Kwa mawazo yangu kamati kupoteza muda kuchunguza mali za viongozi ni ****** wa hali ya juu. Kama kiongozi amepata pesa kinyemela anaweza kuweka mali kwenye jina la mtu yeyote au hata kuweka pesa kwenye account za nje kama watuhumiwa wa rada. Hii ya kuchunguza viongozi eti wana mashamba mangapi, viwanja vingapi na nyumba ni fikra za kimaskini. Kiongozi kutokuwa na nyumba haina maana ni kiongozi mzuri inawezekana ni kiongozi mvivu. Tanzania badala ya kuweka sheria tumekuwa nchi ya kinafiki na kudanganyana sana. Kuna matatizo mengi sana Tanzania na hii kamati yenyewe ya uchunguzi ni tatizo.