Kufanikiwa kisiasa si upeo wa kudhalilisha Viongozi wa dini

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,883
6,884
Nakumbuka miongo kadhaa imepita tangu kutokee mtafaruku wa viongozi wawili mkoani Ruvuma kati ya Askofu na Mkuu wa mkoa. Askofu kilichomponza ni kumtaka Mkuu wa Mkoa kufuata maadili ya dini yake. Mkuu wa Mkoa alitaka aheshimiwe na Askofu kama Kiongozi asiyeguswa hata akienda kinyume cha maadili na miiko ya dini yake.

Mtafaruku huu ulipelekea mkuu wa mkoa kuonyesha mamlaka yake ya kidunia kwa kufunga hospitali kuu iliyokuwa ndio pekee mwambao wa ziwa nyasa huko Lituhi. Hakuishia hapo ila kuwahamisha wakazi wote wa hapo kwa kisingizio kwamba wako kando ya mto Ruhuhu ili kuwanusuru na mafuriko. Hata hivyo wachunguzi wa mambo walishangaa hoja hiyo kwa vile sehemu hiyo ni ya mwinuko na wengi tunavyojua mazingira kando ya ziwa nyasa yalivyo. Hayo yalitokea kipindi Cha Rais Mwinyi. Kitendo hicho kilimwuma sana Askofu huyo na waumini wa Mwambao na hata wakazi wengi wa Mkoa Ruvuma licha ya mkuu wa mkoa huyo kujenga jina zuri kwa mengi aliyotenda mkoani humo katika suala la maendeleo ya jumla.

Kwa waliokuwa karibu na askofu huyo walimsikia akisema, Mkuu wa mkoa aliyofanya bila kujali watu wake na huduma ya kanisa kwa kuwahamisha watu kwa lengo la kuonyesha mamlaka yake katika himaya yake kisiasa, kamwe hatakuwa na mafanikio makubwa kisiasa. Askofu huyo alifariki siku ambayo kulikuwa na sherehe za kitaifa Songea ambapo alialikwa kuwa mmoja wa wageni mashuhuri. Alisalimiana na Rais Mwinyi, kisha na mkuu wa Mkoa na jioni yake tulipata habari za mshtuko kwa Askofu huyo amefariki na kuacha simanzi kubwa kwa kuwa viongozi wengi kitaifa walikuwapo Songea. Amini usiamini, hayo yalitokea, kwani mkuu wa mkoa huyo alibaki kuhamishwa hamishwa na cheo cha juu alichojaribu kushika mambo hayakumwendea vema, hadi mauti yalipokumta hana cheo cho chote. Wengi walimlilia kwa maendeleo mbalimbali aliyofanya katika uhai wake licha ya kumwendea baba wa milele wakati bado nguvu za kimwili na kiakili zilikuwa zinahitajika kujenga taifa lake.

Yanayotokea Arusha si ya kudharau, maana ya hapa duniani yanapita, na hawa manabii wanachoongea ni sauti ya Mungu licha ya kuwa binadamu wenzetu. Tujue kwamba wametwaliwa kati ya watu ili wawahudumie watu katika mambo yamhusuyo Mungu. Tunapojibu kitu kwa hawa viongozi wa dini lets double check, or overlook what you going to respond to them. Usimjibu kama mwanasiasa mwezako kwa sababu kauli yako inaweza kuakisi maudhui yaliyo kinyume cha uadilifu katika maisha. Tukitanguliza heshima ya mtu ni bora kuliko onyesho la mamlaka ya tuliyo nayo ambayo yanapita na pengine yanaweza kutuharibia future yatu machoni mwa tunaowatumikia.
 
Kwa mtazamo wangu unyofu katika maisha husaidia kujenga mazingira mazuri ya maisha na hata utumishi. Lakini kujiona uko juu ya watu au kundi fulani ni kasumba ya kutaka kuonwa mtu wa pekee usiyejali wenzako iwe watumishi wenzako au unaowatumikia.
 
Kweli mkuu, viongozi wanapaswa kujua namna ya kusema na kila kundi la watu.huwezi kwa mfano kutumia lugha hiyo hiyo pale Nkurumah hall then ukaita wanahabari ukarudia yale yale lakini sasa ukitaka kuwagusa viongozi wa dini.Uongozi ni karama,na kiongozi ni mtu ambaye hata ukimtizama tu unajua huyu ni kiongozi,nakumbuka enzi hizo sekondari shule zetu zileee,hata kabla ya uchaguzi wa viongozi wa wanafunzi tulikuwa najua viongozi bora na watu wenye undumilakuwili alikuwa hapiti na hata walimu walikuwa makini kusaidia kupatikana vijana wa kuwaongoza wenzao.siku hizi mpaka ngazi ya kitaifa viongozi tunaletewa na kusomewa historia zao ili kutuvutia na idadi ya degree zao na hadhi ya vyuo walivyosoma,lakini walio bora historia yake haisomwi,mambo aliyofanyia nchi watu wanajua maana wengine unakuta wamefika hatua ya juu ya uongozi huko nyuma.ndio maana hekima na busara hakuna kwa viongozi,uzalendo(neno zito mno hili) hakuna,ujanja ujanja umejaa,watu wanapigwa risasi badala uwape pole wafiwa na kutoa mikakati ya serikali kumaliza tatizo anaropoka kuna chama kinachochea vurugu tena bila ushahidi na kiongozi huyu anadhani kila mahala ni pa kupiga propaganda za kisiasa! hii hulka lazima tuikemee,Kiafrika msibani tunaongea ya msiba na jinsi ya kutunza familia ya marehemu na si kuonesha ufahari,fahari vitani bana.
 
Kweli mkuu, viongozi wanapaswa kujua namna ya kusema na kila kundi la watu.huwezi kwa mfano kutumia lugha hiyo hiyo pale Nkurumah hall then ukaita wanahabari ukarudia yale yale lakini sasa ukitaka kuwagusa viongozi wa dini.Uongozi ni karama,na kiongozi ni mtu ambaye hata ukimtizama tu unajua huyu ni kiongozi,nakumbuka enzi hizo sekondari shule zetu zileee,hata kabla ya uchaguzi wa viongozi wa wanafunzi tulikuwa najua viongozi bora na watu wenye undumilakuwili alikuwa hapiti na hata walimu walikuwa makini kusaidia kupatikana vijana wa kuwaongoza wenzao.siku hizi mpaka ngazi ya kitaifa viongozi tunaletewa na kusomewa historia zao ili kutuvutia na idadi ya degree zao na hadhi ya vyuo walivyosoma,lakini walio bora historia yake haisomwi,mambo aliyofanyia nchi watu wanajua maana wengine unakuta wamefika hatua ya juu ya uongozi huko nyuma.ndio maana hekima na busara hakuna kwa viongozi,uzalendo(neno zito mno hili) hakuna,ujanja ujanja umejaa,watu wanapigwa risasi badala uwape pole wafiwa na kutoa mikakati ya serikali kumaliza tatizo anaropoka kuna chama kinachochea vurugu tena bila ushahidi na kiongozi huyu anadhani kila mahala ni pa kupiga propaganda za kisiasa! hii hulka lazima tuikemee,Kiafrika msibani tunaongea ya msiba na jinsi ya kutunza familia ya marehemu na si kuonesha ufahari,fahari vitani bana.

Umenikumbusha, yanayojilia huko Tarime sasa hivi, wanapotaka fukia fukia habari mradi mambo yamepita, na kesho yakatokea yayo hayo, maana yake hatujifunzi kwa yatokanayo. Kusa ni kosa lakini kurudi kosa juu ya kosa ni dhambi isiyovumilika. Wenzetu walioendelea likitokea jambo kama hilo uchunguzi utakaofanywa huo na vyombo vya habari vinavyofuatilia hadi kieleweke, sisi watumishi wa umma hawana uchungu na wanaowatumikia, inasiktisha.
 
Kwa bahati mbaya katika afrika ya leo wanasiasa walio wengi ni vibaka na ndio maana wakiwa madarakani hawataki mawazo yanayowapa changamoto na ikitokea hivyo wako radhi hata kuua! Uzalendo na upole kwa watawala wetu ni kuwakirimu wawekezaji kwa kuwalinda kwa hali yoyote! Mtawala na wateule wake yuko tayari wananchi wake wafe wakiwa masikini lakini uhusiano wake na wazungu uwe intact huku wazungu wawekezaji wakijichotea wanavyojisikia, na ole wake kiongozi wa dini apanue mdomo na kuwasemea masikini waumini. utasikia viongozi wa dini wanatakiwa kuhubiri injili ya uzima na si siasa. Nadhani kuna haja ya kuwakumbusha watawala na wanasiasa kwamba siasa inahusu maamuzi (decisions) kuhusu maisha yetu yote. Iwe uchumi, jamii, dini, raha na mengine yote.
 
Marais waliomtangulia Kikwete na Kikwete mwenyewe binafsi nawapongeza, kwani licha ya mapungufu kadhaa katika awamu zao wa uongozi lakini wamekuwa vinara wa kujali dini na viongozi wa dini licha ya madhaifu ya kibinadamu ya kuwa na itikadi tofauti jambo lisilokwepeka. Tatizo ninaloliona ni baadhi ya viongozi wanaojiona ndio wanainukia katika ulingo wa siasa na bado hawajapata uzoefu wa kisiasa ndio wanaojiona wameshajitwisha mamlako yote hata yanayopita himaya, uwezo na sheria.
 
Back
Top Bottom