snochet
JF-Expert Member
- Mar 31, 2011
- 1,405
- 1,095
habari wandugu,
leo nimekuja na viswali vyangu baada ya kupita website ya tcra na kukosa majibu yakinifu kuhusu huku kuhamia kwa digitali kutoka analojia(digital migration),na maswali yangu ni kama yafuatavyo.
1.je kuhamia digitali kutatunufaishaje sisi watumiaji?
2.kati ya watumiaji na warusha matangazo ni nani anafaidika zaidi?
3.TCRA inafaidikaje kwa kubadili mfumo huu?
4.kuna ulazima sana wa kuhamia digitali?
5.kwa sisi wenye decoder za satellite kama za "mediacom" ina maana ndo mwisho wa kutumia ma dish yetu ya satellite?
6.je ni tofauti gani zipo kwenye hivi ving'amuzi wanavyotaka tununue vinavyozidi satellite dish?
7.je hivi ving'amuzi vinanyakua mawasiliano kutoka kwenye satellite au katika Terrestirial transmission towers(kama za simu),ne je zimeshafungwa kila mkoa/wilaya?
8.Internet Protocol (IP TV–internet) iko supported na hivi ving'amuzi,au miaka kadhaa ijayo watakuja kutuambia tubadilishe tena?
hiyo hapo chini writtten in blue ndo maelezo ya TCRA,nadhani wanaweza wakafanya jambo la maana zaidi zaidi ya jingle yao ya kimafumbo ambayo haieleweki kirahisi na mwananchi wa kawaida,kwa muda huu mfupi uliobaki nawashauri wawe na vipindi maalum ,kama ilivyokuaga ile ya kusajili namba za simu,watu walielewa zaidi.
"JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA
TAARIFA KWA UMMA
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UZINDUZI WA TANGAZO (JINGLE) NA
WIMBO WA KUHAMASISHA UHAMAJI WA TEKNOLOJIA YA
UTANGAZAJI KUTOKA ANALOJIA KWENDA DIJITALI
1. Wakati Tanzania ikielekea katika ukomo wa kutumia Teknolojia ya
Utangazaji ya Analojia, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania leo
inazindua tangazo (jingle) na wimbo wa kuhamasisha umma
kujiandaa na mabadiliko haya. Tangazo na wimbo unaitwa "Ni
Wakati wa Dijitali Tanzania" vinaanza kutumika rasmi kesho
tarehe 1 Desemba 2012;
2. Tangazo hilo na wimbo vyote vinalenga katika kueleimisha,
kukumbusha na kuhamasisha umma umuhimu na faida za
teknolojia mpya ya dijitali;
3. Tangazo hilo na wimbo vyote vinaelekeza wananchi kutotupa
televisheni zao za zamani kwa kuwa zitaendelea kutumika kwa
kuunganishwa na king'amuzi.
4. Sambamba na kuelimisha na kuhamasisha, tangazo na wimbo
vyote vinasisitiza kuzimwa kwa mitambo ya Analojia tarehe 31
Disemba 2012 kwa mujibu wa kanuni za Mamlaka ya Mawasiliano
kuhusu mifumo ya dijitali za mwaka 2011;
5. Mamlaka ya Mawasiliano inapenda kusisitiza kuwa wananchi
wanunue ving'amuzi kutoka kwa Mawakala waliosajiliwa na
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania na wapate garantii ya
ving'amuzi hivyo;
6. Ni matarajio ya Mamlaka ya Mawasiliano kuwa wananchi na watoa
huduma za dijitali watatoa ushirikiano ili kufanikisha uhamiaji toka
mfumo wa analojia kwenda dijitali.
Imetolewa na:
Mkurugenzi Mkuu
MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA
mwisho kabisa,naombeni wenye ujuzi na majibu kwa maswali yangu wanijuze
cc: Young Master MziziMkavu, cielo watu8 Bujibuji Mzee Mwanakijiji Mbuzi Mzee Nicas Mtei Invisible The Boss Mtambuzi Mkuu rombo Boflo
leo nimekuja na viswali vyangu baada ya kupita website ya tcra na kukosa majibu yakinifu kuhusu huku kuhamia kwa digitali kutoka analojia(digital migration),na maswali yangu ni kama yafuatavyo.
1.je kuhamia digitali kutatunufaishaje sisi watumiaji?
2.kati ya watumiaji na warusha matangazo ni nani anafaidika zaidi?
3.TCRA inafaidikaje kwa kubadili mfumo huu?
4.kuna ulazima sana wa kuhamia digitali?
5.kwa sisi wenye decoder za satellite kama za "mediacom" ina maana ndo mwisho wa kutumia ma dish yetu ya satellite?
6.je ni tofauti gani zipo kwenye hivi ving'amuzi wanavyotaka tununue vinavyozidi satellite dish?
7.je hivi ving'amuzi vinanyakua mawasiliano kutoka kwenye satellite au katika Terrestirial transmission towers(kama za simu),ne je zimeshafungwa kila mkoa/wilaya?
8.Internet Protocol (IP TV–internet) iko supported na hivi ving'amuzi,au miaka kadhaa ijayo watakuja kutuambia tubadilishe tena?
hiyo hapo chini writtten in blue ndo maelezo ya TCRA,nadhani wanaweza wakafanya jambo la maana zaidi zaidi ya jingle yao ya kimafumbo ambayo haieleweki kirahisi na mwananchi wa kawaida,kwa muda huu mfupi uliobaki nawashauri wawe na vipindi maalum ,kama ilivyokuaga ile ya kusajili namba za simu,watu walielewa zaidi.
"JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA
TAARIFA KWA UMMA
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UZINDUZI WA TANGAZO (JINGLE) NA
WIMBO WA KUHAMASISHA UHAMAJI WA TEKNOLOJIA YA
UTANGAZAJI KUTOKA ANALOJIA KWENDA DIJITALI
1. Wakati Tanzania ikielekea katika ukomo wa kutumia Teknolojia ya
Utangazaji ya Analojia, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania leo
inazindua tangazo (jingle) na wimbo wa kuhamasisha umma
kujiandaa na mabadiliko haya. Tangazo na wimbo unaitwa "Ni
Wakati wa Dijitali Tanzania" vinaanza kutumika rasmi kesho
tarehe 1 Desemba 2012;
2. Tangazo hilo na wimbo vyote vinalenga katika kueleimisha,
kukumbusha na kuhamasisha umma umuhimu na faida za
teknolojia mpya ya dijitali;
3. Tangazo hilo na wimbo vyote vinaelekeza wananchi kutotupa
televisheni zao za zamani kwa kuwa zitaendelea kutumika kwa
kuunganishwa na king'amuzi.
4. Sambamba na kuelimisha na kuhamasisha, tangazo na wimbo
vyote vinasisitiza kuzimwa kwa mitambo ya Analojia tarehe 31
Disemba 2012 kwa mujibu wa kanuni za Mamlaka ya Mawasiliano
kuhusu mifumo ya dijitali za mwaka 2011;
5. Mamlaka ya Mawasiliano inapenda kusisitiza kuwa wananchi
wanunue ving'amuzi kutoka kwa Mawakala waliosajiliwa na
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania na wapate garantii ya
ving'amuzi hivyo;
6. Ni matarajio ya Mamlaka ya Mawasiliano kuwa wananchi na watoa
huduma za dijitali watatoa ushirikiano ili kufanikisha uhamiaji toka
mfumo wa analojia kwenda dijitali.
Imetolewa na:
Mkurugenzi Mkuu
MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA
mwisho kabisa,naombeni wenye ujuzi na majibu kwa maswali yangu wanijuze
cc: Young Master MziziMkavu, cielo watu8 Bujibuji Mzee Mwanakijiji Mbuzi Mzee Nicas Mtei Invisible The Boss Mtambuzi Mkuu rombo Boflo
Last edited by a moderator: