ni muhindi wa Tz kwamba familia yake nzima kuanzia mababu na mabibi wamezaliwa huku kwahyo yy ni mbongo kabisa.. na wahindi wengi hua na ubaguzi sio kwa muafrika tu Bali baina ya wao wenyewe pia.. akaniambia wahindi Kuna vikundi vingi.. Kuna muhindi mbongo na kuna muhindi wa India. Wengi wanadhali wahindi wote ni sawa lakini sio ukweli
 
Wahindi waduanzi Sana,ukiwa na hasira ni ngumu kufanya nao kazi yoyote Ile.
 
Jamaa yangu alipata kazi kwa wahindi january mwishon. Yuko vizuri sana kwa kile anachofanya, anajiamini na anaongea kiingereza kimenyooka kama rula. Ile ofisi wote ni wahindi... Last month kasimamishwa kazi kisa eti wafanyakazu wenzake hawataki kufanya kazi naye. Hao wenzake wote ni wahindi. Boss anamwambia unapiga kazi vzuri kuliko wote ila wamegoma hawataki kufanya kazi na wewe.
Wahindi ni Chupli Chupli sana.
 
Dah,huu uzi
Nimepata mchongo wa uhasibu kwenye kampuni flani ya mhindi,kampuni inajishughulisha na uuzaji wa machines na mitambo mbalimbali ya construction na mining. Picha limeanzia kwenye interview boss mkali kinoma,anakuuliza maswali kwa hasira,sasa kanitumia ujumbe WhatsApp jana kuwa nianze kazi leo,ila nimetafakari nimeona hapana,yule boss tutazinguana siku si nyingi tu,bora niendelee kupiga winga tu.
 
Vipi na hawa wa kilimanjaro wapoje kwenye kazi zao
 
Back
Top Bottom