Kuche au kukuche?

Bandu Ncheche

JF-Expert Member
Jul 9, 2016
512
324
Kukicha au kukikucha?
Haya maneno yamekuwa yakitumika mara nyingi sana ila sijui lipi ni sahihi na lipi sio sahihi.
1:Kukicha tu naanza safari.
2:Kukikucha tu '''''''''''’'"'''''’'''''’''
3:Nasubiri kuche ndipo nianze safari.
4:"'’'''''''''''''''''''kukuche"""""""'"'''''’''"""'''
 
Nimeamini Kiswahili ni lugha ngumu kuliko Kiingereza watu 96 wameangalia tu ila hawana majibu.
 
Mkuu lugha ni sauti za watu hivyo watu ndio wanaamua kipi ni sahihi na sio sahihi na sio wataalamu wa lugha ndo mana kile kinachoitwa ugali bongo Kenya ni sima na Rwanda ni sembe ...hivyo yote hapo ni sahihi kwa sababu mosi hutumiwa na watu wa lugha hiyo pili hakuna kanuni ya kiisimu inayopinga utokeaji wa mitindo mbalimbali ya kitenz hicho
Sawa mkuu lakini bado sijajibiwa
 
Mkuu lugha ni sauti za watu hivyo watu ndio wanaamua kipi ni sahihi na sio sahihi na sio wataalamu wa lugha ndo mana kile kinachoitwa ugali bongo Kenya ni sima na Rwanda ni sembe ...hivyo yote hapo ni sahihi kwa sababu mosi hutumiwa na watu wa lugha hiyo pili hakuna kanuni ya kiisimu inayopinga utokeaji wa mitindo mbalimbali ya kitenz hicho
Sawa mkuu kwa mfano huo wa ugali,hata muhogo ni chinangwa lakini sio kwa kiswahili.
 
Sawa mkuu kwa mfano huo wa ugali,hata muhogo ni chinangwa lakini sio kwa kiswahili.
Chinangwa ushasema sio kiswahili tofauti na mifano yangu sima ni kiswahili kinachozungumzwa Kenya na hii sifa ya lugha kuwa na lahaja (utofauti wa kimatumizi) upo katika lugha nyingi ndio mana kwenye british English wanasema Traveller lakini kwa US English ni Traveler
 
Chinangwa ushasema sio kiswahili tofauti na mifano yangu sima ni kiswahili kinachozungumzwa Kenya na hii sifa ya lugha kuwa na lahaja (utofauti wa kimatumizi) upo katika lugha nyingi ndio mana kwenye british English wanasema Traveller lakini kwa US English ni Traveler
Sima kwa Kichewa ni nsima maana yake ni ileile ugali,na wengine wanaita xima(shima)=ugali,kwahiyo ukisema sima ni kiswahili basi na nsima ni kiswahili na sio Kichewa tena.
 
Sima kwa Kichewa ni nsima maana yake ni ileile ugali,na wengine wanaita xima(shima)=ugali,kwahiyo ukisema sima ni kiswahili basi na nsima ni kiswahili na sio Kichewa tena.
Mkuu neno kuwa kwenye lugha mbili inawezekana hivyo sima kuwa kiswahili hakuondoi neno hilo kuwa la kichewa mbona hata bunge ni neno la kigogo lakini pia ni la kiswahili ....kumbuka kiswahili kimechukua maneno mengi ya lugha nyingine za kibantu ...hivyo maneno hayo yanatumika kwa kiswahili na hata hizo lugha nyingine
 
Mkuu neno kuwa kwenye lugha mbili inawezekana hivyo sima kuwa kiswahili hakuondoi neno hilo kuwa la kichewa mbona hata bunge ni neno la kigogo lakini pia ni la kiswahili ....kumbuka kiswahili kimechukua maneno mengi ya lugha nyingine za kibantu ...hivyo maneno hayo yanatumika kwa kiswahili na hata hizo lugha nyingine
Hoo ndio maana Bunge linaongezwa na Mgogo.
Na Ikulu ni Kisukuma ndio maana yupo Msukuma
 
Hoo ndio maana Bunge linaongezwa na Mgogo.
Na Ikulu ni Kisukuma ndio maana yupo Msukuma
Bunge mbona limeomgozwa na makinda wa iringa huko hata spika wa kwanza wa bunge alikuwa mhehe hakuna uhusiano wa ugogo na kuongoza bunge bali lugha ya kigogo na neno bunge
 
Back
Top Bottom