Kuelekea Shirikisho la kisiasa la Afrika Mashariki, pongezi kwa Rais Magufuli!

Cicero

JF-Expert Member
Jan 20, 2016
2,924
3,072
Juzi katika pita pita zangu mjini, nikaona agizo la serikali la kutumika kwa nembo (bendera na wimbo) za Afrika Mashariki katika ofisi zote za serikali limetekelezwa vizuri. Ofisi za wizara zote hivi sasa ukiangalia pembeni mwa bendera ya taifa utakuta bendera ya Afrika Mashariki nayo inapepea. Tulivyoingia ndani kabla ya kuanza kikao ukapigwa wimbo wa taifa wa Tanzania then wimbo wa Afrika Mashariki.
Kama mtanzania na mwana afrika mashariki, nilifurahishwa sana na hilo, na ni vyema nikatoa pongezi za dhati kwa serikali ya awamu ya tano kwa hatua hiyo muhimu.
Haipendezi kuona Tanzania ilikuwa ni nchi ya kwanza kuridhia itifaki ya umoja wa fedha wa Afrika Mashariki wakati watanzania walio wengi hawajui hata bendera wala wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Isitoshe, mchakato wa kuandikwa katiba ya shirikisho la kisiasa uko full speed!
Kazi bado ni kubwa, na ni vyema serikali ikaendelea na kasi ii hii tutafika tu!
PROUDLY EAST AFRICAN!
upload_2016-7-7_23-20-11.png
 
Rwanda, Burundi, Uganda kuna madikteta sasa Tanzania nae anataka kuwa kama wao. Kwa uono wangu hili ni shirikisho la madikteta watupu.
Tofauti na Jumuiya ya enzi za Nyerere Jumuiya ya leo ni ya wananchi!
Hata hivyo.....bora hao madikteta watuingize tu then tutajipanga vizuri tukishaunda Shirikisho!
 
Tofauti na Jumuiya ya enzi za Nyerere Jumuiya ya leo ni ya wananchi!
Hata hivyo.....bora hao madikteta watuingize tu then tutajipanga vizuri tukishaunda Shirikisho!
Kuikosa sukari tu taabani, sasa ikija kuwa north korea itakuwaje?
 
Kuikosa sukari tu taabani, sasa ikija kuwa north korea itakuwaje?
Shirikisho la siasa la afrika mashariki litasaidia kuwadhibiti hao madikteta ulowataja mkuu hauoni hilo?
 
Back
Top Bottom