Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Status
Not open for further replies.
Nyerere hakuondoa jina la JK kumpitisha Mkapa. Mtei angekuwa anajua siasa kulikuwa na njia nzuri tu za kumpa ushindi mkwe wake bila kuondoa jina la Zitto.

Well said Mkuu!
1. Labda CHADEMA wanaweza wakawa wanajipanga kuwa Mbowe abaki kuwa mwenyekiti wa CHAMA na Mbunge na Zitto apewe nafasi ya kugombea Urais wa nchi kwa tiketi ya Chama chao?

2. CHADEMA watoke na jina la mgombea Urais 2010 mapema baada ya uchaguzi wa ndani ili kuweza kumjenga kwa wapiga kura kabla ya 2010.
 
Hivi lile ni baraza la wazee wa CHADEMA au wazee wa kaskazini? Hii ndo sumu pekee inayoiangamiza CHADEMA, Zitto jikalie pembeni watakuwangwe hao!!!!
 
Zitto kaonyesha ushujaa mkubwa kwa kuzingatia ya mbele, the odds favoured him for that post. Lakini kazi yake ingekuwa ngumu ni moja ya mambo ya kuzingatia kwenye chama amna sababu yakuongoza iwapo wana jeshi wakuu hawapo tayari kuona agenda zako za chama zieleke upande gani na mashambulizi yake itaishia kua mvurugano iwapo the closest to you want to see you fail na hiyo ndio ingekempleka Mh, Zitto pengine.

Hila na bwana Mbowe nae kama Zitto anavyosema asigombe pia kwani kama zitto kakubali na kuona faida ya kutokugombea (italeta sokomoko within) nae ni sharti aone hiyo kazi ni ya Dr.Slaa kwa sasa (kwani bwana Mbowe ana luck political skills na strategies vilevile beside ana experience hata ya ubunge ). yeye (Dr.slaa) ndio awe jemedali wa Chadema kwa sasa with exception wajue wazi, uhai na uzima Kikwete anapotoka Zitto ndio jemedali 2015 hiyo watake wasitake kama atakubali ni kipindi hichi zitto akitumie kujipanga kuwa mwanasiasa kamili kwani wafuasi anao mpaka ulaya avumilie tu raisi wetu wa baadae, Mola mpe nguvu bwana Zitto.
 
Huko ndani ya Chadema inaonekana kuna mfukuto mzito. Staili ya kujaza fomu na kuzirejesha aliyotumia Zitto nayo inazua maswali. Ndugu yangu Mtanzania alisema anaandaa popcorn katika sakata hili.
 
Hongera saana Mh. Zitto kwa kukubali chama kisigawanyike ili kuendeleza mshikamano ndani ya CHADEMA, Tunawatakia afya njema Viongozi wote wa chama.

Cheers!
 
edzzz.jpg
 
Kuna Bandiko lingine hapa linaonyesha kuwa Zitto atapewa nafasi ya ukatibu Mkuu kwani Dr. Slaa anataka kupumzika katika nafasi hiyo.
 
http://www.chadema.net/blogu/zitto/

Je, baadhi za maneno haya ya wakati ule yanasimama na kuwa na maana katika hali ya sasa? TUJADILI;

Thursday, November 02, 2006

Uchaguzi wa Afrika Mashariki - Demokrasia yabakwa

Leo Bunge la Tanzania lilitakiwa kuchagua wawakilishi wake katika Baraza la kutunga sheria la Afrika Mashariki (East African Legilstative Assembly). Uchaguzi huo unaendeshwa kwa mujibu wa kanuni za Bunge la Tanzania, Mkataba wa Afrika Mashariki na kanuni ndogo za uteuzi wa Wabunge wa Afrika Mashariki. Leo tumeshuhudia, kwa mara nyingine tena, CCM wakitumia wingi wao ndani ya Bunge kuminya demokrasia na kukanyaga bila woga maslahi ya nchi yetu.

Kanuni za Bunge na Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zinataka uwakilishi uzingatie uwiano wa vyama ndani ya Bunge.

Kambi ya upinzani ilitengewa nafasi moja tu licha kuongeza viti vyake kutoka 17 mwaka 2001 mpaka 45 mwaka 2006. Na hata hako ka nafasi kamoja ka upinzani CCM wameamua kuwachagulia kwa kumpa kura Mzee Msha ili kumpa zawadi John Cheyo ambae siku hizi anaimba nyimbo za CCM. Nikikumbuka kuwa Cheyo ndie mwenyekiti wa kamati ya bunge ya hesabu za serikali (PAC), machozi yananitoka kwani sasa serikali itaponda mali ya umma itakavyo maana hakuna chombo ya kuizuia. Cheyo ameshapewa carrot!

Katika Bunge la Afrika Mashriki kuna nafasi tatu kutoka Zanzibar. Kanuni inasema uwiano wa vyama. Zanzibar CUF na CCM zipo neck to neck. Lakini nafasi zote za Zanzibar zimechukuliwa na CCM. Maslahi ya Zanzibar katika Afrika Mashariki yapo mashakani.

Kiongozi wa Upinzani Bungeni anaomba mwongozo wa Spika ndani ya Bunge, Spika anafoka na kutishia. Haki imaminywa.

Niliamua kutoka nje ya Bunge na kususia uchaguzi. nikiungana mkono na wabunge 4 wa CHADEMA na wabunge wote wa CUF. Wabunge mashujaa wa CHADEMA waliotoka ni Bi. Halima Mdee, Bibi Maulidah Anna Komu na Chacha Zakayo Wangwe.

Kwa nini nimewalk out? Ni kwa sababu ya Principle - Misimamo isiyoyumba.

Mimi niliamua kuwa mtu wa principles mara tu niliamua kuanza siasa.

Nilitoka nje ya Bunge kwa sababu sikutaka kuingia katika histroia ya kukanyaga demokrasia. Ninaamini uchaguzi huu ni batili kwa sababu kanuni za Uchgauzi hazikufuatwa toka mwanzo wa mchakato.

Siamini katika CCM kutuchgaulia wapinzani Mbunge wake.

Siwezi kuramba miguu ya CCM, chama ambacho asilimia 90 ya wabunge wake wameingia Bungeni kwa takrima (soma rushwa). Walk out, ni kuonesha kuwa siridhiki na mchakato wa uchaguzi. Sikubaliani na kuburuzwa.

Ninawajutia Watanzania. kuamua kuchagua Bunge lililojaa chama kimoja. Hawapati thamani ya kura zao.

Najiuliza. Katika hali kama hii ya demokrasia ndani ya Bunge. Kuna haja ya kuwa Mbunge? Sipati Jibu. Nachanganyikiwa.

Je, hakuna njia nyingine ya kuimarisha demokrasia katika nchi? Demokrasia ya vyama vingi. Natafuta kitabu kinachoitwa 'ending one party dominance: Doroth Solinger. yeyote atakayepata kitabu hiki popote pale, anifanyie utaratibu nikipate. Labda nitapata mikakati ya kuimarisha demokrasia ya vyama vingi nchini.

Ni kupitia Bunge lenye angalau theluthi ya Wabunge kutoka upinzani, ndio Watanzania watapata thamani ya kura na kodi wanazolipa. Vinginevyo, nikitumia msemo wa Freeman Mbowe Bunge litabaki kuwa mchezo wa kuigiza katika Luninga (rejea makala za Freeman Mbowe za mwaka 2003).

Natoa wito kwa vijana wa Tanzania mliopo popote duniani, tuungane kuimarisha demokrasia nchini petu. This is a noble call. Wale wanaoweza kushika majimbo na waseme mapema ili tuyaandae majimbo yao, wale wasioweza wachangie mawazo na rasilimali ili kuweka miundombinu ya demokrasia katika nchi yetu. Muundombinu mkubwa ni vyama imara vya siasa vyenye mtandao mpana na sera za uhakika na zinazotekelezeka. Inawezekana, timiza wajibu wako katika ujenzi wa demokrasia.

Uchaguzi wa Afrika Mashariki - Demokrasia yabakwa


Leo Bunge la Tanzania lilitakiwa kuchagua wawakilishi wake katika Baraza la kutunga sheria la Afrika Mashariki (East African Legilstative Assembly).

Uchaguzi huo unaendeshwa kwa mujibu wa kanuni za Bunge la Tanzania, Mkataba wa Afrika Mashariki na kanuni ndogo za uteuzi wa Wabunge wa Afrika Mashariki. Leo tumeshuhudia, kwa mara nyingine tena, CCM wakitumia wingi wao ndani ya Bunge kuminya demokrasia.

Kanuni zinataka uwakilishi uzingatie uwiano wa vyama ndani ya Bunge. Kambi ya upinzani ilitengewa nafasi moja tu licha kuongeza viti vyake kutoka 17 mwaka 2001 mpaka 45 mwaka 2006. Na hata hako ka nafasi kamoja ka upinzani CCM wameamua kuwachagulia kwa kumpa kura Mzee Msha ili kumpa zawadi John Cheyo ambae siku hizi anaimba nyimbo za CCM.

Nikikumbuka kuwa Cheyo ndie mwenyekiti wa kamati ya bunge ya hesabu za serikali (PAC), machozi yananitoka kwani sasa serikali itaponda mali ya umma itakavyo maana hakuna chombo ya kuizuia. Cheyo ameshapewa carrot!

Katika Bunge la Afrika Mashriki kuna nafasi tatu kutoka Zanzibar. Kanuni inasema uwiano wa vyama. Zanzibar CUF na CCM zipo neck to neck. Lakini nafasi zote za Zanzibar zimechukuliwa na CCM. Maslahi ya Zanzibar katika Afrika Mashariki yapo mashakani.

Kiongozi wa Upinzani Bungeni anaomba mwongozo wa Spika, Spika anafoka na kutishia. Haki imaminywa.

Niliamua kutoka nje ya Bunge na kususia uchaguzi. nikiungana mkono na wabunge 4 wa CHADEMA na wabunge wote wa CUF. Kwa nini nimewalk out? Principle. Mimi ni mtu wa principle. Sikutaka kuingia katika histroia ya kukanyaga demokrasia. Ninaamini uchaguzi huu ni batili kwa sababu kanuni za Uchgauzi hazikufuatwa toka mwanzo wa mchakato. Siamini katika CCM kutuchgaulia wapinzani Mbunge wake. Siwezi kuramba miguu ya CCM, chama ambacho asilimia 90 ya wabunge wake wameingia Bungeni kwa takrima (soma rushwa). Walk out, ni kuonesha kuwa siridhiki na mchakato wa uchaguzi. Sikubaliani na kuburuzwa.

Jambo la ajabu ni kwamba, hata wagombea hawakuruhusiwa kuwa na mawakala katika kuhesabu kura. Uchaguzi haukuwa na uwazi wowote. Tutaamini vipi kuwa wagombea walipata kura zilizotangazwa? Demokrasia inakanyagwa.

Ninawajutia Watanzania. kuamua kuchagua Bunge lililojaa chama kimoja. Hawapati thamani ya kura zao.

Najiuliza. Katika hali kama hii ya demokrasia ndani ya Bunge. Kuna haja ya kuwa Mbunge? Sipati Jibu. Nachanganyikiwa. Je, hakuna njia nyingine ya kuimarisha demokrasia katika nchi? Demokrasia ya vyama vingi. Natafuta kitabu kinachoitwa 'ending one party dominance: Doroth Solinger. yeyote atakayepata kitabu hiki popote pale, anifanyie utaratibu nikipate. Labda nitapata mikakati ya kuimarisha demokrasia ya vyama vingi nchini. Ni kupitia Bunge lenye angalau theluthi ya Wabunge kutoka upinzani, ndio Watanzania watapata thamani ya kura na kodi wanazolipa. Vinginevyo, nikitumia msemo wa Freeman Mbowe Bunge litabaki kuwa mchezo wa kuigiza
 
Last edited by a moderator:
Hongera saana Mh. Zitto kwa kukubali chama kisigawanyike ili kuendeleza mshikamano ndani ya CHADEMA, Tunawatakia afya njema Viongozi wote wa chama.

Cheers!
kimeshagawanyika hicho. Na bado, hii ni TLP au NCCR- Mageuzi ya pili.

Uchu wa madaraka ndio chanzo cha mgawanyiko.

Tatizo ni kwamba, ikiwa Zitto atajitoa na hata wakimfujuza Chamani atarudi kwenye profesional yake na Mbowe atarudi wapi?

Jibu sahihi- Birikana.... umepata 100%
 
Je, Kujitoa Kwako Kugombea Uenyekiti Kunajenga au Kunabomoa Chama?

Ndugu Zitto Kabwe (MB),

Nimeamua kukuuliza swali hili la wazi kwa faida ya Jamii ya Kitanzania kwa ujumla. Ningeweza kukuuliza kwa faragha ila kufanya hivyo kungenisaidia mimi binafsi. Naamini suala hili linapaswa kujadiliwa kwa uwazi na ukweli.

Nilikuwa safarini hivyo nilipitiwa na hizi taarifa za wewe kujitoa kugombea Uenyeketi. Leo baada ya kusoma taarifa hizo katika za Vyombo vya Habari nimepigwa na butwaa. Swali kuu nalojiuliza ni, je, kujitoa kwako kutasaidia kuleta huo umoja ndani ya chama chenu au ndio utakigawanya zaidi?

Swali hilo kuu linazaa maswali haya mengine ambayo naomba uyajibu:

1. Je, hukuona kuwa utakigawanya chama ulipochukua fomu?
2. Je, huoni kuwa ni hatari kubadili msimamo mzito kama huo?
3. Je, haionekani kuwa umewasaliti waliokuomba ukagombee?

Ndugu nitashukuru kama utanijibu maswali hayo ili nisibaki naamini kuwa hata hicho 'chama kina wenyewe'!

Wasalaam,
Mpiga Kura


Companero:

Mbona unauliza maswali ya kipolisi wakati tupo kwenye siasa?
 
Hivi lile ni baraza la wazee wa CHADEMA au wazee wa kaskazini? Hii ndo sumu pekee inayoiangamiza CHADEMA, Zitto jikalie pembeni watakuwangwe hao!!!!
kama uldhani CHADEMA, ni sawa na CUF ilivyotafnwa na propaganda za CCM kuwa ni chama cha kigaidi zitaimaliza CHADEMA, chama chochote hakiwezi kusambaa kama hewa ndani ya dakika tu....kuna ukweli kua CHADEMA ilipoanza ilikua na makada wengi wa Kaskazini,ila taratibu hali imebadirika hadi kua Chama cha kitaifa, na ndio maana tunakijadili humu.
Umedanganya , ukadanganyika kua CHADEMA ni chama cha Kaskazini......hicho ni kielezo tosha cha UJINGA wa KUFIKIRI.
 
Hii issue ya Mhe. Zitto inaacha maswali mengi bila majibu. Katika ile thread ya makala ya Kibanda, nilisema, Zitto amechukua fomu kugombea ili kutesti zali na kujipatia sababu ya heshima ya kutimkia CCM.Tangu alipodai hagombei, nilianza kupata mashaka, baadae akaamua atagombea nilijiuliza maswali bila majibu.Niliposikia anagombea uenyekiti kwa stail aliyotumia, nilijua haweza sikia la muadhini wala la mnadi swala, ni mbele kwa mbele..kumbe.Sasa Zitto ameshadhibitisha Chedema ina wenywew na wenyewe ndio wale wale, kinachofuatia atasusa nafasi zoter atakazopewa, baada ya bunge kuvujwa, jamaa nae ndio hapo hapo atakapobainisha msimamo wake ni kuelekea kule kule ambako tayari ameshaahidiwa uwaziri.Sisi yet macho, tusubiri tuone.
 
You Must belong to CCM....Sorry brother ur aim will no longer achieved....!!!
So what had you want to happen....?
CCM mkubwa wee...toka....Mwakani mtakiona..pumbavuuu.....
 
kimeshagawanyika hicho. Na bado, hii ni TLP au NCCR- Mageuzi ya pili.

Uchu wa madaraka ndio chanzo cha mgawanyiko.

Tatizo ni kwamba, ikiwa Zitto atajitoa na hata wakimfujuza Chamani atarudi kwenye profesional yake na Mbowe atarudi wapi?

Jibu sahihi- Birikana.... umepata 100%

We Zawadi Umewaza mbali sana................
 
Hii issue ya Mhe. Zitto inaacha maswali mengi bila majibu. Katika ile thread ya makala ya Kibanda, nilisema, Zitto amechukua fomu kugombea ili kutesti zali na kujipatia sababu ya heshima ya kutimkia CCM.Tangu alipodai hagombei, nilianza kupata mashaka, baadae akaamua atagombea nilijiuliza maswali bila majibu.Niliposikia anagombea uenyekiti kwa stail aliyotumia, nilijua haweza sikia la muadhini wala la mnadi swala, ni mbele kwa mbele..kumbe.Sasa Zitto ameshadhibitisha Chedema ina wenywew na wenyewe ndio wale wale, kinachofuatia atasusa nafasi zoter atakazopewa, baada ya bunge kuvujwa, jamaa nae ndio hapo hapo atakapobainisha msimamo wake ni kuelekea kule kule ambako tayari ameshaahidiwa uwaziri.Sisi yet macho, tusubiri tuone.

Mkuu, sina hakika sana na hilo (Japo si ajabu na si dhambi ktk siasa) na kama akiondoka Chadema na kwenda CCM hatokuwa amewatendea haki wengi walio nyuma yake na nadhani hata wanaotaka aondoke Chadema hawawatakii meme vijana wengi ndani ya Chadema. Jambo la msingi ni yeye kufanya kazi na Mbowe na kusafisha hali ya hewa ndani ya chama chao na baadaye kusonga mbele. Naamini mambo yakitulia hata Mbowe anaweza kufanya maamuzi mazito baadaye. Hili lilikaa vibaya sana kwa wote wakuu
 
Kuna tofauti kati ya kumchezea mtu rafu na kumuwekea pingamizi asicheze. Wakati la mwanzo linavumilika (kwa kinyongo) la pili linamaanisha woga. Zitto amewekewa pingamizi asigombee! Period.
 
Naomba niseme kwamba hili swala by all accounts..lazima watu wataliangalia katika prism ya Uchagga vs..nini sijui. Hata kama hawana hiyo nia. Its simply a human nature to connect the dots. Baba mkwe alikuwa mwenyekiti..akamuachia mkwe..leo..baba mkwe ndo anaongoza kikao cha kuwaengua wagombeaji wengine....simply say..Numbers dont add up. .

Mzee Mtei alipoacha uenyekiti aliyefwatia ni Mzee BOB MAKANI. Uongo ni mbaya sana....jenga hoja zako kwenye facts mkuu.
 
Wamejimaliza kaka; wajanja huwa wanabadili matokeo sio kumzuia mtu asigombee!
hajazuiliwa kugombea, ila alishauriwa , na somo likamkolea.....maisha marefu na mema kwa CHADEMA.
Mnatammani kuona anguko lake lakini haliji....mtasubiri sana mwishowe Tanzania itakua Chini ya Chama hiki. sio ndoto bali ukweli utatokea, Fumbua macho.
 
nakubaliana na wewe Mimibaba. huwa kila wakuu wanapokosa issues yakusema wanapoishiwa mitazamo wanakimbia ukabila na kwahakika wanakuaa wanaondoa macho na akilizao katika kuaangalia jambo kwa mapaa zaidi.Manake wanataka kuniaambia wote (wajumbe) waliopiga kura walikua wanapiga kura katika misingia ya ukabila ? tena kama si kosei waliosimama kungombania nafasi hizo na aganst Lucy na Ndesamburo pia walikua wachanga so ? au mtasema kuna wachaga weupe na weusi?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom