Leak
JF-Expert Member
- Feb 22, 2012
- 52,206
- 42,068
Mahakama ya Hakimu mkazi Kinondoni imeridhia ombi la mawakili wa Mwandishi wa Habari, Said Kubenea la kuondoa maombi ya kuwashtaki Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) pamoja na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaama, Paul Makonda.
Hatua hiyo imejiri leo Ijumaa, Desemba 3, 2021 mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Aron Lyamua ambapo upande wa mleta maombi, Said Kubenea mawakili wake, Hekema Mwasipo umedai kuwa wamefikia hatua hiyo kutokana na kasoro mbalimbali zilizojitokeza katika maombi ya kufungua kesi hiyo na kwamba wanakusudia kuongeza mashtaka ambayo awali hayakuwepo kwenye maombi hayo.
Miongoni mwa kasoro zilizojitokeza ni uandishi wa majina ya mpelekewa maombi na ya aliyeapa ambayo yapo tofauati jambo ambalo wanahofia kuwa yanatakiwa kufafana. Wamedai kuwa wanakusudia kuwashtaki wa watu hao kutokana na madai ya kushindwa kutimiza vyema wajibu wao.
Baada ya maombi hayo wakili wa serikali, Daisy Makakala amekubaliana na ombi la mawakili wa Kubenea bila pingamizi. Hata Hivyo Mawakili wa Kubenea tayari wamewasilisha maombi mengine ambayo yamefanyiwa marekebisho ambayo awali kulikuwa na mapungufu.
Kinachosubiriwa sasa ni mahakama kupanga tarehe ya kusikiliza kesi hiyo pamoja na kuweka wazi namba ya kesi na aina ya mashtaka yanayowakabili.
Hatua hiyo imejiri leo Ijumaa, Desemba 3, 2021 mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Aron Lyamua ambapo upande wa mleta maombi, Said Kubenea mawakili wake, Hekema Mwasipo umedai kuwa wamefikia hatua hiyo kutokana na kasoro mbalimbali zilizojitokeza katika maombi ya kufungua kesi hiyo na kwamba wanakusudia kuongeza mashtaka ambayo awali hayakuwepo kwenye maombi hayo.
Miongoni mwa kasoro zilizojitokeza ni uandishi wa majina ya mpelekewa maombi na ya aliyeapa ambayo yapo tofauati jambo ambalo wanahofia kuwa yanatakiwa kufafana. Wamedai kuwa wanakusudia kuwashtaki wa watu hao kutokana na madai ya kushindwa kutimiza vyema wajibu wao.
Baada ya maombi hayo wakili wa serikali, Daisy Makakala amekubaliana na ombi la mawakili wa Kubenea bila pingamizi. Hata Hivyo Mawakili wa Kubenea tayari wamewasilisha maombi mengine ambayo yamefanyiwa marekebisho ambayo awali kulikuwa na mapungufu.
Kinachosubiriwa sasa ni mahakama kupanga tarehe ya kusikiliza kesi hiyo pamoja na kuweka wazi namba ya kesi na aina ya mashtaka yanayowakabili.