Uchaguzi 2020 Kuelekelea Uchaguzi mkuu 2020: Tupe tetesi na maoni yako, unapendekeza nani agombee wapi na nafasi gani?

Kajabila

JF-Expert Member
Jan 7, 2017
537
925
Amani iwe kwenu!!

Tutumie thread hii kupendekeza wale wanaofaa kugombea 2020, Tetesi za watu watakaogombea

Mimi naanza na Dr. Tulia, Huyu dada amekuwa msaada kwetu na jamii ya Wana Mbeya kwa ujumla kwani kawasaidia wakina Mama wengi kupata mikopo yenye riba nafuu na vijana wengi kwenda Shule Mimi na awa wenzangu tumeapa kumpigia kampeni bure kabisa Dr Tulia Ackson Mwansansu kuwa Mbunge wa Mbeya 2020.
Mwenye Jimbo lake alishatangulia mbele ya haki, Mwenyezi Mungu amrehemu Samwel John Sitta,
jimbo likahikwa na mke wake Mama Sitta ambae mpaka sasa ndio mbunge, baadae zikazuka tetesi kuwa mama anaendelea ila watu wakasema tumemchoka, mama akaona upepo hauko kwake.

Zikaanza tetesi anakuja Ben Sitta upepo ulikata baada ya yeye kuteuliwa kuwa Meya, Upinzani nao wankasi, Je Bado watamuamini Sam Ntakamulenga, CCM nao wataendelea na mama au Ally Masudi Maswanya atajichukulia kiulaini jimbo lake?

Sam Ntakamulenga - Chadema
Magreth Sitta - CCM
Ally Masudi Maswanya - CCM

Nani kulinyakua jimbo la Urambo?

Habarini Wanajukwaa,

Mbunge wa Mbinga Vijijini Ndung Martin Msuha kwasasa yupo katika hatari kubwa ya kupoteza jimbo hilo la Mbinga vijijini, Mnyetishaji aliepo Mbinga vijijini ameeleza kuwa Tangu aingie ndugu msuha hakuna cha maana alichofanya zaidi ya kwenda bungeni na kupumzika hata pale baadhi ya wanambinga walipomfuata huko kuomba msaada wa mambo ya kitendaji jimboni amekuaa akiwajibu kwa dharau sana, ni hivi mwaka jana tu ndugu msuba alialikwa kwenfa kuchangia hospital ya mikalanga aliishia kuahidi(na sio kutoa)/50,000(Elfu Hamsini), hii ni hatari hasa kwa kiongozi kama yeye alieaminiwa na wananchi kushindwa saidia hospitali iliyowasaidia na inayowasaidia watu wengi w bonde la agati..

Sasa mbunge amekumbuka shuka pakiwa pamekucha hali yake ya kiuongozi ni mbaya na anahofu ya kutorudi tena.

Zaidi ya hayo ndugu Dr.John Ndunguru anazungumziwa sana na watu waliowengi kuwa mrithi wa jimbo hilo ila zaidi kuna vijana wengi wasomi wakimatengo wanatafsirika sana na wanazungumzwa sana midomoni mwa wanambinga kijijini wengi na wanashawishiwa sana warudi wasaidie kupush baadhi ya mambo kwa imani kuwa vijana ndo taifa la sasa na la baadae..Kijana mapunda aliepo bodi ya mikopo, kijana Ndunguru(mkulima), kijana Ndunguru( huyu mwanaharakati wa muda mrefu chuo kikuu cha Dar es salaam), Kijana Kapinga(mwalimu), Meneja wa kiwanda cha kahawa hapo.Mbinga..

Hali imekuwa ngumu sana hapo jimboni, vijana hao wanasikika na kusemwa semwa midomobi mwa wanambinga walio wengi lakini mwisho wao ndio wenye maamuzi ya kuwasaliti ndugu zao au kwenda kuwakomboa ndugu zao.

Yetu Macho!!! Vita vya panzi ziumiazo Nyasi.

Mwisho Tunataka wajasiri na wapambanaji Mbinga watakaoweza vusha Mbinga yetu toka ilipo kwenda sehemu nyingine.

Kuna dalili kubwa kuwa Mheshimiwa Mwigulu Nchemba wa Jimbo la Iramba Magharibi akawa na upinzani mkubwa sana mwaka huu katika kutetea nafasi yake ya Ubunge.

Kuteuliwa kwa Prof. Kitila Mkumbo ambaye anaonekana kuwa kipenzi cha Raisi Magufuli kimesababisha Mheshimiwa Mwigulu kupooza sana. Wengine ambao wanampa kiwewe ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa na aliyewahi kuwa Mbunge Jimbo hilo Juma Kilimba ambaye taarifa zinaonyesha akiwa katika maandalizi makali sana ya kugombea jimbo hilo.

Ukiacha mchakato wa wana CCM wenyewe, katika uchaguzi uliopita upinzani mkubwa wa Mwigulu ulitoka kwa Mwanadada Jesca Kishoa (Mbunge Viti Maalum kupitia CHADEMA) ambaye ni Mke wa Mwana CCM David Kafulila.

Kumekuwa na tetesi kuwa huyu mwanadada anaweza akahamia CCM ili kwenda kuongeza mbinyo kwa Mwigulu Nchemba ambaye dalili zinaonesha kuwa sio kipenzi cha Rais kwa sasa.

Halo JF siasa.

Nimekuja na Uzi maalumu wa tetesi za wagombea majimboni mkoa kwa mkoa. Tunaanza na Alphabet, Mkoa wa Arusha alafu itafuatiwa na Dar es salaam na mtiririko huohuo.

1. Mkoa wa Arusha.
Jimbo la Arusha mjini wagombea kupitia CCM ni Monabana au Philimon Mollel, RC Mrisho Gambo na mfanyabiashara mmoja mwenye asili ya Asia. Wengine wakiongezeka nitawajuza.

Jimbo la Arumeru Magharibi ni Stephen Zelote, Daniel Ole Njoolay, Elsa Mollel (Mbunge wa zamani) Goodluck Olemedeye (Mbunge wa zamani)na kijana moja machachari jina nalisaka.

Arumeru Mashariki ni Joshua Nassari na Mbunge wa sasa. Nassari anahamia CCM hivi punde.

Ngorongoro: Ole Nasha, Ole Telele na Mhadhiri moja wa chuo cha SAUT.

Monduli: Julius Kalanga MB, Joseph Sokoine, Namelok Sokoine, Fredy Lowassa na Loota Ole Sanare RC Morogoro. Huenda familia ya Sokoine wakafanya kikao ili mmoja ajitoe.

Karatu: Nafanya mawasiliano.

Longido: Dr Stephen Kiruswa MB, na Daniel Marari.

NB: Kama una tetesi za mkoa wowote nifuate inbox.
 
Amani iwe kwenu!!
Huyu dada mhe! Amekuwa msaada kwetu na jamii ya Wana Mbeya kwa ujumla kwani kawasaidia wakina Mama wengi kupata mikopo yenye riba nafuu na vijana wengi kwenda Shule Mimi na awa wenzangu tumeapa kumpigia kampeni bure kabisa Dr Tulia Ackson Mwansansu kuwa Mbunge wa Mbeya 2020

#Tunaenda_na_Tulia_2020
Tulia ndio nani?? Mbona wengine hapa Mbeya hatumjui....

Au ndio wale wa kupita bila kushinda??

Msituchokoze Mbeya Mjini...nadhani mnatuelewa....
 
Kwani anagombea hapo kwenu koromitdje?
Amani iwe kwenu!!
Huyu dada mhe! Amekuwa msaada kwetu na jamii ya Wana Mbeya kwa ujumla kwani kawasaidia wakina Mama wengi kupata mikopo yenye riba nafuu na vijana wengi kwenda Shule Mimi na awa wenzangu tumeapa kumpigia kampeni bure kabisa Dr Tulia Ackson Mwansansu kuwa Mbunge wa Mbeya 2020

#Tunaenda_na_Tulia_2020
tapatalk_1567627458569.jpeg
 
Anacho kiweza ni hiki tu
Amani iwe kwenu!!
Huyu dada mhe! Amekuwa msaada kwetu na jamii ya Wana Mbeya kwa ujumla kwani kawasaidia wakina Mama wengi kupata mikopo yenye riba nafuu na vijana wengi kwenda Shule Mimi na awa wenzangu tumeapa kumpigia kampeni bure kabisa Dr Tulia Ackson Mwansansu kuwa Mbunge wa Mbeya 2020

#Tunaenda_na_Tulia_2020
FB_IMG_1575190134993.jpeg
 
Amani iwe kwenu!!
Huyu dada mhe! Amekuwa msaada kwetu na jamii ya Wana Mbeya kwa ujumla kwani kawasaidia wakina Mama wengi kupata mikopo yenye riba nafuu na vijana wengi kwenda Shule Mimi na awa wenzangu tumeapa kumpigia kampeni bure kabisa Dr Tulia Ackson Mwansansu kuwa Mbunge wa Mbeya 2020

#Tunaenda_na_Tulia_2020
Mtakua 101 against 100,000+ za Ukawa
 
Ameanza kampeni mapema mpeni kura muone km mtamuona, ila watu wa Mbeya jinsi walivyo na msimamo sidhani km atachukua Ubunge.
Asubuhi kabisa 2020 anachukua kitu huyo Sugu ajafanya chochote Mbeya Amejenga hotel yake ndo cha msingi alichokifanya
 
Amani iwe kwenu!!
Huyu dada mhe! Amekuwa msaada kwetu na jamii ya Wana Mbeya kwa ujumla kwani kawasaidia wakina Mama wengi kupata mikopo yenye riba nafuu na vijana wengi kwenda Shule Mimi na awa wenzangu tumeapa kumpigia kampeni bure kabisa Dr Tulia Ackson Mwansansu kuwa Mbunge wa Mbeya 2020

#Tunaenda_na_Tulia_2020
Na idadi itaishia hapo hamtazidi 100
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom