Paparazi Muwazi
JF-Expert Member
- Dec 23, 2007
- 310
- 79
Taarifa nilizopokea ni kwamba NEC ya CCM itakutana Dodoma kwa dharura kujadili kuhusu Kilimo. Wadadisi wa mambo wanasema kitendo cha kutanza kwa umma kuwa ajenda ni Kilimo ni katika kupunguza mjadala wa umma kuhusu kikao hicho kama ilivyokuwa kwa kikao cha Butiama. Lakini wachambuzi wa msingi wanasema ajenda zitakazojadiliwa ni Hali ya Maisha ya Watanzania baada ya kupanda kwa Bei ya Mafuta na Chakula, Tishio la Njaa, Suala la Mpasuko wa Kisiasa Zanzibar-hatma ya kura za maoni, Ripoti ya EPA, na Ripoti ya utekelezaji wa Kamati ya Pinda kuhusu Richmond. Kwa mujibu wa Mjumbe mmoja wa NEC, kuna kundi la wajumbe lina nia ya kushinikiza maamuzi ya kihistoria katika kikao hicho
PM
PM