idawa
JF-Expert Member
- Jan 20, 2012
- 25,284
- 38,312
Binafsi nilijiandikisha tena mara mbili lakini nimefuatilia namba zangu NIDA kama naomba mkopo benki. Hakuna nilichoambulia. Uzembe wa NIDA usumbufu nabebeshwa mimi.
Matokeo yake naambiwa nijiandikishe upya, yaani nianze taratibu za kwenda kwa Mtendaji, Uhamiaji halafu NIDA.
---
Mambo ya msingi ya kufanya kabla ya laini kufungwa kama huna namba ya kitambulisho cha NIDA
---
Dakika chache kutoka sasa simcard zisizosajiliwa zitazimwa
---UPDATE 21 January, 2020---
TCRA kufungia laini zisizosajiliwa kwa awamu
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), James Kilaba amesema uzimaji wa laini za simu ambazo hazijasajiliwa kwa alama za vidole unafanyika kwa awamu
Amesema zoezi hilo lililoanza jana Januari 20, 2020 linafanyika kwa awamu ili kuondoa usumbufu na hadi kufikia jana usiku saa nne walikuwa wamezima laini 975,041
Amesema kundi la kwanza waliozimiwa laini ni watu 656,091 ambao wana Vitambulisho vya Taifa au namba lakini hawajasajili laini zao
Amebainisha kuwa kundi la pili ni watu 318,950 waliosajili laini zao kwa Kitambulisho cha Taifa kabla ya kuanza mfumo wa kusajili kwa alama za kidole
Amesema, “Tunazima kidogo kwa sababu ya mambo ya kitaalamu, hauwezi ukazima laini milioni tano au 10 kwa mara moja kwa maana watajazana kwenye kusajili kitu kinachofanya mifumo ya Nida inaelemewa.”
Matokeo yake naambiwa nijiandikishe upya, yaani nianze taratibu za kwenda kwa Mtendaji, Uhamiaji halafu NIDA.
---
Mambo ya msingi ya kufanya kabla ya laini kufungwa kama huna namba ya kitambulisho cha NIDA
Kuthibitisha kama laini yako ya simu imesajiliwa kwa alama za vidole piga *106# chagua 1
Kwanza niwape pole wale wote ambao wanashinda ofisi za NIDA bila kufanikiwa.
Ukweli process ya vitambulisho ni ndefu sana.
Kwa wale ambao hawana vitambulisho vya NIDA unaweza tafuta ndugu yako ukasajili kwa kutumia kitambulisho chake, kitambulisho kimoja kinaruhusiwa kusajili laini 10.
Kwa wale ambao hawajasajili hakikisha fedha zote umezitoa na kama umezoea kutumia mobile banking hakikisha kadi yako ya ATM ipo valid otherwise utapata usumbusu mkubwa sana kupanga foleni bank na kupata ATM mpya inachukua more than one week.
Kwa NIDA nashauri watume majina na namba za wananchi ambao wameshajaza form na hawajapata namba zao ili mitandao ya simu (MNO) wasiwafungie kwa sababu hawana hatia.
Nawatakia weekend njema.
------
Waziri Nditiye asema hekima itatumika usajili wa laini kwa wasio na vitambulisho vya Taifa
Serikali ya Tanzania imesema itatumia hekima kuwasaidia wananchi walioshindwa kusajili laini za simu kwa sababu ya kukosa kitambulisho cha Taifa na namba licha ya kuanza mchakato wa kupata kitambulisho hicho.
Imesema wananchi hao taarifa zao zipo katika Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), huenda wamekosa kitambulisho au namba kwa sababu zilizo nje ya uwezo wao.
Hayo yameelezwa leo Jumapili Januari 19, 2020 na naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Atashasta Nditiye katika mkutano wa ndani wa CCM mkoani Kigoma.
"Serikali itaona jinsi ya kutumia hekima kwa wananchi ambao taarifa zao zipo katika ofisi za Nida kuona namna ya kufanya lakini kwa wengine ambao hawajajaza fomu laini zao zitazimwa,” amesema Nditiye.
Amesema ambao laini zao zitazimwa ni wale waliosajili laini chache na kuacha nyingine licha ya kuwa na kitambulisho hicho.
Amebainisha kuwa usajili wa laini za simu ni endelevu licha ya baadhi ya wananchi kupuuza.
Chanzo: Mwananchi
NIDA: Namba za Utambulisho (NIN) Milioni 6 bado hazijatumika kusajili laini za simu
Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imesema kuwa inaendelea na zoezi la usajili na utambuzi wa watu, uzalishaji wa namba za utambulishi wa taifa na vitambulisho na ugawaji wake kwa wananchi ili waweze kuvitumia kusajili kadi (laini ) za simu kwa alama za vidole na huduma nyingine. Katika...www.jamiiforums.com
---
Dakika chache kutoka sasa simcard zisizosajiliwa zitazimwa
Imebakia robo saa kutimia saa sita kamili ya tarehe 20. January. 2020.. Muda ambao ni kikomo cha mwisho kwa wasiosajiliwa kwa alama za vidole wafanye hivyo la sivyo kuanzia saa sita na dakika moja laini zote ambazo hazijafanya USAJILI WA vidole zitazimwa... Ina maana baada ya hapo laini kwenye simu husika haitafanya kazi tena...
Huu ni mtego wa hatari mno kwa serikali kama haijajipanga vema na tayari kuna baadhi ya wananchi wameshaanza kubeza hiyo hatua kama hili zoezi la kuzima lisipofanyika ama lisipofanikiwa
Kuna machache kwenye mengi ya kujadili hapa...
1. Je serikali imeshafanya upembuzi yakinifu kwenye hili, hasara na faida zake? Je hasara ni zipi na faida ni zipi?
2. Je muda huu mamlaka ya mawasiliano kupitia mitandao husika wako kazini wakisubiri dakika zilizobakia waminye kitufe cha kuzima laini? Je mamlaka kupitia mitandao husika ina uwezo na zana zenye nguvu za kuweza kuzima laini zaidi ya milioni 20 ambazo bado hazijapata usajili?
3. Je hili haliwezi kuchukuliwa kama uhujumu uchumi kutokana na serikali kukosa mapato makubwa ndani ya saa 24 zijazo? Kuanzia miamala ya pesa, manunuzi ya muda wa maongezi, vifurushi vya data nknk?
4. Je serikali haiwezi kushitakiwa kwa uzembe na usumbufu? kwakuwa kama wangetuma watu wao kwenye vituo vya usajili wangeona wananchi wanavyopatishwa tabu kwenye kupata vitambulisho vya taifa kwa ajili ya kupata usajili wa simcard?
5. Dhihaka ni jambo baya sana kwenye mambo muhimu ya KITAIFA.. Lakini mkuu wa mkoa wa DSM katoa dhihaka kwa wale watakaozimiwa simu zao usiku huu kama ni watu waliokuwa na michepuko... Je ana ushahidi na ithibati kwenye hili? Nini maana ya kuwa kiongozi?
Tayari ni saa sita na dakika tatu siku ya tar 21 January 2020... Nadhani muda huu tayari zoezi la kuzima limeshaanza... Likifanikiwa hili kuna madhara mengi yatatokea usiku huu.. Kuna dharura hazitafanyiwa kazi.. Kuna vifo vitatokea kwa kukosa mawasiliano... Kuna watu watakwama kusafiri, kutuma pesa ya dawa, chakula nk kwa kukosa kufanya miamala nknk...
Kuna nafasi bado ya kutafakari kwenye hili... Lakini je serikali iko tayari kujishusha na kukiri wazi kuwa haikutafari vema kwenye hili? Muda utasema kukipambazuka.. Lakini tayari kejeli zimeshaanza
View attachment 1329002
Jr
---UPDATE 21 January, 2020---
TCRA kufungia laini zisizosajiliwa kwa awamu
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), James Kilaba amesema uzimaji wa laini za simu ambazo hazijasajiliwa kwa alama za vidole unafanyika kwa awamu
Amesema zoezi hilo lililoanza jana Januari 20, 2020 linafanyika kwa awamu ili kuondoa usumbufu na hadi kufikia jana usiku saa nne walikuwa wamezima laini 975,041
Amesema kundi la kwanza waliozimiwa laini ni watu 656,091 ambao wana Vitambulisho vya Taifa au namba lakini hawajasajili laini zao
Amebainisha kuwa kundi la pili ni watu 318,950 waliosajili laini zao kwa Kitambulisho cha Taifa kabla ya kuanza mfumo wa kusajili kwa alama za kidole
Amesema, “Tunazima kidogo kwa sababu ya mambo ya kitaalamu, hauwezi ukazima laini milioni tano au 10 kwa mara moja kwa maana watajazana kwenye kusajili kitu kinachofanya mifumo ya Nida inaelemewa.”