Kuelekea 2020:Asilimia kubwa ya wenye access na internet kupitia simu za mikononi(smartphone),laptop,n.K, sidhani kama watawachagua wagombea wa CCM

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,014
144,371
Kwa sasa ninaamini asilimia kubwa ya watanzania wanapata habari za kina za nini kinaendelea katika nchi hii kupitia mitandao na si vyombo rasimi vya habari kama magazeti na television hasa juu ya yale mambo ambayo si mazuri kusikia au kuonekana machoni mwa watu.

Vile vile,ni kupitia mitandao hii, watu wanasikia kupitia clip zinazosambazwa mitandaoni matamshi ya baadhi ya wanasiasa, matamshi ambayo media ama zinakwepa kuyaandika au kuandika huku wakiacha baadhi ya maneno(wakichuja) lakini mitandaoni clip zinasambaa kama zilivyo bila kujali uliongea au kuropoka nini(hakuna kinachofichwa).

Pia,ni kupitia mitandao hii, propaganda zote za wanasiasa wa awamu hii zinajibiwa,kuchambuliwa na kutolewa ufafanuzi unaosaidia watu kuelewa/kuchambua pumba na mchele.

Kwa kifupi,mitandao kwa sasa ndio inasaidia watanzania kujua yale yanayofichwa pamoja na yale yanayopotoshwa hivyo nina kila sababu ya kuamini asilimia kubwa ya watu wenye access na internet mpaka kufikia 2020, watakuwa na ufahamu na uelewa wa kutosha juu ya namna mambo yanavyokwenda katika nchi yao kwa sasa na iwapo mambo haya(utekaji,unyanyasaji wa raia,watu kupotea,kauli za viburi na kejeli za baadhi ya wanasiasa,utendaji wa wabunge na Bunge lenyewe ,n.k) yataendelea kutokea kila siku,binafsi sioni uwezekana wa wagombea wengi wa CCM kupigiwa kura za ndio na watanzania walioa na access na internet kupitia simu zao za mikononi,kompyuta mpakato(laptop,n.k).

Nasema haya kwasababu,ukiacha matendo na kauli za wanasiasa mmoja mmoja,CCM ndio chama tawala kinachounda serikali hivyo wao na chama chao na wagombea wao ndio watakaobeba lawama na kuwajibishwa na wapiga kura kupitia sanduku la kura.

Naelewa tume si huru, ila maamuzi ya wananchi watayaona kupitia kura zao bila kujali nani anatangazwa mshindi(ukweli watauona kwenye ballot papers na wataelezeana).
 
Unajua kuna muda nadhan Rais analishwa matango pori na watu wanaompa ripoti kinachojiri kila siku.....I wish angekua anapata muda waku peruse kwenye social media rather than relying on briefings from his subordinates!
 
Unajua kuna muda nadhan Rais analishwa matango pori na watu wanaompa ripoti kinachojiri kila siku.....I wish angekua anapata muda waku peruse kwenye social media rather than relying on briefings from his subordinates!
Kwenye mitandao wamejaa pro-fisadi ndiyo wanaonyooshwa unategemea nini?
 
Kwa sasa ninaamini asilimia kubwa ya watanzania wanapata habari za kina za nini kinaendelea katika nchi hii kupitia mitandao na si vyombo rasimi vya habari kama magazeti na television hasa juu ya yale mambo ambayo si mazuri kusikia au kuonekana machoni mwa watu.
Kwa siasa za matukio kama ya kuvunja line za voda,ikulu mtaiona kwenye tv tu
 
Mawazo ya mleta Uzi hayana ukweli kwa sababu kuu mbili.
1. Watz wengi hatuwezi kusoma makala hii Ni kutokana na mfumo wa elimu iliyopp na hivyo kuondoa uwezekano wa ujuzi wa kutosha --- uchawi huu umefaa Sana. Waliowengi wanaingia mitandaoni sio kuipata habari Bali kuipata burdan
2. Kwa jinsi maisha yalivyobana hata kupata bando issue
 
naanzaje sasa kuanza kuacha kumchagua MAGU? ninani anaefaa kuongoza hii nchi na tukaendelea na heshima iliyopo sasa mtaani? vijana wengi tulizowea mtelemko. umeajiliwa leo baada ya mwenzi 1 unakwiba fedha za uma unanyanyasa watu mtaani. lazima tuwe na shukrani mda mwingine MAGUFULI ni binaadam anamapungufu yake,lakini sehem kubwa kaitendea haki hii nchi hadi hapa ilipo.
2020 nitamchagua RAISI wangu MAGUFULI 👏👏👏👏👏👏👏
 
Nadhani watu wengi wenye uelewa haijalishi wako mitandaoni au laah watachagua wagombea kutokana na sifa zao na utendaji wao kazi, pia wataanglia rekodi ya chama husika katika awamu iliyopita. Zile zama za kuchagua mgombea kisa yupo chama fulani ilhali ni mbovu sidhani kama watanzania ni wajinga kiasi hicho.

Vyama vinapaswa kuteua wagombea wenye sifa kama za Raisi JPM chama kitakacho fanya hivyo mimi naimani kitapata wabunge na madiwani wakutosha lakini wakituwekea wagombea ambao hawana rekodi yoyete ya kiutendaji zaidi ya kubwabwaja tu au waliokwisha tawala kwa muda mrefu bila mafanikio yeyote wengi hawataenda kupiga kura.
 
Nadhani watu wengi wenye uelewa haijalishi wako mitandaoni au laah watachagua wagombea kutokana na sifa zao na utendaji wao kazi, pia wataanglia rekodi ya chama husika katika awamu iliyopita. Zile zama za kuchagua mgombea kisa yupo chama fulani ilhali ni mbovu sidhani kama watanzania ni wajinga kiasi hicho.

Vyama vinapaswa kuteua wagombea wenye sifa kama za Raisi JPM chama kitakacho fanya hivyo mimi naimani kitapata wabunge na madiwani wakutosha lakini wakituwekea wagombea ambao hawana rekodi yoyete ya kiutendaji zaidi ya kubwabwaja tu au waliokwisha tawala kwa muda mrefu bila mafanikio yeyote wengi hawataenda kupiga kura.
Hivi wewe kama uko timamu na unafuatilia yanayoendelea Bungeni kupitia mitandao na hata vyombo vya habari,unapata wapi hamu ya kuchagua wabunge wa CCM waliogeuka watetezi wa serikali?

Wabunge hawa wa CCM wako kulinda masilahi ya wananchi au cham chao?

Hivi kweli unaweza kuchgua watu waliopitisha utitiri wa sheria za hovyo hovyo zinazokandamiza wananchi kama sheria ya Bodi ya Mikopo inayonyonga watu wa kukata asilimia 15 ya mshara kulipia mkopo wa Bodi na huu ukiwa ni mfano mmoja tu sheria kandamizi walizopitisha?!
 
Back
Top Bottom