real G
JF-Expert Member
- Feb 7, 2013
- 5,227
- 5,287
Jeshi la Polisi limeongeza askari na vifaa vyake Mkoani Dodoma ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu wa CCM ambao unatarajiwa kumchagua Rais Magufuli kama Mwenyekiti wa CCM Taifa.
Awali baraza la vijana wa CHADEMA walisema wangelisaidia jeshi la polisi kuzuia mkutano huo ili kuunga mkono kauli ya Magufuli ya kupiga marufuku mikutano ya kisiasa, lakini kamanda wa polisi wa mkoa huo Lazaro Mambosasa akasema hawaitaji msaada na watawasweka ndani wote watakaoingilia mkutano huo