#COVID19 Kuchanja sasa kuwe lazima, hasa wafanyakazi serikalini. Chanja au achia ngazi

Tunafahamishwa kitaalamu kwamba MTU akichanjwa hata kama ataambukizwa covid madhara yake hayatakuwa makubwa kama yule MTU ambaye hajachanjwa,
Asante mkuu.
Hilo somo kuna watu hawataki kulisikia maana mioyo yso imejazwa sumu na akina Gwajima.
Matokeo yake watu wanakufa kimya kimya baada ya kuikana chanjo.
Tuwashauri waende mortuary Muhimbili wajionee wenyewe.
 
Tunafahamishwa kitaalamu kwamba MTU akichanjwa hata kama ataambukizwa covid madhara yake hayatakuwa makubwa kama yule MTU ambaye hajachanjwa,
Umeishafahamu ufafanuzi wa kitaalamu wa nini ufanye kabla ya kuchanjwa?
Na je,nini kinatokea endapo utachanjewa huku mwilini tayari una virusi vya corona?
Na nikitaka nipime kabla ya kuchanjwa ili nisiongeze kirusi juu ya virusi,kupima nako ni bure au laki mbili na therathini inanihusu na baadaye niende kupata chanjo ya bure?
 
Watu wengi ambao hawataki kuchanja wanaamini kwamba ule muda ulioelezwa kwenye maandiko kuhusu namba 666 umeshawadia, Hahahaha !! Saa nyingine unaona hii dunia inayo mambo ya ajabu sana,
Mkuu kuna watu wanashauriwa kuchanja, tena kwa faida yao na familia zao, utafikiri wanashauriwa kutahiri!
Si matusi hayo!
 
Umeishafahamu ufafanuzi wa kitaalamu wa nini ufanye kabla ya kuchanjwa?
Na je,nini kinatokea endapo utachanjewa huku mwilini tayari una virusi vya corona?
Na nikitaka nipime kabla ya kuchanjwa ili nisiongeze kirusi juu ya virusi,kupima nako ni bure au laki mbili na therathini inanihusu na baadaye niende kupata chanjo ya bure?
Mimi nimechanjwa na niliulizwa una homa? Nikajibu sina homa, nikaulizwa tena ulishaugua covid ? Nikajibu sijui kama niliugua au sikuugua maana sikuwahi kupimwa covid, wakaniuliza una aleji ya kitu chochote nikawajibu sina aleji yeyote, basi nikachanjwa, na baada ya hapo nikawauliza jamaa zangu waliopo huko ulaya je nyinyi huko mlipo huwa mnaulizwa nini kabla ya kuchanjwa ? Wakaniambia maswali ni kama hayo niliyoulizwa mimi huku Tz, pia huwa wanauliza unayo magonjwa gani yale sio ya kuambukizwa ? Yaani kama moyo kisukari shinikizo na mengineyo, baada ya hapo unachanjwa biashara imeisha,
 
Huko huko ilikotoka chanjo barakoa nikama kawaida imeshajumuishwa kwenye mavazi ya mwanadamu, wewe kusanya familia yako mkachanje
 
Pia kuna waliochanjwa wengi wana hofu hawajui nini kitawapata hapo baadae,wanataka kushinikiza wote wachanjwe ili kama kuna madhara yasiwapate peke yao,hii ni roho mbaya na ya kichawi.
Ikumbukwe hii chanjo siyo ya kwanza zipo zizilizotangulia, Kwenye zilizotangulia,ukishampa taarifa jirani yako basi
unaendelea na maisha suala la ataenda kuchanjwa au la hatufuatilii,jiulize hii mbona wakishachanjwa wanataka na wewe uende hata kama ni kwa lazima?
wanataka iwe msiba wa wengi ni harusi? Wameze tu halafu na round ya pili wanatakiwa kuchoma lini?
 
Vita ya waliochanja na wasiochanja inaanza ila kuna kundi moja linajiamini msiniulize ni kundi gani.
Jiulize kwa nini mataifa ya nje yanaisemea vizuri Tz wakati waliochanja ni chini ya laki 4 kati ya milioni 60. Neno LAZIMA halifai kwenye huu uzi labda ile fomu ifutwe sentensi ya kwamba Serikali haitahusika na madhara yatakayojitokeza hapo baadae. Ukisema iwe lazima ni sawa na kulazimisha watu wavute sigara wakati imeandikwa uvutaji wa sigara ni hatari kwa afya yako ila kuvuta ni hiari.
Kwani wakichanja wana pewa cheti? Form si inabaki huko huko
 
Sasa inabidi Serikali ichukue uamuzi mgumu juu ya chanjo.

Wafanyakazi Serikalini lazima wachanje, au waachie ngazi kutazama afya zao.

Tutavaa barakoa hadi lini?

Tatizo kubwa ni hao wa Gwajima, wasiotaka kuchanja na ndio kwa kiasi kikubwa wanaeneza Covid katika jamii.

Ni jambo la kusikitisha vifo vya hivi karibuni familia ya Hanspoppe, kuna waliokataa kuchanja, mauti imewatembelea.

Imefika muda tusicheze na hili janga.
Unaandika maada ukiwa umepakatwa na beberu unalikatikia bila kilainisho kweli mapenzi upofu endelea kula koni kama mama J
 
Unaandika maada ukiwa umepakatwa na beberu unalikatikia bila kilainisho kweli mapenzi upofu endelea kula koni kama mama J
Mkuu kama ulikuzwa hivyo na babaako ujue JF kuna wastaarabu.
Na kwa muonekano tu, unanuka kama kinyesi mtu alichokanyaga barabarani na kimeshikilia soli ya kiatu.
 
nimekueleza kwa watu wenye akili huwa wanawaza.

hawa watu walikuwa wanaishi na familia zao, eti ugonjwa ukaingia ukapukutisha watu muhimu tu lakini siyo familia zao walizokuwa wakiishi nazo. huoni hapo kuna jambo la kuawa wewe?

tu fikirie kuna mtu mmoja alipata ugonjwa, alafu akawaambukiza wengine wa ofisini tu lakini majumbani kwao hawakuambukizwa.

kwa mwenye fikra atajiuliza mambo mengi, acheni kukalili nyie ngozi nyeusi
Tena wanyumbani mwingine anajifunika naye shuka moja na yupo maajabu hayo! Corona inafuatilia wale mnaoshinda pamoja mchana , lakini si mnaolala nao pamoja
 
Jidu La Mabambasi
white wizard

Why covid mnaichukulia as movie trailer?.

Yaani watanzania tuna mambo ya ajabu sana, ni afadhali yule mzee alikuwa na msimamo thabiti juu ya hii kitu ila leo mnasisitiza ugonjwa upo ila mnacheza nao movie!.
Mkuu ngoja ufiwe na mtu au jamaa wa karibu, uone mateso anayopitia na huna la kufanya hata kama una pesa.
Hapo ndio utajua trailer hili si la kupuuza.
 
Kweli hii Nchi inayo watu wa ajabu sana, yaani hata hichi kifo cha Zakaria Hans pope bado unataka kubisha kuwa hakuugua Covid ? Yeye mwenyewe ametangazia watu akiwa amelazwa Aghakhan Hospital kwamba anaugua covid na kwamba huu ugonjwa unatesa sana, akaendelea kumwambia Gerson Msigwa Waambieni watu wachukue tahadhari, huu ugonjwa unatesa sana !! Acheni ubishi katika kitu ambacho kiko wazi kabisa, Huko duniani walikoendelea sana wameshaanza kuwachanja mpaka watoto wadogo, je wanataka kuwaua watu wao wote mpaka watoto ??!!!
Hakuna part of my reply nimeandika covid haipo ila nasema mnachokifanya kupitia covid ndicho mnakosea sana na hiyo ndiyo sababu nakataa biashara ya kuaminisha watu kuwa fulani kafa kwa covid.

Kwanza hamchukui hatua muhimu, mnajazana kwa mgonjwa, mnajazana kwenye mazishi, mnajazana every where alafu mgonjwa akisema ni covid, kisa kuhojiwa na wewe unakimbia eti (alisema kaambukizwa)😨
 
Kwakweli Mungu atusaidiye, anahitajika kuzidi wakati wowote! Amina.
 
Tena wanyumbani mwingine anajifunika naye shuka moja na yupo maajabu hayo! Corona inafuatilia wale mnaoshinda pamoja mchana , lakini si mnaolala nao pamoja
Hata waziri mkuu wa Uingereza Boris Johnson aliugua covid akawekwa kwenye ICU na oksijen kibao na alikuwa taaban mpaka watu wakadhani jamaa atachomoka lakini bahati yake baada ya zaidi ya wiki 2 au 3 akapona lakini mke wake ambaye alikuwa ni mja mzito aligunduliwa naye ameambukizwa lakini hakupata shida yeyote ile, wala hakulazwa hospitali hata siku moja, huu ugonjwa ni wa ajabu sana, kwahiyo usidhani kila mtu atakayeambukizwa atalazimika kwenda hospitali, wengine wanapata covid mpaka inaisha bila kujua kama aliugua, lakini wengine wakiupata moto unamuwakia, Sasa kwa kuwa hatujui nani akipata itamdhuru na nani hats akipata haitamdhuru ndio maana tunahamasishana tuende tukachanje bandugu
 
Hata waziri mkuu wa Uingereza Boris Johnson aliugua covid akawekwa kwenye ICU na oksijen kibao na alikuwa taaban mpaka watu wakadhani jamaa atachomoka lakini bahati yake baada ya zaidi ya wiki 2 au 3 akapona lakini mke wake ambaye alikuwa ni mja mzito aligunduliwa naye ameambukizwa lakini hakupata shida yeyote ile, wala hakulazwa hospitali hata siku moja, huu ugonjwa ni wa ajabu sana, kwahiyo usidhani kila mtu atakayeambukizwa atalazimika kwenda hospitali, wengine wanapata covid mpaka inaisha bila kujua kama aliugua, lakini wengine wakiupata moto unamuwakia, Sasa kwa kuwa hatujui nani akipata itamdhuru na nani hats akipata haitamdhuru ndio maana tunahamasishana tuende tukachanje bandugu
Ni kweli kabisa
 
Back
Top Bottom