Kudharauliana katika Imani (Imani za Kishirikina)

Mzalendo39

JF-Expert Member
Apr 17, 2015
882
1,029
Watanzania wengi wanasahau walipotokea na kuziita Imani zao za kale kuwa za kishirikina. Katika historia Dini tunazoabudu hivi sasa zilikuja kwa meli (Wazungu) na kabla ya hapo tulikuwa na imani zetu zilizotuongoza kabla ya Wazungu na Waarabu.

Imani zetu hazina tofauti na lugha zetu za asili pamoja na kiswahili ambacho hivi sasa kinazidi kudumazwa na lugha za kigeni (Kingereza) kupewa chapuo hadi kufundishia mashuleni.

Kwa sasa imani zetu Watanzania na asili zetu zimeendeleatupiliwa Mbali hadi kufikia kuitwa Imani za kishirikina. Ni vyema serikali ikatoa uhuru kwa imani zote tulizonazo kama wanavyopigia chapuo Imani za wazungu na Waarabu.

Mimi nimezaliwa bila dini yoyote ya Wazungu nitaendelea kuwa na imani nilizozikuta toka kwa babu zangu.
 
Unapobatizwa na kupewa jina la kizungu unashangilia kama zuzu na kudharau jina lako la asili.
 
Nchi imeharibika bora jeshi wachukue madaraka tu.
Nchi hiko vizuri Sana chini ya Samia, fanya kazi mkuu,acha kukaa kwa shemeji,



Magufuli hayupo sasaivi biashara zipo Safi hakuna bugdha Tena, na kwa wafanyakazi maslai yameongezwa maradufu
 
إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا وَمَاتُوا وَهُمْ كُفَّارٌ أُولَٰئِكَ عَلَيْهِمْ لَعْنَةُ اللَّهِ وَالْمَلَائِكَةِ وَالنَّاسِ أَجْمَعِينَ


Hakika walio kufuru na wakafa hali ni makafiri, hao iko juu yao laana ya Mwenyezi Mungu na ya Malaika na ya watu wote.


خَالِدِينَ فِيهَا ۖ لَا يُخَفَّفُ عَنْهُمُ الْعَذَابُ وَلَا هُمْ يُنْظَرُونَ

Watadumu humo. Hawata-punguziwa adhabu wala hawatapewa muda wa kupumzika.


وَإِلَٰهُكُمْ إِلَٰهٌ وَاحِدٌ ۖ لَا إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ الرَّحْمَٰنُ الرَّحِيمُ

Na Mungu wenu ni Mungu mmoja tu, hapana mungu ila Yeye. Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu.


إِلَّا الَّذِينَ تَابُوا وَأَصْلَحُوا وَبَيَّنُوا فَأُولَٰئِكَ أَتُوبُ عَلَيْهِمْ ۚ وَأَنَا التَّوَّابُ الرَّحِيمُ

Ila wale walio tubu na wakatengeneza na wakabainisha, basi hao nitapokea toba yao, na Mimi ni Mwenye kupokea toba na Mwenye kurehemu.


وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ اتَّبِعُوا مَا أَنْزَلَ اللَّهُ قَالُوا بَلْ نَتَّبِعُ مَا أَلْفَيْنَا عَلَيْهِ آبَاءَنَا ۗ أَوَلَوْ كَانَ آبَاؤُهُمْ لَا يَعْقِلُونَ شَيْئًا وَلَا يَهْتَدُونَ

Na wanapo ambiwa: Fuateni aliyo yateremsha Mwenyezi Mungu; wao husema: Bali tutafuata tuliyo wakuta nayo baba zetu. Je, hata ikiwa baba zao walikuwa hawaelewi kitu, wala hawakuongoka?


وَمَثَلُ الَّذِينَ كَفَرُوا كَمَثَلِ الَّذِي يَنْعِقُ بِمَا لَا يَسْمَعُ إِلَّا دُعَاءً وَنِدَاءً ۚ صُمٌّ بُكْمٌ عُمْيٌ فَهُمْ لَا يَعْقِلُونَ

Na mfano wa walio kufuru ni kama mfano wa anaye mpigia kelele asiye sikia ila wito na sauti tu -- ni viziwi, mabubu, vipofu, kwa hivyo hawaelewi.
 
Nyie ndo wachawi mliojazana huko vijijini hadi watu hawatamani kurudi makwao, kadanganye wajinga....eti imani za kale.
 
Back
Top Bottom