Kuchelewa Kutoa Shule na Vyuo Wanafunzi Waliofaulu Kidato cha Nne Walizopangiwa.

Zakaria Lang'o

JF-Expert Member
Apr 2, 2012
2,593
2,767
Nionavyo hili limekuwa tatizo kwa Wizara inayohusika. Wanachelewa kutoa majina ya Shule na Vyuo wanakowapeleka wanafunzi wa Kidato cha Nne. Kuchelewa huku husababisha adha kubwa kwa wanafunzi na wazazi hasa inapotokea watoto wao wamepelekwa katika shule au Vyuo vya mbali ukizingatia gharama za nauli, ada na matumizi.
Chukulia mfano wa Mwanafunzi anayetoka Kyaka kule Kagera, mpakani mwa Uganda na kupelekwa Mtwara, kusini, mpakani mwa Msumbiji, atahitaji gharama kubwa sana.
Kwa hali hiyo Wahusika wa Wizara wanaposubiri Hadi wiki za mwisho za mwezi wa sita ndipo watangaze shule na Vyuo, inakuwa si sawa. Ikumbukwe kuwa matokeo ya wanafunzi hawa yalitoka mwezi wa tatu, hivyo sioni sababu za msingi za uchelewevu huu wa makusudi.
Mhe. Waziri najua anapita humu, ni wajibu wake kuwahimiza wapanga shule na Vyuo watangaze mapema ili wazazi watayarishe gharama zinazotakiwa. Kujifungia Dar es Salaam na kufikiri wanafunzi wote watatoka Mbagala na kwenda Mikocheni si sahihi hata kidogo.
 
Wanafunzi mnaoingia humu, pazeni sauti zenu ili hawa watu wanaokula na kusaza wajue Kuna maandalizi ya kufanya hasa wakati huu wa uchumi mgumu. Tokeni huko FB, tafadhalini sana.
 
Nikweliii kabsaa uuandaji na upangaji wa post ní mbovu hvyo yawapasa serikal kubadil mfumo wakoo has a wazir usika ulionee hilii kama kelo kwa wananchi
 
Kuna mambo mengi yanafuata baada ya matokeo kutoka kama vile waliokata rufaa n.k. kwahivyo unaweza ukaona ni muda mwingi wanao lakini kwao ni muda mchache na mambo ni mengi ya kukamilisha ndani ya huu muda.
 
Kuna mambo mengi yanafuata baada ya matokeo kutoka kama vile waliokata rufaa n.k. kwahivyo unaweza ukaona ni muda mwingi wanao lakini kwao ni muda mchache na mambo ni mengi ya kukamilisha ndani ya huu muda.
Acheni scapegoat zisizo kichwa. Kutotoa nafasi hizi mapema ni tatizo kubwa. Hebu zisitafutwe sababu za uchelewevu. Uchumi ni mgumu kiasi kwamba mkulima wa kawaida kupata TZS300,000/- Ni issue kubwa kama si kuuza maksai wa kulimia Ni kukata kipande Cha ardhi ili kupata pesa hiyo!!! Halafu mnaleta hoja mfu za "wakata rufaa."
 
Acheni scapegoat zisizo kichwa. Kutotoa nafasi hizi mapema ni tatizo kubwa. Hebu zisitafutwe sababu za uchelewevu. Uchumi ni mgumu kiasi kwamba mkulima wa kawaida kupata TZS300,000/- Ni issue kubwa kama si kuuza maksai wa kulimia Ni kukata kipande Cha ardhi ili kupata pesa hiyo!!! Halafu mnaleta hoja mfu za "wakata rufaa."


Wakata rufaa nimesema ni mojawapo ya vitu vingi wanavyofanya kabla ya posts na sio hoja kuu. Unadhani wahitimu wa mwaka jana ndio wa kwanza kuhitimu Tanzania?. Mbona wengine walisubiri na wanaendelea vizuri tu.
 
Wakata rufaa nimesema ni mojawapo ya vitu vingi wanavyofanya kabla ya posts na sio hoja kuu. Unadhani wahitimu wa mwaka jana ndio wa kwanza kuhitimu Tanzania?. Mbona wengine walisubiri na wanaendelea vizuri tu.
Rafiki huelewi na inaonekana hujaisoma post hii ukaelewa hoja ya msingi. Nirudie tena kwamba watendaji tunapofanya mambo yanayohusu jamii yetu, ni lazima tuifahamu kiundani jamii hiyo hasa upande wa vipato vya kiuchumi. Unatoa nafasi kwa kijana wa mkulima maskini (peasant) kutoka Sirari mpakani mwa Kenya, kwenda Mtwara mpakani mwa Msumbiji, na unamtaka mzazi wake atayarishe gharama zote zaidi ya TZS300,000/- kwa mkupuo ndani ya wiki moja au mbili. Huku Ni kumhujumu huyu kijana asifike shule au chuo kwa kukosa gharama.
Hayo ya kufanya mambo kwa mazoea ya mwaka jana au juzi ni upuuzi usiokubalika.
 
Back
Top Bottom