kuelekea miaka 50 ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam

Kindimbajuu

JF-Expert Member
Jul 8, 2009
710
243
tukiwa tuna timiza miaka 50 ya chuo kikuu cha dar es salaam tunatakiwa tuangalie tuliko toka , tulipo na changamoto zipi zinatukabili huko tuendako. changamoto moja niionayo mimi ni hii ya matumizi sahii ya sayansi na teknolojia kwenye vyuo vyetu na nchi nzima kwa ujumla. nionavyo mimi chuo kikuu cha dar es salaam bado kinatakiwa kiwe makini ktk kutumia teknolojia ya habari, kisipoteze haki ya msingi ya wateja wake (ambao ni wanafunzi). kwa mfano ni hili la kuweka matokeo ya wanafunzi yakiwa yana toa usiri wa jina la mtu ma daraja alilopata kwenye mtandao. unaweza kusoma hii linki hii http://www.udsm.ac.tz/userfiles/201...011_12 examinations results (for display).pdf


hapa majina ya wanafunzi na matatizo yao yameanikwa, hii si sawa , haya si matumizi sahihi ya teknolojia ya mawasilianoa kwakuwa mawasiliano yanatumika wakati usiri wa mtu ukiwa unamwagwa kwa jamiii. je uongozi wa chuo kikuuu unaweza siku moja kuweka majina ya wafanyakazi wao na mishahara yao , ikiwa kama njia ya kuwafikishia ujumbe wafanyakazi juu ya mabadiliko ya mishahara?, kwanini hili linawezekana kwa wanfunzi tu??
tulia, tafakari, chukua hatua
 
Back
Top Bottom