Kuelekea Nyerere Day 14 Oktoba 2020: Tumkumbuke Mwalimu...

zagarinojo

JF-Expert Member
Jul 26, 2020
2,622
2,835
Kuelekea Maadhimisho ya Nyerere Day tarehe 14.10.2020.
Akiwa kama muasisi na Baba Wa Taifa hili Mwalimu Julius Kambarage Nyerere anakumbukwa kwa mengi aliyoyafanya .

Likiwemo la kusaidia Tanganyika kupata uhuru wake kutoka kwa mabepari na mabeberu mnano tarehe 9.12.1961.

Anakumbukwa kwa mengi pia alizisaidia nchi nyingine za kiafrika kupata Uhuru wake.

Sasa ni miaka takribani 21 hatunaye tena lakini nukuu,maneno na ujasiri na ukakamavu na uongozi vitabaki kuwa kumbukumbu tosha kwa wale tuliosoma historia yake au hata wale waliomshuhudia akiwa hai

Tukielekea siku ya maadhimisho hebu tujikumbushe aliyoyafanya mwalimu na jinsi uongozi wake ulivyotukuka.

Unamkumbuka Mwalimu kwa lipi hasa?

Hizi ni baadhi ya nukuu za Mwalimu Julius Nyerere

"Hatuwezi kutatua matatizo yetu kwa kujidanganya kuwa hayapo"

"Elimu sio njia ya kuepukana na umasikini bali njia ya kupambana na umasikini"

"Uchumi katika nchi haupimwi na maskini wanaotumia usafiri wao Bali na matajiri wanaotumia usafiri wa umma"
 
Nikisomaga "uongozi wetu na hatima ya Tanzania"
Kuna sehemu anasema "Ccm sio mama yangu,nikiona chama chenye Sera nzuri na fikra za ukombozi wa kweli kwa Tanzania ntahamia hiko chama"
 
Mwalimu aliwahi kusema kwamba "Taifa hili linahitaji vijana shupavu, jeuri, wanaojiamini na wenye kuhoji mambo kuhusu watawala bila ya kuogopa na siyo wale wa akina ndiyo mzee".
Kama Lissu.

Pia mwalimu aliwahi kusema Ole wake Tanzania tusipoisaidia Nifanyalo nimeliweza kushauri nakuonya zaidi nifanye nini nimeshatokakktini, Naomba maanani jalia uilinde Tanzania.

# NI YEYE 2020
 
JK Nyerere alikubali mfumo wa mageuzi vyama vingi, akashawishi chama chake tawala kwa shingo upande wakakubali.Rai yangu kwa shuhuda na umuhimu checks and balance ni vyema CCM wakaridhia rasmi kwa kuruhusu mifumo huru.Dunia ya leo huwezi kuzuia mawazo mbadala.
 
Mwalimu aliwahi kusema kwamba "Taifa hili linahitaji vijana shupavu, jeuri, wanaojiamini na wenye kuhoji mambo kuhusu watawala bila ya kuogopa na siyo wale wa akina ndiyo mzee".
Kama Lissu.

Pia mwalimu aliwahi kusema Ole wake Tanzania tusipoisaidia Nifanyalo nimeliweza kushauri nakuonya zaidi nifanye nini nimeshatokakktini, Naomba maanani jalia uilinde Tanzania.

# NI YEYE 2020
Lissu amefuata nyayo za mwalimu za kuonesha uthubutu na ujasiri?
 
Mwalimu Jk Nyerere alisema.

"Udikteta ni selikali ya watu wachache ama kikundi cha watu kinachotunga sheria kandamizi atakayebisha atakipata cha moto".

Dikteta jiwe na Ndugai wamesimamia utungwaji wa sheria kandamizi
 
Alisema Watanzania wakikosa mafanikio nje ya CCM basi ipo siku watayatafuta nje ya CCM lisemwalo lipo ..........malizia
 
Alisema watu wanaposhindwa kutumia sera kuwashawishi wananchi wawachagu
Huanza kutumia "ukabila na udini" hapo ndipo matatizo huanzia
Ukabila na udini unagawa wananchi na kazi ya kiongozi ni kuwaunganisha wananchi
 
Back
Top Bottom