Kudai haki za msingi za yeyote ni masuala yasiyo hitaji ridhaa za asiyehusika na hasa mlalamikiwa.
Haki za msingi kwa mlalamikaji haziwezi kutegemea ukubali wa mlalamikiwa.
Mlalamikaji na ategemee machungu kamili kutoka kwa mlalamikiwa, ujira wa kutokuchoka kwake ni kupatikana kwa haki husika.
Huku ni kuchezana shere ambako ni muhimu mlalamikiwa akafahamu kuwa hakukubaliki.
Kama wewe si mlalamikiwa na unadhani hauhusiki kwenye madai ya haki husika, mambo ya pilipili usizozila ndipo yanapoingia hapo!
Ni sahihi kuombana kutowashwa washwa enyi mnaodhani kuwa hamhusiki kwenye agenda hii yenye maslahi makubwa kwa nchi yetu.
Nakazia: Kuelekea Makongamano ya kudai katiba mpya, haki za msingi za watu na ziheshimiwe kwani haki huinua taifa.
Amandla!
Haki za msingi kwa mlalamikaji haziwezi kutegemea ukubali wa mlalamikiwa.
Mlalamikaji na ategemee machungu kamili kutoka kwa mlalamikiwa, ujira wa kutokuchoka kwake ni kupatikana kwa haki husika.
Huku ni kuchezana shere ambako ni muhimu mlalamikiwa akafahamu kuwa hakukubaliki.
Kama wewe si mlalamikiwa na unadhani hauhusiki kwenye madai ya haki husika, mambo ya pilipili usizozila ndipo yanapoingia hapo!
Ni sahihi kuombana kutowashwa washwa enyi mnaodhani kuwa hamhusiki kwenye agenda hii yenye maslahi makubwa kwa nchi yetu.
Nakazia: Kuelekea Makongamano ya kudai katiba mpya, haki za msingi za watu na ziheshimiwe kwani haki huinua taifa.
Amandla!