Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Kama vile vitisho vya mwanzo havikutosha; na kama vile kupigwa na mijeba hakukunoga; na kama kumwagiwa tindikali hakukuonesha kilele cha umafia wa baadhi ya watu muda mfupi uliopita Mhariri Mtendaji wa MwanaHalisi Bw. Saed Kubenea amejikuta tena kwenye kona ya wale "watishao"!
Habari za uhakika na zilizothibitishwa zinasema kuwa Usiku huu (tanzania) Bw. Kubenea amejikuta amepigiwa tena ile "simu ya kifo" na mtu asiyejulikana ambaye namba yake ya simu inaonesha "private". Mtu huyo ambaye hakujitambulisha alitaka kujua kama ni Kubenea anayeandika habari za zisizo nzuri za mmoja wa wanasiasa maarufu ambao wameguswa na Kashfa ya Richmond hivi karibuni.
Bw. Kubenea alipokiri kuwa yeye ni mwandishi wa habari zinazodaiwa mpiga simu alimuambia "sali sala zako za mwisho".
Hadi dakika hii tunavyozungumza juhudi za kuviarifu vyombo vya usalama zinaendelea kwa kasi ili hatua zianze kufuatiliwa hasa baada ya kuzingatia kuwa kupuuzia vitisho kama hivi ni kukaribisha vitendo vya kihuni na vya kihalifu.
KLHN inasimama pamoja na Bw. Kubenea pamoja na waandishi wengine wote ambao wanajikuta kwenye matishio ya kuwafanya washindwe kufanya kazi zao za uhandishi kwa uhuru na kwa uwazi. Endapo jambo lolote litamtokea Bw. Kubenea wakati huu wa msuguano wa mawazo na mgongano wa kifikra na hasa kama ni kitendo cha kihalifu lawama za kwanza na kuwajibika kwa kwanza kutaendea vyombo vyetu vya usalama kwa kushindwa ku "trace" "private" calls kwani ni hatari hata kwa usalama wa nchi!!
Tunatoa wito kwa vyombo vya usalama kuhakikisha usalama wa watu wote hasa wale ambao wana sababu ya kuamini kuwa madhara yanapangwa dhidi yao.
Habari za uhakika na zilizothibitishwa zinasema kuwa Usiku huu (tanzania) Bw. Kubenea amejikuta amepigiwa tena ile "simu ya kifo" na mtu asiyejulikana ambaye namba yake ya simu inaonesha "private". Mtu huyo ambaye hakujitambulisha alitaka kujua kama ni Kubenea anayeandika habari za zisizo nzuri za mmoja wa wanasiasa maarufu ambao wameguswa na Kashfa ya Richmond hivi karibuni.
Bw. Kubenea alipokiri kuwa yeye ni mwandishi wa habari zinazodaiwa mpiga simu alimuambia "sali sala zako za mwisho".
Hadi dakika hii tunavyozungumza juhudi za kuviarifu vyombo vya usalama zinaendelea kwa kasi ili hatua zianze kufuatiliwa hasa baada ya kuzingatia kuwa kupuuzia vitisho kama hivi ni kukaribisha vitendo vya kihuni na vya kihalifu.
KLHN inasimama pamoja na Bw. Kubenea pamoja na waandishi wengine wote ambao wanajikuta kwenye matishio ya kuwafanya washindwe kufanya kazi zao za uhandishi kwa uhuru na kwa uwazi. Endapo jambo lolote litamtokea Bw. Kubenea wakati huu wa msuguano wa mawazo na mgongano wa kifikra na hasa kama ni kitendo cha kihalifu lawama za kwanza na kuwajibika kwa kwanza kutaendea vyombo vyetu vya usalama kwa kushindwa ku "trace" "private" calls kwani ni hatari hata kwa usalama wa nchi!!
Tunatoa wito kwa vyombo vya usalama kuhakikisha usalama wa watu wote hasa wale ambao wana sababu ya kuamini kuwa madhara yanapangwa dhidi yao.