Elections 2015 Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni ...

Pasco, unajua mada zako unazipanga vizuri, unaziandika vizuri na unazifafanua vizuri kwa lugha rahisi kiasi kwamba hata kama kimantiki si kweli watu wengi wanaweza kukubaliana na hoja zako? Ndivyo ilivyo hata kwa hoja yako hii ya leo.

Kiukweli kulekea elfu mbili na kumi na tano adui mkubwa wa Chadema ni…..CCM.

Dhana kwamba adui mkubwa wa watanzania si CCM bali ni sisi wenyewe siyo sahihi sana. Ni kweli kwamba kuna vi element fulani vya utamaduni wa kitanzania vinavyotubakisha sana nyuma lakini adui mkubwa ni yule anayecapitalize kwenye udhaifu wetu ili kuendelea kutunyonya na kutukandamiza. CCM haina huruma, haina tofauti na mkoloni wa kiarabu au kijerumani aliyetumia ukarimu wetu, upole wetu na kukosa elimu kwetu ili kujinufaisha juu ya migongo yetu. Ni kweli, hata hivyo, kwamba njia ya kumshinda adui wa namna hii ni kusambaza elimu ya uraia. Hii inatusaidia sana kuongeza ukali kidogo tunapodai haki zetu za kikatiba na kumpinga hasa pale anapoleta uhuni na ndicho Chadema wanachofanya.
Mkuu zimmerman, kwanza nakushukuru sana kwa sababu mpaka sasa, hii thread imeshamkomboa kifkra mtu angalau mmoja ambaye ni wewe!. Kitendo tuu cha kukubali kuwa "Dhana kwamba adui mkubwa wa watanzania si CCM bali ni sisi wenyewe siyo sahihi sana" hii kauli peke yake imenifariji kuwa dhana hii siyo sahihi sana inamaanisha ni sahihi kidogo!, kwangu uelewa kidogo tuu unatosha kuleta ukombozi wa kweli wa pili wa Mtanzania.

Wewe mkuu Zimme, jifikirie kama wewe ni mlenga shabaha, umemaliza risasi zako zote ila umebakisha risasi moja tuu ya mwisho iliyosalia ndani ya bunduki yako na mbele yako unawaona adui wawili, mmoja ni lile lidubwana kubwa linalotisha linaloitwa CCM ambalo limebebwa na adiu wa pili anayeitwa watu!. Jee utaitumia hiyo risasi yako kulitarget hili dubwana CCM ulilenge, ulishoot au life, au lijeruhiwe na kuanguka chini na kuanza kugalagala au ndipo life, au lisalimike!.

Adui wa pili ni wale watu waliolibeba lile dubwana CCM, ambapo ukimlenga tuu mmoja, wate wataliachia hilo dubwana CCM liporomoke, na bila hao watu, lidubwana CCM, haliwezi kusimama lenyewe!, jee wewe utamtarget adui yupi kati ya hao?!.

Opposition siku zote wanalitarget hilo dubwana, as a result wanalijeruhi, lakini kwa vile wale wanaolibeba wako intact, no matter lijeruhiwe vipi, ikifika uchaguzi, hulibeba tena na kuliwezesha kuendelea kuwakalia hao waliolibeba hivyo kuendelea kupeta uchaguzi hadi uchaguzi!.

Lakini ukiitumia hiyo risasi yako moja ya ngama, kutarget ule mhimili hilo dubwana liliposhikilia na kusimamia, hutaligusa hilo dubwana, bali utaisambaratisha nguzo yake dubwana linaloitegemea, hivyo kupelekea nguzo kukatika na dubwana kuporomoka, na bila hiyo nguzo, dubwana haliwezi kusimama peke yake, litaishia kujifia natural death!.

Kwani CCM ni nini?, inategemea nini ili kuendelea kuwa madarakani?, hutumia mbvinu gani ili kuendelea kuchaguliwa, na jee wanaichagua hiyo CCM ni kina nani?, nikimaanisha determinant factor ya CCM kuchaguliwa ni nani kama sio watu?!.

Nachukua baadhi ya mistari yako "aliyetumia ukarimu wetu, upole wetu na kukosa elimu kwetu ili kujinufaisha juu ya migongo yetu. Ni kweli, hata hivyo, kwamba njia ya kumshinda adui wa namna hii ni kusambaza elimu ya uraia. Hii inatusaidia sana kuongeza ukali kidogo tunapodai haki zetu" mwisho wa kunukuu. Hayo maneno niliyobold, wetu, wetu, kwetu, yetu ​na zetu, ni kinanani!?, jibu hao ni sisi, ni sisi ndio tunaiweka CCM madarakani kwa kura zetu!. Kama tutaendelea kuitarget CCM badala ya kuwa target watu, we will be doing the same mistake again and again, na CCM itaendelea kupeta kwa ku capitalize on people!.

Kinachoipa CCM ushindi ni kipi?, lets deal na kinachoipa CCM ushindi na sio ku deal na CCM!.

Pasco.
 
Pasco bahasha zitaua taaluma yako Mkuu!

TUMBIRI (PhD, University of HULL - UK),
tumbiri@jamiiforums.com

Mkuu Tumbiri, hizo bahasha zitaiua taaluma yangu ipi kati ya hizi ,

mimi ni mwandishi wa habari wa kujitegemea,
mimi ni mtangazaji wa kujitegemea
mimi ni producer wa kulipwa
mimi ni media consultant wa kulipwa
mimi ni political advisor wa kulipwa
na kitaaluma nimesomea LL.B ya UDSM nikiamua nafanya tuu petition na kuwa registered as an advocate,

Sasa hizi bahasha zitakazo iua taaluma yangu ni zipi hazwa na taaluma itakayo uliwa ni ipi kati ya hizo?.

Nimeshawahi kusema humu sio mara moja wala mara mbili kuwa nilipoikuwa mwandishi tuu wa habari, bahasha nimezipokea sana, na sasa kama mshauri wa habari, hizo bahasha mimi ndio nazigawa with clear and honest conscious kuwa bahasha za uwezeshaji is the right thing na ni haki za msingi za waandishi kuwezeshwa ili waweze kutimiza majukumu yao ya kila siku!.

N.B hili la bahasha, nimelifafanua vizuri hapa waandishi-wa-habari-na-bahasha-sio-kila-bahasha-ni-rushwa
 
There is no such thing as a magic bullet that can shoot all the birds. All that is required to remove CCM from power is combination of several strategies including the Mafia style strategy.
 
Mkuu Tumbiri, hizo bahasha zitaiua taaluma yangu ipi kati ya hizi ,

Mimi ni Mwandishi wa habari wa kujitegemea,
Mimi ni Mtangazaji wa kujitegemea
Mimi ni Producer wa kulipwa
Mimi ni Media Consultant wa kulipwa
Mimi ni political Advisor wa kulipwa
na kitaaluma nimesomea LL.B ya UDSM nikiamua nafanya tuu petition na kuwa registered as an advocate.

Sasa hizi bahasha zitakazo iua taaluma yangu ni zipi hazwa na taaluma itakayo uliwa ni ipi kati ya hizo?.

Nimeshawahi kusema humu sio mara moja wala mara mbili kuwa nilipoikuwa mwandishi tuu wa habari, bahasha nimezipokea sana, na sasa kama mshauri wa habari, hizo bahasha mimi ndio nazigawa with clear and honest conscious kuwa bahasha za uwezeshaji is the right thing na ni haki za msingi za waandishi kuwezeshwa ili waweze kutimiza majukumu yao ya kila siku!.

N.B hili la bahasha, nimelifafanua vizuri hapa waandishi-wa-habari-na-bahasha-sio-kila-bahasha-ni-rushwa
Pasco,
Taaluma siyo lazima uwe na cheti au upite formal education system ndiyo uwe recognized as specialist in that field. Kwa wale tunaojenga nyumba zetu bila kutumia Registered Engenering Company huwa tunawatumia mafundi wa mitaani. Wale watu ukiwachunguza vizuri wengi wao hawajasome ujenzi wa nyumba. Wamejua through experience. Na ukiwapa nyumba kukujengea hakika wanakujengea nyumba nzuri kama Engeneer mwenye BSc in Civil Engeneering.

Mfano mwingine umeutoa wewe mwenyewe. Umesema umesoma BA L.L.B (UDSM) lakini kwa sasa hivi upo field ya Journalists. Kwa hiyo na wewe unayo taaluma ya uhandishi wa habari. Watu wanakuamini hadi unakuwa Media Consultant na Mtangazaji wa kulipwa hakika si jambo rahisi. Unakuwa hadi Political Advisor bila kuwa na BSc in Political Science hakika mtaalamu wa siasa na uhandishi wa habari ingawa hujasomea.

Sasa bahasha zinaharibu vipi taaluma, nakujibu kama ifuatavyo. Umesema "ulipoikuwa mwandishi tuu wa habari, bahasha umezipokea sana, na sasa kama mshauri wa habari, hizo bahasha wewe ndiye unazigawa with clear and honest conscious kuwa bahasha za uwezeshaji is the right thing na ni haki za msingi za waandishi kuwezeshwa ili waweze kutimiza majukumu yao ya kila siku".

Sasa sisi tunapozungumzia bahasha hatuzungumzii hizo ambazo ni za uwezeshaji kwa ajili ya kukusanya na kuandika habara. After all hizo haziitwi bahasha. Hizo ni Allowance za kawaida tu. Bahasha tunazozungumzia ni zile mnazopewa kwa ajili ya kutunga habari ili kutimiza malengo ya mtu au kikundi flani. Sasa hivi unasema wewe ni mshauri wa habari na hizo bahasha wewe ndiye unazigawa. Kwa hizi namaanisha zile unazozigawa kwa maofisa wa Taasisi za Serikali na mashirika ili upatiwe matangazo nk.

TUMBIRI (PhD, Hull University - HULL City, UK),

tumbiri@jamiiforums.com
 
Kwa hiyo ukitaka kuuwa nyoka una unapiga risasi kwenye mwili wake au mkia sio?

Ndo hapo sasa mkuu, huyu jamaa anataka kuharibu mchuzi kwa kujifanya mchambuzi makini, ila anatakiwa akumbuke pia kuchamba kwingi ni kuondoka na kinyesi. TATIZO NI CCM, huwezi kumlaumu mwananchi wa kawaida kule kijijini ambaye kanyimwa hata elimu ya kung'amua mambo. CCM NDO IMEWANYIMA WATANZANIA ELIMU BORA, MATOKEO YAKE UWEZO WA WATANZANIA WENGI KUNG'AMUA MAMNBO HASA VIJIJINI NI MDOGO, MPAKA WANASHAWASHIWA KWA CHUMVI ILI WAMPIGIE MTU KURA. usiwalaumu watanzania, ulemavu walio nao wamelazimishwa makusudi na hili li-ccm. SHULE HAZINA WALIMU BORA, WALIOPO WENYEWE HAWALIPWI STAHIKI ZAO MUDA MUAFAKA, UNATEGEMEA NINI MKUU??? NARUDIA TENA MARA 100 ZAIDI, TATIZO LA TANZANIA NI CCM, MCHAWI WETU TANZANIA NI CCM.
 
Pasco,
Bahasha tunazozungumzia ni zile mnazopewa kwa ajili ya kutunga habari ili kutimiza malengo ya mtu au kikundi flani. Sasa hivi unasema wewe ni mshauri wa habari na hizo bahasha wewe ndiye unazigawa. Kwa hizi namaanisha zile unazozigawa kwa maofisa wa Taasisi za Serikali na mashirika ili upatiwe matangazo nk.

TUMBIRI (PhD, Hull University - HULL City, UK),

tumbiri@jamiiforums.com

Mkuu Tumbiri, kama unaamini hii ni habari ya kutunga, na mimi nimeshikishwa ili kuisambaza hii habari kwa malengo fulani, endelea kuamini hivyo! ila bahasha ninazozigawa mimi ni zile genuine za uwezeshaji waandishi kutimiza wajibu na majukumu yao!.

Hili la bahasha hapa limetosha, tuendelee na mada!.
 
Wanabodi,



Kutokana na kauli hiyo, nimekuwa inspired kuandika kidogo kuhusu adui mkuu wa Tanzania wengi wakidhani ni CCM, kumbe sio, bali adui mkuu wa Watanzania ni ... kwa maoni yangu,

1. Tatizo kubwa .... ni sisi Watanzania tulioiweka CCM madarakani and it plays games on us again and again na sisi
tukiendelea kuiweka madarakani again and again na sitashangaa kama hata 2015, tukairudisha tena!.

Pasco.

NB. Pasco wa jf, sio mwanachama, mfuasi wala mshabiki wa chama chochote cha siasa, bali ni Mtanzania wa
kawaida mwenye kuweka mbele maslahi ya taifa.

Mkuu Pasco

Kama unakumbuka, Mwenyekiti mpya wa Tume ya Uchaguzi ameeleza wazi tatizo ni nini...kuwa Tume inafuata matwaka ya Chama dola.

CCM haichaguliwi na wananchi,,inajichagua na inajitangaza mshindi. Hili hakuna asiyelijua.

Unajua maana ya kuiba kura? Kuchakachua matokeo?

Haya maelezo mengine ni kuzunguka m-buyu tu. Tanzania hakuna uchaguzi huru na wa haki.

Siku itapatikana Tume huru ya Uchaguzi, Uchaguzi ukawa huru na wa haki, Mshindi anatangazwa mshindi ndio tatizo moja litaondoka(usanii) tutaanza kushughulikia matatizo mengine.

Maelezo juu ya CUF ni mazuri ,pia umetaja walikubali yaishe. Walikubali yaishe maana yake ni nini?

Ukifafanua hili,utakuwa umetaja adui adui mkubwa bila kumung'unya maneno.

Adui mkubwa is an open secret, anajulikana, mkuu Pasco!!!
 
Ndo hapo sasa mkuu, huyu jamaa anataka kuharibu mchuzi kwa kujifanya mchambuzi makini, ila anatakiwa akumbuke pia kuchamba kwingi ni kuondoka na kinyesi. TATIZO NI CCM, huwezi kumlaumu mwananchi wa kawaida kule kijijini ambaye kanyimwa hata elimu ya kung'amua mambo. CCM NDO IMEWANYIMA WATANZANIA ELIMU BORA, MATOKEO YAKE UWEZO WA WATANZANIA WENGI KUNG'AMUA MAMNBO HASA VIJIJINI NI MDOGO, MPAKA WANASHAWASHIWA KWA CHUMVI ILI WAMPIGIE MTU KURA. usiwalaumu watanzania, ulemavu walio nao wamelazimishwa makusudi na hili li-ccm. SHULE HAZINA WALIMU BORA, WALIOPO WENYEWE HAWALIPWI STAHIKI ZAO MUDA MUAFAKA, UNATEGEMEA NINI MKUU??? NARUDIA TENA MARA 100 ZAIDI, TATIZO LA TANZANIA NI CCM, MCHAWI WETU TANZANIA NI CCM.
Kama umeshang'amua wananchi ndio wamerubiniwa na CCM ili kuichagua, then ili kuiondoa hiyo CCM iliyowarubuni ni kuwafikia hao wananchi na kuwaelkimisha ili wasiendelee kurubuniwa!. Wewe jiulize anayepiga kura kuchagua ni nani?, CCM si ni inachaguliwa?!, unatakiwa kumfuata mchaguaji na sio mchaguliwa!, ukiendelea kumtarget mchaguliwa tuu, mchaguaji ataendelea kumchagua huyo huyo mchaguliwa aliyemzoea, ukimtarget mchaguaji na kumuelimisha asiendelee kuchagua kwa mazoea bali kwa sababu, then, mchaguliwaji wa mazoea, hata chaguliwa tena na atajifia natural death!.
 
PASCO,
Hakuna cha kujiuliza sana tatizo kubwa Tanzania ni CCM ikiwa imeshikilia Uongozi wa Serikali ya JMT chini ya Katiba ya Chama chenyewe. Kumbuka hatuongozwi au kufuata Katiba ya Tanzania na wala haipo. Bali tunafuata itikadi ya CCM iliyobatizwa na kuitwa Katiba ya Tanzania. Ndiyo maana kila kiongozi nchini anachaguliwa na Mwenyekiti wa CCM na ni lazima awajibike kwake na siyo kwa wananchi.
 
You are a bush-league law graduate. If you were licensed to practice law I wouldn't advise anyone to come to you.
Mkuu Bwa'Nchuchu, hii umeihamishia humu?!, hii ilistahili kule "chit chat", ila kwa vile umeileta humu, nitakujibu tuu kwa sasa na kukuomba ukishasoma hili jibu, jirudie zako kule "chit chat"!.

Kwa uhaba wa ma advocates uliopo nchini, nikiamua ku register as an advocate, belive me, sitahitaji recomendation yako kupata wateja kwa sababu nitaregiter ili kutoa huduma za kisheria bure kwa wasio na uwezo, media consultancy zangu na production company yangu inatosha kabisa kunisustain to my grave, nita register to help the helpless not to make it!.
 
Mkuu Bwa'Nchuchu, hii umeihamishia humu?!, hii ilistahili kule "chit chat", ila kwa vile umeileta humu, nitakujibu tuu kwa sasa na kukuomba ukishasoma hili jibu, jirudie zako kule "chit chat"!.

Kwa uhaba wa ma advocates uliopo nchini, nikiamua ku register as an advocate, belive me, sitahitaji recomendation yako kupata wateja kwa sababu nitaregiter ili kutoa huduma za kisheria bure kwa wasio na uwezo, media consultancy zangu na production company yangu inatosha kabisa kunisustain to my grave, nita register to help the helpless not to make it!.

Rudi shule ukajifunze tahajia.
 
PASCO,
Hakuna cha kujiuliza sana tatizo kubwa Tanzania ni CCM ikiwa imeshikilia Uongozi wa Serikali ya JMT chini ya Katiba ya Chama chenyewe. Kumbuka hatuongozwi au kufuata Katiba ya Tanzania na wala haipo. Bali tunafuata itikadi ya CCM iliyobatizwa na kuitwa Katiba ya Tanzania. Ndiyo maana kila kiongozi nchini anachaguliwa na Mwenyekiti wa CCM na ni lazima awajibike kwake na siyo kwa wananchi.
Mkuu MpendaTZ, nina swali dogo tuu kwako, anayeichagua CCM kupitia ballot box ni nani?, kama CCM inajichagua na kuprint zile kura, then hao members wa opposition waliomo bungeni, wasingekuwemo!.

Ukienda website ya CCM, wanajitapa wao wana wanachama milioni 6 nchini kote!. Watanzania tuko milioni 40!. Kati ya hawa milioni 40, watu milioni 26, wanauwezo wa kupiga kura!. Uchaguzi wa 2010, JK amechaguliwa kwa kura milioni 6 plus!, lets assume waliomchagua JK ndio hao wana CCM milioni 6!. Ili upinzani ushinde 2015, upinzani uachane kabisa kujishughulisha na hawa milioni 6 walioichagua CCM, ujikite kuwamobilize hawa milioni 20 ambao hawakupiga kura kwa sababu moja au nyingine!.
 
Du Bwanchu unanitesa!, ngoja kwanza nitafute kamusi ya Kisuaheal ili kulitafasiri hili neno halafu nitakurudia!.

Teh teh teh....sasa unakosea kwa makusudi. Ulidhani sitagundua? Nimeshakuambia wewe ukubwa umri tu. Akili yako bado ya kitoto sana.
 
1. Tatizo kubwa la Watanzania sio au adui mkubwa wa Tanzania sio CCM, CCM is just the vehicle, haikujiweka
hapo ilipo, imewekwa, hivyo tatizo sio CCM iliyowekwa, bali tatizo ni walioiweka CCM hapo ilipo!. That simply
means, tatizo ni sisi Watanzania tulioiweka CCM madarakani and it plays games on us again and again na sisi
tukiendelea kuiweka madarakani again and again na sitashangaa kama hata 2015, tukairudisha tena!.

Wananchi hasa wa vijijini wameachwa katika ujiinga unochangia katika kudumisha umaskini mkubwa wa hali na mali. Zingatia uduni wa elimu na uwezo mdogo wa ku "analyze" issues. CCM imedhoofisha suala la elimu systematically ikijua wazi kuwa taifa lenye watu walioelimika wataipa upinzani mkubwa na kwa hili imefanikiwa sana. Usishangae 2015 CCM ikarudi kwani CCM imerekebisha hiyo hali? Kumbuka sakata la walimu we acha tu.

 
Wanabodi,

6. Kwa sasa, angalau Chadema, kupitia M4C, imeshagundua adui halisi anayewakosesha ushindi, na sasa
imejielekeza kwa wananchi ambao ndio wenye maamuzi ya mwisho na wamekuwa wakiichagua CCM
kwa mazoea tuu, hivyo concetration ikiwekwa kwenye "changing mindset ya wenye maamuzi, kuacha kuchagua
kwa mazoea tuu, bali kuchagua kwa sababu. Wananchi, watafunguka macho, na hawatakuwa na sababu tena
ya kuendelea kuichagua CCM!.

7. Mara baada ya uchaguzi wa 2010 na mafanikio makubwa upande wa Chadema, kwenye ile mada yangu ya
"CCM Imechokwa, Chadema Haijajipanga", niliwaeleza kuwa wapinzani bado hawajipanga mkao wa kushika
dola, lakini kwa kwa sasa kupitia M4C, Chadema wanaonyesha dalili za kujipanga japo bado wanakabiliwa na
madhaifu haya na yale, yakiwemo, lile koti la ukanda, udini, ukabila na ubinafsi wa "umimi" etc.

8. Kwa leo naomba nisiingie tena kwenye udini, ukanda na ukabila wa Chadema, bali naomba nijikite kwenye
ubinafsi au "umimi" kwa Chadema kujiamini kupita kiasi kuwa peke yao wataweza!, nilisema peke yao
hawawezi, na leo nasema te na na tena, "Chadema peke yanu hamuwezi Kuiondoa CCM Madarakani" kwa
sababu hili CCM ni dubwana kubwa sana ambalo haliwezi kung'oka bila umoja ambao ni nguvu ya Watanzania
wote wenye kuliutakia mema taifa hili.


10. Chadema na wapinzani wengine wote wa ukweli, ni lazima wa join forces kutafuta the common working
grounds na wenzenu wengine wote mu work together towards a common enemy hata na nyinyi wenyewe kwa
wenyewe lazima mkubali kushirikiana kwa kukubali kutokubaliana kwa hayo madogo madogo lakini lazima
mkubaliane kwenye kubwa la msingi kwa kukubali "umoja ni nguvu" vinginevyo matokeo ya 2015 yatakuwa ni
yale yale ya, vyama vile vile, na watu wale wale!.


12. Hakuna ubishi kuhusu nguvu ya CUF kule Zanzibar na Chadema itake isitake, ipende isipende, ili kujihakikishia
njia nyeupe ya kuwa mpangaji wa magogoni kwa 2015, ni lazima ikubali kuisupport ya CUF kwa upande
Zanzibar ili CUF nao wakubali kuisupport Chadema huku bara!. Chadema wakae chini na CUF, waainishe
maeneo ya strong holds za kila mmoja na kuachiana maeneo hayo ili 2015, kuepuka kumfaidisha kunguru
kwa vita vya panzi!.

Wasalaam.

Pasco.
Haya mawazo niliwahi kuyapigia kelele 2010..kama CHADEMA wanapenda kusikia wanayotaka kuyasikia tu, itakula kwao.

1. https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-unapopinzana-unapohujumiana.html#post1322769

2. https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-unapopinzana-unapohujumiana.html#post1324549
 
Ukilijua tatizo utakuwa umelisove kwa 50% Usipolitambua ni kinyume chake.Katika hili nakubaliana na Pascal kuwa mwananchi ni sehemu kubwa ya Tatizo usitetee sana akili ya kujua mema na Mabaya wote tunayo!kinachofuata ni uzembe wa kufikiri tu na ubinafsi,kumbukaa hasa Wadanganyika tuna taizo hili ,Hatupigi kura, hatutafakari na tukipiga tuna sababu za kijinga kama:
  1. Kura moja itasaidia nini hata nisipopiga haitabadili kitu.
  2. Prof.Lipumba /Dr.Slaa ,...... anafaa ila hatashinda nikimpigia kura tutashindwa wote!
  3. CCM ni baba na Mama
  4. Wamunzengo kanipa Chumvi si vizuri nikamnyima kura etc
  5. watu wenyewe wanakufa au kufiwa kwa kukosa huduma hospitali ,kufelisha watoto shule za kata nk. wanajua, wanahukumiwa isivyo polisi mahakamani hata na mtendaji wa kitongoji balozi lakini bado wana mchagua.
  6. Yeyote utakaye mchagua lazima ale bora waendelee hawa walioshiba etc
  7. Hatuko serious kwenye mambo ya msingi kama uchaguzi ,katiba nk, fuatilia mchakato wa katiba hapana sitaenda nitakuwa kwenye kikundi ,saccos nk,katiba yamalizeni tu kama hawajui mbona hawaulizi?
Ndiyo maana nyerere alisema ili tuendelee tunahitaji mambo manae watu ,ardhi ,siasa ,sasi na Uongozi .
alianza na watu wewe unataka tuanzie namba 3 na nne tua hatua ya kwanza inaanzia ulipo (watu) zingine zinafuata. Ndiyo maana mimi huwa na pinga sana unachotaka kusema watu ni wazuri viongozi wabaya unasahau viongozi ni sehemu wakati mwingine Cream ya jamii to me Kama viongozi ni wabovu Jamii pia mbovu pengine zaidi! Humuwezi kuwa Wasafi mkaongozwa na wabovu kila wakati!
Mimi nimeshuhidi chaguzi hadi UDSM kama huku tu street nao hawana elimu? je Mkoa wa Mara ,Bariadi ,Pemba , Mwibara ,Bunda ,Msoma Vijini na Mjini,Tarime wamesoma kuliko Dar, Kagera,Mbeya!?
TATIZO NI CCM, huwezi kumlaumu mwananchi wa kawaida kule kijijini ambaye kanyimwa hata elimu ya kung'amua mambo. CCM NDO IMEWANYIMA WATANZANIA ELIMU BORA, MATOKEO YAKE UWEZO WA WATANZANIA WENGI KUNG'AMUA MAMNBO HASA VIJIJINI NI MDOGO, MPAKA WANASHAWASHIWA KWA CHUMVI ILI WAMPIGIE MTU KURA. usiwalaumu watanzania, ulemavu walio nao wamelazimishwa makusudi na hili li-ccm. SHULE HAZINA WALIMU BORA, WALIOPO WENYEWE HAWALIPWI STAHIKI ZAO MUDA MUAFAKA, UNATEGEMEA NINI MKUU???
 
Back
Top Bottom