Uchaguzi 2020 Kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2020: Upinzani umefanya kitu gani?

Habari wakuu
Ni zaid ya miaka mitatu imepita toka uchaguzi mkuu umalizike.Mimi kama mtanzania mkazi ya sinza jimbo la ubungo kata yangu ikiongozwa na diwani wa chadema,jimbo langu likiongozwa na mbunge wa chadema mh kubenea pamoja na manispaa yangu ikiongozwa na meya wa chadema.Lakini kinachoniumiza mimi kama mtanzania myonge Tangia uchaguzi umeisha sijawahi kumuona mbunge akifanya kikao chochote ndani ya kata yangu ili kujua kero zinazotukabili sisi wananchi,sijawahi kumuona diwani toka amechaguliwa sinza na ubungo zaidi ya kuwaona kwenye magazeti wakimdhihaki na kumtukana raisi wetu ambaye kazi zake kama Rais tunaziona kama ujenzi wa barabara kutoka kijiweni hadi magomeni.

Je lengo la kuchagua kiongozi wa upinzani kama mbunge au diwani sio kumchagua ili atuletee maendeleo bali tunamchagua ili akamtukane rais au akamkejeli rais.Sisi wana sinza tunataka maendeleo
Kipenga cha kampeni kuanza kikipulizwa ndio mtajua wamefanya nini? kwa sasa endeleeni kujitekenya na kucheka wenyewe!
 
masuala ya leli ambayo imepelekea deni la taifa kufikia tirion 61 . somethinging, ctaki kuongelea hzo ndege bila shaka mwenzangu unazifurahia atakuwa ana panda baba ako na mama ako, ila kwa upande wangu hazina manufaa, kuna upuuzi mnaita "elimu bure" huku kwetu shule za kata, wanaokaa day, mchango wa chakula n lak 2 na 50, na wanaokaa bwen n laki 4 na 50, michango hiyo n ya lazimaa!! hapo nmetoa mchango maji, umeme, afya, mlinzi, jembe, ndoo. , mifagio, reki. Kwanja, track suti. ,na uchafu mwngne naona uvivu kuandika, hapo bado ww hujamuaandaa mwanafunzi wako, hyo elimi bure ni ipi?????
mkuu pombe na ngono vimeingiaje jibu hoja kwa hoja sio hoja kwa matusi na kejeli ulipaswa kuniambia kuwa kubenea kafanya hichi na hichi au diwani kafanya hili na lile kama mimi navyoweza kukwambia Rais anajenga reli amenunua ndege ametoa elimu bure

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jiulize yafuatayo:-
(i). Wajibu wa vyama vya siasa ni upi?
(ii). Wajibu wa mwanasiasa ni upi?
(iii). Mazingira ya kufanyia siasa yanapaswa kuwa yapi?

Ukiongozwa na itikadi wakati wa kuamulia jambo huwezi kuwa hakimu mwema!
 
Mbunge au Diwani hakusanyi Kodi ,Raisi sawa ana kusanya Kodi kupitia Mamlaka za Kodi hivyo elekeza Lawama zako huko..
kwa maana hiyo hakuna haja ya kuwa na mbunge wala diwani je ahadi alizotuahidi alitudanganya je kama alijua awezi kututumikia kwanini asijiuzulu kama dhima ya uwajibikaji
 
Una ushahidi kwamba fedha za mfuko wa jimbo hao wabunge wa upinzani hawajatumia kwenye hayo mambo madogo madogo? Au umekariri ujinga kisha unauleta hapa kwa wanaume na ww uonekane upo?
mkuu mimi nina ushahidi wa jimbo langu nalotoka la ubunge hasa katika kata yangu ya sinza
 
kwa maana hiyo hakuna haja ya kuwa na mbunge wala diwani je ahadi alizotuahidi alitudanganya je kama alijua awezi kututumikia kwanini asijiuzulu kama dhima ya uwajibikaji

Katafute Wajinga wenzio mkajadili nnaona unanimalizia tu MB.
 
Habari wakuu
Ni zaid ya miaka mitatu imepita toka uchaguzi mkuu umalizike.Mimi kama mtanzania mkazi ya sinza jimbo la ubungo kata yangu ikiongozwa na diwani wa chadema,jimbo langu likiongozwa na mbunge wa chadema mh kubenea pamoja na manispaa yangu ikiongozwa na meya wa chadema.Lakini kinachoniumiza mimi kama mtanzania myonge Tangia uchaguzi umeisha sijawahi kumuona mbunge akifanya kikao chochote ndani ya kata yangu ili kujua kero zinazotukabili sisi wananchi,sijawahi kumuona diwani toka amechaguliwa sinza na ubungo zaidi ya kuwaona kwenye magazeti wakimdhihaki na kumtukana raisi wetu ambaye kazi zake kama Rais tunaziona kama ujenzi wa barabara kutoka kijiweni hadi magomeni.

Je lengo la kuchagua kiongozi wa upinzani kama mbunge au diwani sio kumchagua ili atuletee maendeleo bali tunamchagua ili akamtukane rais au akamkejeli rais.Sisi wana sinza tunataka maendeleo
Maendeleo hayana chama!
 
Back
Top Bottom