Mpaka Kieleweke
JF-Expert Member
- Feb 27, 2007
- 4,132
- 1,571
Leo Katibu Mkuu wa CHADEMA ametoa tamko rasmi la Mkutano Mkuu wa Ndani ya Chama nalo ni kama ifuatavyo;
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinawatangazia wanachama wote wa CHADEMA na umma wa Watanzania wapenda Maendeleo kuwa Mkutano Mkuu wa uchaguzi wa ndani ya Chama utafanyika tarehe 03-04/09/2009 Jijini Dar Es Salaam .
Mkutano huu utatanguliwa na Mikutano mbalimbali kama ilivyoorodheshwa kwenye ratiba yetu ikiwa pia ni kwa mara ya kwanza uzinduzi rasmi wa Mabaraza ya Chama utaweza kufanyika pamoja na Uchaguzi wa Viongozi wa Mabaraza husika.
Hivyo wanachama wote kutoka Mikoani, Wilayani, Katani na Vijiji mbalimbali wenye nia, uwezo,uadilifu na sifa za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ngazi ya Taifa mnataarifiwa kwenda kuchuka fomu za kugombea na Fomu hizo zirejeshwe Makao Makuu zikiwa zimejazwa kwa ukamilifu na kwa kuzingatia muda uliowekwa na Kamati Kuu ya Chama .
Fomu kwa ajili ya kugombea nafasi mbalimbali zimeshatumwa tangu August 10 2009 kwenye kila ofisi za Chama Mikoani ,hivyo tangazo hili ni kwa ajili ya kuwakumbusha wanachama wetu kuhusu ratiba ya mchakato mzima wa uchaguzi ndani ya Chama. Kwa wale ambao hawajachukua fomu,bado wanayo nafasi kwani tarehe ya mwisho ya kurudisha fomu ni August 24, 2009 saa kumi kamili mchana.
Fomu zilizotumwa ni kwa ajili ya kugombea nafasi zifuatazo;
(a) Mwenyekiti Taifa
(b) Makamu Mwenyekiti Bara
(c) Makamu Mwenyekiti Zanzibar
(d) Wajumbe wa kuchaguliwa kuingia kwenye Kamati Kuu na Baraza Kuu kwa mujibu wa Katiba ya Chama .
(e) Wenyeviti wa Mabaraza ya
(i) Wazee
(ii) Wanawake (BAWACHA).
(iii) Vijana (BAVICHA).
(f) Makamu wenyeviti wa mabaraza ya
(i) Wazee
(ii) Wanawake (BAWACHA)
(iii) Vijana (BAVICHA).
Ratiba kamili ya Mikutano hiyo ni kama ifuatavyo;
(i) Kamati Kuu tarehe 30/08/2009.
(ii) Mkutano Mkuu wa Baraza la Wazee 31/08/2009.
(iii) Mkutano Mkuu wa Baraza la Vijana (BAVICHA) 31/08/2009.
(iv) Mkutano Mkuu wa Baraza la Wanawake (BAWACHA) 01/09/2009.
(v) Mkutano wa Baraza Kuu 02/09/2009.
(vi) Mkutano Mkuu wa Chama (Siku mbili ) 03-04/09/2009.
(vii) Mkutano wa Baraza Kuu 05/09/2009.
(viii) Mkutano wa Kamati Kuu 06/09/2009.
Hivyo basi tunapenda kuwafahamisha Wanachama wetu na Watanzania wote kwa ujumla kuwa hii ndio ratiba yetu rasmi ya kuingia kwenye uchaguzi Mkuu wa Chama na pia ni hatua muhimu sana katika Mapambano yetu dhidi ya Mafisadi na Ufisadi na kuhamasisha uwajibikaji na kutetea rasilimali za Taifa.
Ni muhimu ikazingatiwa kuwa ndani ya CHADEMA kila Mwanachama anayo haki ya kugombea nafasi yeyote ile kwa mujibu wa Katiba ya Chama,hivyo basi kila Mwanachama atumie haki yake ya kidemokrasia kuchukua fomu .
Ahsante sana kwa ushirikiano wenu.
Dr. Willibrod P. Slaa (Mb)
Katibu Mkuu.
19/08/2009.
TAARIFA KWA UMMA WA WATANZANIA.
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinawatangazia wanachama wote wa CHADEMA na umma wa Watanzania wapenda Maendeleo kuwa Mkutano Mkuu wa uchaguzi wa ndani ya Chama utafanyika tarehe 03-04/09/2009 Jijini Dar Es Salaam .
Mkutano huu utatanguliwa na Mikutano mbalimbali kama ilivyoorodheshwa kwenye ratiba yetu ikiwa pia ni kwa mara ya kwanza uzinduzi rasmi wa Mabaraza ya Chama utaweza kufanyika pamoja na Uchaguzi wa Viongozi wa Mabaraza husika.
Hivyo wanachama wote kutoka Mikoani, Wilayani, Katani na Vijiji mbalimbali wenye nia, uwezo,uadilifu na sifa za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ngazi ya Taifa mnataarifiwa kwenda kuchuka fomu za kugombea na Fomu hizo zirejeshwe Makao Makuu zikiwa zimejazwa kwa ukamilifu na kwa kuzingatia muda uliowekwa na Kamati Kuu ya Chama .
Fomu kwa ajili ya kugombea nafasi mbalimbali zimeshatumwa tangu August 10 2009 kwenye kila ofisi za Chama Mikoani ,hivyo tangazo hili ni kwa ajili ya kuwakumbusha wanachama wetu kuhusu ratiba ya mchakato mzima wa uchaguzi ndani ya Chama. Kwa wale ambao hawajachukua fomu,bado wanayo nafasi kwani tarehe ya mwisho ya kurudisha fomu ni August 24, 2009 saa kumi kamili mchana.
Fomu zilizotumwa ni kwa ajili ya kugombea nafasi zifuatazo;
(a) Mwenyekiti Taifa
(b) Makamu Mwenyekiti Bara
(c) Makamu Mwenyekiti Zanzibar
(d) Wajumbe wa kuchaguliwa kuingia kwenye Kamati Kuu na Baraza Kuu kwa mujibu wa Katiba ya Chama .
(e) Wenyeviti wa Mabaraza ya
(i) Wazee
(ii) Wanawake (BAWACHA).
(iii) Vijana (BAVICHA).
(f) Makamu wenyeviti wa mabaraza ya
(i) Wazee
(ii) Wanawake (BAWACHA)
(iii) Vijana (BAVICHA).
Ratiba kamili ya Mikutano hiyo ni kama ifuatavyo;
(i) Kamati Kuu tarehe 30/08/2009.
(ii) Mkutano Mkuu wa Baraza la Wazee 31/08/2009.
(iii) Mkutano Mkuu wa Baraza la Vijana (BAVICHA) 31/08/2009.
(iv) Mkutano Mkuu wa Baraza la Wanawake (BAWACHA) 01/09/2009.
(v) Mkutano wa Baraza Kuu 02/09/2009.
(vi) Mkutano Mkuu wa Chama (Siku mbili ) 03-04/09/2009.
(vii) Mkutano wa Baraza Kuu 05/09/2009.
(viii) Mkutano wa Kamati Kuu 06/09/2009.
Hivyo basi tunapenda kuwafahamisha Wanachama wetu na Watanzania wote kwa ujumla kuwa hii ndio ratiba yetu rasmi ya kuingia kwenye uchaguzi Mkuu wa Chama na pia ni hatua muhimu sana katika Mapambano yetu dhidi ya Mafisadi na Ufisadi na kuhamasisha uwajibikaji na kutetea rasilimali za Taifa.
Ni muhimu ikazingatiwa kuwa ndani ya CHADEMA kila Mwanachama anayo haki ya kugombea nafasi yeyote ile kwa mujibu wa Katiba ya Chama,hivyo basi kila Mwanachama atumie haki yake ya kidemokrasia kuchukua fomu .
Ahsante sana kwa ushirikiano wenu.
Dr. Willibrod P. Slaa (Mb)
Katibu Mkuu.
19/08/2009.
Last edited by a moderator: