Kuelekea Mechi ya Simba SC dhidi ya AS Vita Club, hatua ya Makundi Ligi ya Mabingwa Afrika 'Hatoki Mtu'

Simba kumbukeni Okwi,Juko, Mkude, Nyoni hawapo sasa huo ushindi bila hawa watu msahau aiseee......Okwi bado anamgomo anataka pesaaa zake

Sent using Jamii Forums mobile app
Acheni kusikiliza maneno ya mitaani. Huyo hapo Okwi aloshika kiuno na Nyoni, Jouko wote wamefanya mazoezi leo..NguvuMoja
IMG_20190313_175310_121.jpeg
 
Ila nilichowakubali mnawaogopa sana FC Mashujaa Musica kiasi kwamba hamtaki kuwasikia na hata kuliona jina mashujaa.
Habari za Mama zinahusu nini hapa..!

Jibu hoja Mashujaa na ligi ya mabingwa wapi na wapi..Kama huwezi mjadala na kutaniana kaa kimyaa Maluuni Waheed
 
Kuelekea mechi ya Simba SC dhidi AS Vita Club kutoka Kongo, hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Barani Afrika, mchezo utakaovurumishwa Jumamosi Machi 16, 2019 kunako Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, Hatoki Mtu.

Kocha wa Simba SC, Mbelgiji Patrick Aussems amesema na kusisitiza kuwa wanaelekeza nguvu na akili katika mechi hii ya mwisho huku akiongeza kuwa anajua anapambana na wapinzani wa namna gani kwenye ligi hii Mabingwa Afrika.

••Kulipewa Mwana.....Kulitaka Mwana

AS Vita Club haitoki salama, itapigwa vibaya kutokana na uwezo wa Simba SC kutumia vema Uwanja wa Taifa, MKAPA STADIUM, kwa kuwachinja wapinzani wao hatua ya makundi kila aliyetia mguu Kimataifa.

Vilevile kumbuka na fahamu kwamba kwenye kundi D hakuna timu ambayo imeshinda ugenini, wala kupoteza mchezo (kufungwa) nyumbani, kila timu imeshinda nyumbani kwake.

Yatasemwa mengi na uchambuzi wa kila aina kutoka pande zote zenye kufuatilia soka, lakini ukweli unabaki pale pale kwamba hakuna timu imeshinda nje ya mji wake kwenye kundi D, hivyo tunatarajia Simba SC itaigaragara vilivyo AS Vita Club na Washirika wake hivyo kuweza kufuzu katika hatua ya robo fainali ligi ya Mabingwa Afrika.

Timu ushindi JF Simba SC, sembo OKW BOBAN SUNZU Shunie King Ngwaba Sapta Sapta Tui barafuyamoto toxic9 Jaby'z Mshuza2 nyakubonga Twende sasa hapa Ubaoni..Na uwanja wa Taifa.

This Is Simba SC...SimbaNguvuMoja.

View attachment 1044481View attachment 1044483
Mikia kwa kujipa moyo.......
 
Hivi toka tumeanza michuano hii ya ligi ya mabingwa afrika 2018/2019, hivi huoni kinachofanyika? Huko kujipa moyo ni kupi?

Nyie endelea kufuga pale bwawani..SimbaNguvuMoja
Mmefanya nini wakati nyie ndo wa mwisho kwenye kundi? Mmekula +255 labda ndo jambo linaloshangaza
 
Back
Top Bottom