Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,467
- 113,582
- Thread starter
- #41
1. Tatizo kubwa la Watanzania sio au adui mkubwa wa Tanzania sio CCM, CCM is just the vehicle, haikujiweka
hapo ilipo, imewekwa, hivyo tatizo sio CCM iliyowekwa, bali tatizo ni walioiweka CCM hapo ilipo!. That simply
means, tatizo ni sisi Watanzania tulioiweka CCM madarakani and it plays games on us again and again na sisi
tukiendelea kuiweka madarakani again and again na sitashangaa kama hata 2015, tukairudisha tena!.
Wananchi hasa wa vijijini wameachwa katika ujiinga unochangia katika kudumisha umaskini mkubwa wa hali na mali. Zingatia uduni wa elimu na uwezo mdogo wa ku "analyze" issues. CCM imedhoofisha suala la elimu systematically ikijua wazi kuwa taifa lenye watu walioelimika wataipa upinzani mkubwa na kwa hili imefanikiwa sana. Usishangae 2015 CCM ikarudi kwani CCM imerekebisha hiyo hali? Kumbuka sakata la walimu we acha tu.
Mkuu makundi4619, ndio maana nasisitiza "reaching out" Wapinzani waachane kabisa na CCM, concentration ielekezwe kwenye reaching out strategy to change the mindset ya wapiga kura, ili kwanza kuwahamasisha kujitokeza kwa wingi kujiandikisha, kisha wajitokeze kwa wingi kupiga kura!.
Uchaguzi uliopita JK amechaguliwa kwa kura milioni 5!, waliojiandikisha ni milioni 20, waliojitokeza kupiga kura ni milioni 8, hii inamaana kuna watu milioni 12, walijiandikisha lakini hawakujitokeza kupiga kura kwa sababu zozote zile, ile wengi wao hawakujitokeza kutokana na kukata tamaa kuwa hata wapige vipi kura, itakuwa ni kujisumbua tuu, matokeo yatakuwa ni yale yale!. Hawa watu sasa ndio upinzani unatakiwa kuhangaika nao!.