IMBOMBONGAFU
Senior Member
- Jun 7, 2009
- 147
- 3
Subirini mtavunjwa miguu Mwaka huu..MOI wameambiwa waongeze Madaktari siku ya Uchaguzi maana miguu kwisha.Kumepakuliwa rungu kubwa za Mpingo.....mwaka huu tutapata Wakimbizi wa TZ nchini Rwanda
kwanza siku hiyo ya uchaguzi chadema mutanyweshwa pombe ile mbaya kisha usiku wakati wa kuhesabu kura umeme utakatika ghafla!! Sasa huku mukiwa mumelewa chakari, na taa zimezimwa mpaka usiku wa manane ndio utarudi wakati huo mumesha lala fofofo!!! Kitaeleweka nini? Na huku mumelala?
MfanoMartial law is the imposition of military rule by military authorities over designated regions on an emergency basisusually only temporarywhen the civilian government or civilian authorities fail to function effectively (e.g., maintain order and security, and provide essential services), when there are extensive riots and protests, or when the disobedience of the law becomes widespread. In most cases, military forces are deployed to quiet the crowds, to secure government buildings and key or sensitive locations, and to maintain order
Martial law can be used by governments to enforce their rule over the public. Such incidents may occur after a coup d'état (Thailand 2006); when threatened by popular protest (China, Tiananmen Square protests of 1989); to suppress political opposition (Poland in 1981);
Hii ya huko mbona mjeshi ndio amemwokoa uyo raisi baada ya manjagu eti kuchoka na mambu yake,bado jeshi limempa sapoti na kuwasambaratisha polisi ,kwenye runinga inaonyesha wazi polisi wakitoka baru ,yaani polisi anaogopa mjeshi ile mbaya !!Hehhe heheh wakaulize wenzao wa Equador yapo wapi maana prez yupo hosp kapigwa mabomu ya machozi na familia yake imepewa hifadhi kwa marafiki!
Baba yake Shimbo na Baba yake Kikwete walifanya kazi pamoja ,Kikwete na Shimbo wamekuwa pamoja kwa hiyo rafiki yakejakaya amemtuma aseme hayo,Alipomteua Mwamumunyange ilikuwa ni geresha mambo mengi alikuwa anamwagiza Shimbo nyuma ya mgongo wa Mwamunyange mpaka mwamunyange alipomkoromea ndipo akanza kumpa heshima yake .
Shimbo kuna mfano wa thailand and wafilipino wananchi walipoamua kuchukua nchi yao kutoka kwa wahafidhina na mafisadi hawakujali Jeshi ,Nchi hii siyo ya mamako Shimbo ni yetu sote tupo tayari kwa lolote nyakati za vitisho zilishapita.
Katiba inasema wanajeshi hamruhusiwi kuwa wanasiasa kwa hiyo munataka kuilekeza tume kwa mtutu wa buduki wa mtangaze kikwete kwamba ameshinda halafu museme akishatangazwa huwezi kupinga
SHIMBO damu ya mtanzania yeyote ikimwagika wewe ndio wa kwanza tutalala mbele na wewe,tuachie nchi yetu
huna busara kabisa waroho wa madaraka wakubwa
Sijui rafiki yangu Reginald Mengi amejisikiaje pale JK alipomsifu RA kuwa ni mtu makini na msafi!Kwa vile Viongozi wa JWTZ wameamua kuingia katika siasa, bani tuwakaribishe, lakini inabidi watueleze mustakabali hasa wa nchi hii unakwendaje -- iwapo tunaeleke pema au pabaya.
Mimi nawaambia kwamba JK na CCM yake ndiye wanaipeleka nchi pabaya na ndiyo wastahili kukemewa kwa kutaka kuleta vurugu.
Nitatoa mfano mmoja tu: Kitendo cha JK kukumbatia na kuwasifia watuhumiwa wa ufisadi, hasa wale ambao kesi zao za ufisadi ziko mahakamani limeleta dharau kubwa kwa mahakama zetu -- na pia kuamsha hasira kubwa miongoni mwa wananchi hasa wale wenye kutambua sheria na haki ni vitu gani.Kamwe si kitendo cha utawala bora.
Wanachi hawa wana hasira sana kwa ukiukwaji mkubwa huu wa sheria. Karibuni jamvini.
Sijui rafiki yangu Reginald Mengi amejisikiaje pale JK alipomsifu RA kuwa ni mtu makini na msafi!
Ama kweli mtu akikutawala kiuchumi anakutawala hadi mawazo!...ataamua yeye useme nini, useme na nani, uvae nini, nahisi anaweza hadi kukupa ratiba ya kuwa na mkeo:A S wink::A S wink::A S wink:!
usemayo ni kweli. Mengi alimtaja ra kuwa ni fisadi papa na kuanzisha bifu kubwa kati yao. Sasa ni lazima mengi aseme kitu -- iwapo anayofanya jk ni mazuri. Hata hivyo gazeti lake la nipashe leo halina habari hiyo ya jk kumnadi ra. Sijui katika electronic media zake.
Watanzania jamani msishabikie ujinga,leo mnaona majeshi yetu mabaya kwa kuwa mnaushabiki wa kisiasa,natakakuwaambia kama mnatka kujua nini maana ya kupotea kwa amani endeleeeni kuwashawishi watu kubeba mapanga na visu kudai udiwani na ubunge.nchi hii haiwezi kuangalia kaundi ka wachaga na wamasai wachache wanaotaka madaraka kwa nguvu kuipeleka kusiko takiwa ,mimi nazani muda umefika wote wanaotoa kauli kama za mbowe na slaa waakamatwe.
hv wengine mnafikiri kuumwa mpaka yawe marelia? Huyu anaumwa, akili yake siyo nzuri. Kwani wewe huoni jk na wanawe unaleta ukwele hapa! Nyambafu ......... Zako''@@@@watanzania jamani msishabikie ujinga,leo mnaona majeshi yetu mabaya kwa kuwa mnaushabiki wa kisiasa,natakakuwaambia kama mnatka kujua nini maana ya kupotea kwa amani endeleeeni kuwashawishi watu kubeba mapanga na visu kudai udiwani na ubunge.nchi hii haiwezi kuangalia kaundi ka wachaga na wamasai wachache wanaotaka madaraka kwa nguvu kuipeleka kusiko takiwa ,mimi nazani muda umefika wote wanaotoa kauli kama za mbowe na slaa waakamatwe.
mimi jana , wakati naangalia, taharifa ya habari kwa mara , ya kwanza chanel 10, nilipigwa namshangao, nikajiuliza hivi hii nchi inaelekea wapi?,IGP yuko wapi au SHIMBO ndo anakaimu, au wamechoka kazi ya kusafisa silaa, na kupanga mabomu yasije kuripuka tena, au michongoma haijarefuka,Hii kali, ina maana mwaka huu uchaguzi utalindwa na jeshi? Huku ni kufilisika kifikira, ni wehu, ni uendawazimu au ni kitu gani? Who is Shimbo katika mambo ya uchaguzi? Ina maana Mwema amestaafu. Atuondolee uchuro wake hapa. Yaani JWTZ ndiyo inayoshughulikia usalama wa uchaguzi? Kwani IGP anafanya nini? Ameshindwa kukamata maharamia wa Somalia na wahamiaji haramu anataka kushughulika na uchaguzi. Hii serikali ya Kikwete kweli imepinda!! Kama ndiyo hivyo, bora tu tuingie vitani wasitubabaishe hapa tushachoka na mfumo wa kibepari na kandamizi wa CCM.