CCM yamfukuza uanachama Bernard Membe, Kinana apewa karipio kali huku Makamba akitoka salama

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,746
11,877
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi, Humphrey Polepole amesema kuwa Membe aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje ya Tanzania amefukuzwa ndani ya chama hicho

Amesema uamuzi huo umekuja baada ya taarifa zake ndani ya chama kuonesha mwenendo wake kutoka mwaka 2014 kuwa amewahi kupata adhabu nyingine ambazo zingeweza kumsaidia kujirekebisha ila imeonekana haikuwa hivyo

Kamati kuu ya Halmashauri ya Taifa ya CCM imeazimia hayo leo baada ya kupokea ripoti ya Kamati Ndogo ya Maadili kwenye Kikao chake ilichokaa chini ya Mwenyekiti Dkt. John Magufuli.

Feb 6, 2020 Kamati ya Maadili na Usalama ya Chama Cha Mapinduzi CCM ilitumia Takribani saa tano Kumuhoji Bernad Membe ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Kamati kuu ya taifa ya chama hicho la kuhojiwa kwa wanachama wake watatu wakiwamo waliowahi kuwa makatibu wakuu Mzee Yusuph Makamba na Abdulrahman Kinana.

Mwezi Disemba, Halmashauri kuu ya CCM (NEC) iliagiza makada hao watatu kuhojiwa, hatua hiyo ilitimu baada ya 'vuta n'kuvute' ya muda ndani ya chama hicho.

Makada wote hao, "wanakabiliwa na tuhuma za maadili kwa mujibu wa Katiba ya Chama na Kanuni ya Maadili na Uongozi." Taarifa iliyotolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Humphrey Polepole Disemba 13 2019, hata hivyo haikueleza bayana ni makosa gani ya kimaadili ambayo wanatuhumiwa nayo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, makada wengine watatu, Januari Makamba, Nape Nnauye na William Ngeleja walisamehewa baada ya kumuomba radhi mwenyekiti wa CCM, Rais John Pombe Magufuli.

Wanachama hao waliomba radhi kwake (Magufuli) baada ya "kukiri mbele yake kufanya makosa ya kimaadili yaliyokidhalilisha chama na viongozi wake mbele ya umma," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Wanachama hao watatu wa CCM pamoja na watatu ambao walihojiwa, wote sauti zao zao wakiwa wakifanya nawasiliano kwa njia ya simu zilivujishwa kwenye mitandao nchini Tanzania wakizungumzia masuala mbalimbali kukihusu chama na mwenyekiti wake Magufuli.

Sehemu ya mazungumzo yaliyovuja ya Mzee Yusuf Makamba na Kinana ni pamoja na kuandaa taarifa ya malalamiko dhidi ya 'mawanaharakati' Cyprian Musiba ambaye wanamtuhumu kwa 'kuwadhalilisha' bila kuchukuliwa hatua yoyote na kuhoji analindwa na nani.

Kwa upande wa Membe, licha ya kusikika kwenye mazungumzo hayo yalivuja, amekuwa pia akituhumiwa na baadhi ya wanchama wa chama hicho kuwa anajipanga 'kumhujumu' Magufuli katika uchaguzi mkuu wa Urais mwaka huu 2020.

Bernard K. Membe said:
Watanzania wenzangu nimepata habari ya kufukuzwa kwangu kutoka kwenye Chama changu cha CCM. Simu zinamiminika hadi nashindwa kuzijibu. Tulieni! Nitapata muda wa kuongea na wote muda si mrefu!

Zaidi, soma:
1) Sauti inayodaiwa ni ya Membe na Katibu Kata kijiji cha Rondo video clip yao yavuja

2) Bernard Membe: Sauti iliyodukuliwa na kusikika ni ya kwangu

3) Bernard Membe aitwa kwenye Kikao cha Kamati ndogo ya Udhibiti wa Nidhamu CCM

4). 3). CCM yamfukuza uanachama Bernard Membe, Kinana apewa karipio kali huku Makamba akitoka salama

5). Uchaguzi 2020 - Bernard Membe achukua fomu ya kugombea Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo

WASIFU WA MEMBE
1582887027923.png
Bernard Kamilius Membe alizaliwa tarehe 9 Novemba, 1953, Rondo, Chiponda, katika Mkoa wa Lindi, akiwa ni mtoto wa pili kati wa watoto saba (7) waliozaliwa katika familia ya Mzee Kamillius Anthony Ntachile na Mama Cecilia John Membe. Kwa kabila, Bernard Membe ni Mmwera, na kama ilivyo desturi ya Wamwera, watoto hutumia jina la ukoo wa Mama. Hivyo watoto wote saba wa familia hii ya Mzee Kamillius wamekuwa wanatumia jina la upande wa mama yao, Cecilia, yaani Membe.

Elimu:
1962 – 1968: Elimu ya msingi katika shule ya msingi ya Chiponda, Lindi.
1969 – 1972: Elimu ya Sekondari, (O-level) Namupa Seminary, Lindi
1973 – 1974: Kidato cha tano na sita (A-level) Itaga Seminary, Tabora
1975 – 1980: Aliajiriwa serikalini, ofisi ya rais
1981 – 1984: Alipata Shahada ya kwanza katika tasnia ya Sayansi katika maswala ya Siasa na mahusiano ya kimataifa (Bachelor Political Science and International Relations)
1985 – 1989: Aliendelea na ajira yake serikalini katika katika ofisi ya rais
1990 – 1992: Alipata Stashada ya Uchumi, Mahusiano ya Kimataifa na Sheria za Kimataifa (Masters- Economics, International Relations and International Law)
1993 – 1994: Alirudi serikalini kuendelea na kazi kama mchambuzi za mambo ya ulinzi na usalama

Mafunzo:
Kati ya mwaka 1975 na 1976 Ndugu Bernard Membe alijiunga na mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kambi ya Oljoro, Arusha. Hii ni kwa mujibu wa Sheria ambapo vijana wote waliohitimu kidato cha Sita walitakiwa kujiunga na mafunzo ya Jeshi kwa muda wa mwaka mmoja. Baada ya kuhitimu mafunzo hayo ya Jeshi, Ndugu Membe aliajiriwa katika Ofisi ya Rais, Utawala bora.

Mwaka 1978, Ndugu Membe alipata Mafunzo ya sheria za Jinai na usalama wa nchi, nchini Uingereza. Aidha, mwaka 1980, Ndugu Membe alipata mafunzo ya siasa, katika Chuo cha Chama cha Mapinduzi (CCM), Kivukoni, Dar es Salaam.

Familia:
Mwaka 1986, Ndugu Bernard Membe alifunga ndoa Takatifu na Dorcas Richard Masanche, katika Parokia ya Mtakatifu Joseph, Dar es Salaam. Ndugu Membe na mama Dorcas wamejaliwa kupata watoto watatu, Cecilia, Richard na Denis.

Siasa:
Ndugu Membe ametumikia nafasi mbalimbali ikiwemo Kamanda wa Vijana wa Mkoa wa Lindi, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa, na Katibu wa Secretariat ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa. Mwaka 2000, aliingia Bungeni baada ya kuchaguliwa na wananchi wa jimbo la Mtama, kuwawakilisha katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Licha ya uchanga wake bungeni, akiwa kama mbunge wa kawaida (back bencher), Bernard Membe alikuwa mchangiaji mkubwa wa mijadala inayohusu Amani, Ulinzi na Usalama pamoja na Utawala Bora. Membe aligombea urais ndani ya chama cha Mapinduzi ya CCM 2015 na kuchujwa katika vikao vya ndani ambapo hatimaye Magufuli alipewa ridhaa.

Mwaka 2005, Bernard Membe alichaguliwa tena na wananchi wa Jimbo la Mtama kuwawakilisha katika Bunge la Jamhuri ya Muungano. Tofauti na kipindi cha nyuma, Bernard Membe alianza muhula wa pili wa Ubunge, Januari 2006, kama ‘front bencher’ baada ya kuteuliwa na rais Jakaya Mrisho Kikwete kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani. Kufuatia mabadiliko ya baraza la Mawaziri mnamo mwezi Oktoba, 2006, Bernard Membe alihamishwa Wizara na kuwa Naibu Waziri katika Wizara ya Nishati na Madini – moja ya wizara ngumu na nyeti kwa Taifa.

Hata hivyo miezi michache baadae, yaani January 2007, rais Jakaya Mrisho Kikwete alimteua Bernard Membe kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa baada ya aliyakuwa anashikilia wadhifa huo - Dr Asha Rose Migiro - kuteuliwa na Katibu Mkuu Baraza la Umoja wa Kimataifa na kuwa Naibu Katibu mkuu wa baraza hilo. Bernard Membe amehudu katika nafasi hiyo ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa tangu 2007 hadi 2015, akiwa ni Mtanzania wa pili kushika wadhifa huo kwa miaka mingi mfululizo, akitanguliwa na Rais Kikwete ambaye alidumu katika Wizara hiyo kwa miaka 10 mfululizo.

Mafanikio:
Bernard Membe ameongoza Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kipindi ambacho Tanzania na dunia, kwa ujumla, ilikabiliwa na changamoto kubwa katika mambo mbalimbali yanahusiana na ulinzi na usalama, uchumi na ajira (hasa kwa vijana). Changamoto hizo zimepelekea hali ya amani kwa ujumla kutetereka katika maeneo mengi ya dunia.

Hata hivyo, chini ya uongozi wa Bernard Membe, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimatafa, Tanzania imeendelea kuwa mtetezi na mshirika mkubwa wa ulinzi na usalama ndani ya Ukanda wa Afrika na duniani. Tanzania imeshiriki kuleta amani katika nchi za Maziwa makuu yaani, DRC, Burundi na Malawi, lakini pia Tanzania imeshiriki katika utatuzi wa migogoro ya kisiasa katika nchi za Comoro, Madagasca, na Sudan ya Kusini. Aidha, Tanzania imekuwa mshiriki mzuri katika kuchangia vikosi vya kulinda amani katika mataifa ambayo yalipata machafuko kisiasa.

Uchumi: Bernard Membe amesimamia vema utekelezaji wa sera ya Diplomasia ya uchumi ili kuwezesha Tanzania kufanya mageuzi ya kiuchumi na kijamii na kuininua hali za wananchi wake. Ni katika kipindi chake, nchi imeshuhudia uwekezaji mkubwa katika eneo la viwanda, gesi, makaa ya mawe, kilimo na utalii. Chini ya uongozi wa Ndugu Bernard Membe, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, ilipata tuzo ya utendaji bora iliyotolewa na sekta binafsi kwa kutambua mchango mkubwa wa Wizara katika kukuza sekta binafsi Tanzania.

Kudumisha mahusiano kimataifa: Katika kipindi chake, Tanzania imefanikiwa kuipaisha Diplomasia yake katika Jumuiya ya Kimataifa kwa kutembelewa na viongozi mbalimbali mashuhuri kama, Marais George W. Bush na Baraka Obama wote wa Marekani, Xi Jinping wa Uchina, Joachim Gauck wa Ujerumani, Jacob Zuma wa Afrika Kusini, Mwai Kibaki na Uhuru Kenyatta wa Kenya, Paul Kagame wa Rwanda, Piere Nkuruzinza wa Burundi, Joseph Kabila wa DRC, Philipe Nyusi wa Msumbiji, Mwana wa Mfalme wa Malkia wa Uiengereza, na Mwana wa Mfalme wa Japan.

Pia chini ya uongozi Ndugu Bernard Membe Tanzania imefanikiwa kupanua wigo wa mahusiano yake Kaimataifa kwa kufunguwa Balozi mpya katika nchi za Malaysia, Brazil, Comoro, Oman, Umoja wa Falme za Kiarabu na Kuwait. Aidha, Wizara imefanikiwa kufungua upya Ubalozi wa Tanzania the Hague, Uholanzi uliofungwa mwaka 1994. Kadhalika Balozi Mpya za Brazil, Oman, Uturuki, Kuwait, Qatar, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na Namibia zilifunguliwa hapa nchini.

Kutambuliwa:
Kwa kutambua mchango wake katika kurejesha hali ya amani na utulivu katika Visiwa vya Comoro, mwaka 2008, Bernard Membe alikuwa miongoni mwa watanzania waliotunukiwa Nishani ya Operesheni Demokrasia Comoro na rais Jakaya Mrisho Kikwete.

Uozefu:
2006 – hadi sasa: Mjumbe wa Baraza la Mawaziri wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
2008 – Mwenyekiti Baraza la Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Umoja wa Africa, Addis Ababa, Ethiopia.
Mkuu wa waangalizi wa uchaguzi mkuu wa Zimbabwe kutoka muungano wa nchi za ukanda wa Afrika Kusini, SADC
2006 – 2011: Katibu wa Secretariat ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, CCM
2006 – 2011: Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa.
2006 – hadi sasa: Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM, Taifa
2013 – hadi sasa: Mwenyekiti Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Madola Commonwealth
2014 – hadi sasa: Mwenyekiti Baraza la Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Amekuwa mjumbe wa kamati za usuluhishi katika migogoro kwenye nchi za Sudan ya Kusini, Madagascan na katika mzozo wa mpaka kati ya Tanzania na Malawi.

Pia Tanzania imefanikiwa kushiriki katika zoezi la Uangalizi wa chaguzi kwa niaba ya SADCC katika nchi za Zambia, Zimbabwe, Madagasca, Kenya, Comoro na Afrika ya Kusini.

Zaidi, soma:

Uchaguzi 2020 - Bernard Membe achukua fomu ya kugombea Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo
 
Wadau.

Tunawaletea Taarifa za Maamuzi yaliyochukuliwa na Kamati Kuu Ya Halmashauri Kuu Ya CCM Kutokea Lumumba Dar es salaam dhidi ya Waliokuwa Makada wa Chama hicho wakiongozwa na Bernard Membe.
CCM-Membe.jpg

UPDATES: SAA 7:39 MCHANA

MAAMUZI YA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM.

1. Ndg. Bernard Membe Afukuzwa Uanachama wa CCM. Mwenendo wake haukuwa wa Kuridhishwa mzuri kuanzia 2014.Aliwahi kupewa adhabu kwa matarajio kuwa mwenendo wake utabadilika Lakini imekuwa kinyume Chake.

2. Ndg. Abdulhaman Kinana Apewa Karipio Kali na Atakuwa chini ya Uangalizi Maalumu kwa muda wa miezi 18 kuanzia Tarehe 28/2/2020

3. Ndg. Yusuph Makamba amepewa Msamaha na hii ni baada ya kutoa Ushirikiano wa kutosha kwa mamlaka Husika sambamba na kuomba msamaha kwa maandishi.
 
IGWE,
Na la kwanza nalo ni gumu sana. Siasa is all about uchaguzi, hasa mkuu... ukizingatia wana haki ya kuchagua na/au kuchaguliwa
 
Boniphace Kichonge,
Naonya CCM wasifanye Maamuzi ya Hasira na Kukomoa dhidi ya hawa Makada Waandamizi kwani wanaweza wakaja Kujuta kama si Kujutia hapo baadae.

Nimeonya hivi hasa baada ya kupata za chini chini kuwa Maamuzi yatakayotolewa dhidi yao yatakuwa ni ya Kuwakomoa zaidi badala ya kuwa ya Kibusara kwa Afya na Ustawi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
 
Wadau.

Tunawaletea Taarifa za Maamuzi yaliyochukuliwa na Kamati Kuu Ya CCM Kutokea Lumumba Dar es salaam dhidi ya Waliokuwa Makada wa Chama hicho wakiongozwa na Bernard Membe.

View attachment 1371282

Tafadhali usikae mbali.
Kampeni meneja mwaka huu wa mgombea uraisi wa CCM anakuwa nani? Mh. Kinana ametumika kama kampeni meneja wa Mh Kikwete na baadaye Mh Magufuli; jee CCM itamteua nani kuchukua nafasi ya Kinana?
 

Similar Discussions

34 Reactions
Reply
Back
Top Bottom