Kubana matumizi: Tumshauri Magufuli kufanya haya:-

2kimo

JF-Expert Member
Jan 23, 2014
2,029
2,071
Naomba tuanze kumshauri raisi, tutoe maoni ya namna ya kufanya baadhi ya mambo ili tuongeze ufanisi ktk uwajibikaji, usimamizi wa rasilimali na kuendelea kubana matumizi! Yeye mwenyewe ameshafanya mengi, mengine mazuri, mengine hayana msingi wowote ktk kuongeza ufanisi na kubana matumizi Ila at least ali try akiwa na dhamira njema! Hebu tumuombe pia atazame na angle hii:-
  1. Kupunguza idadi ya mashirika ya umma yanayofanya kazi moja na hivyo kuongeza mzigo kwa serikali!
    1. Mfano wa hili ni mifuko ya hifadhi za jamii ambayo yote inalengo moja, na yote ipo chini ya Jamhuri! Matokeo yake tumeunda ofisi nyingine SSRA ambayo inaisimamia mifuko hiyo! Ikumbukwe wakurugenzi ndio watu wenye mishahara mikubwa kuliko mtumishi mwingine wa umma including Mkuu wa nchi! Sasa kama tume-merge wizara au kufuta vitengo ili tubane matumizi nadhani wakati sasa umefika wa kuiunganisha hii mifuko! Idadi ya wafanyakazi isipunguzwe kuongeza ufanisi, Ila wakuu wake wapunguzwe kutoka karibu 6 kwa sasa hadi 1! Watakaobaki, watakuwa wakiongoza kurugenzi mbalimbali za mfuko huo mmoja! Hii itasaidia kufanya harmonisation ya funds na utendaji! Pia malipo tofauti kwa beneficiries wa ngazi moja ya mshahara na makato isingeweza kutokea kama ilivyo sasa! Pia SSRA ingekuwa natural death hivyo kuokoa pesa nyingi!
    2. NDC na NHC nadhani wanafanya kazi zote za maendeleo, so ujenzi wa nyumba na Nyanja nyingine za maendeleo vingeunganishwa!
    3. Sanjari na kuziunga NDC, NHC na ule wa muunganiko wa mifuko ya hifadhi, hilo shirika jipya na nyumba na maendeleo ya miji, lingefanya kazi na hii mifuko kupitia bank yao ya umoja! Badala ya shughuli za maendeleo na ujenzi kuwa chini ya shirika moja moja, huku NHC, huku PSPF, NSSF, PPF etc, then wote hawa pesa zao zipite ktk bank yao na NDC/NHC (shirika jipya) likopeshwe kusimamia mipango ya uendelezaji miji, makazi, Viwanda vya kati na shughuli nyingine za maendeleo!
    4. Katika sekta ya Bima, tuunge NHIF na NIC, kwa kuwa zote ni Bima Ila ni just branches tofauti! NIC inakaribia kufa, inawatumishi wengi ambao NHIF ingewatumia bila ya shida!
Msingi wa kuunganisha idara au taasisi sio tu utapunguza gharama kwa kupunguza wakurugenzi wakuu, bali pia utaruhusu utilisation ya resources ambazo nyingine zinatumika kidogo huku wengine wakiwa na upungufu na wengine wakiwa na plenty!
Kwa ilivyo sasa baadhi ya ofisi kama TRA inafanya ktk sekta tofauti bila ya kubadilishwa au kuzaliwa taasisi nyingine! Vinabaki kuwa vitengo tu ndani ya mfumo mmoja, kama wanaosimamia ushuru wa forodha bandarini na airports, biashara ndogondogo, nyumba/majengo, leseni za udereva etc! Hizi ofisi tunazoomba viunganishwe zinaweza kufanya review ya model ya TRA na jinsi inavyofanya kazi kwa ufanisi! Kukua kwa taaluma ya IT na uwepo wa harmonisation ya taarifa za kibank, mishahara, vitambulisho vya taifa, tin number kwa watanzania na mpango wa universal Bima ya afya vyote vinazua ushawishi wa kumerge taasisi, ili monitoring na issues za accountability/transparency ziimarike zaidi!
Toa maoni yako kusaidia kujenga mifumo bora zaidi ya kuimarisha uchumi!
 
Back
Top Bottom