Mwajiri wangu amenibambikizia kesi ya wizi, akanishitaki Polisi kisha uchunguzi ukafanywa na jeshi hilo la Polisi majibu yakaja kwamba sina kosa hilo na wakashindwa kunipeleka mahakamani.
Baadaye Mwajiri akaamua kunifukuza kazi nikiwa na mkataba wa kudumu. Niliamua kumburuza CMA Mwajiri wangu.
Swali langu ni kwamba " Nikishinda hii kesi huko CMA na kurudi kazini. Je, naweza kumfungulia Mwajiri wangu kesi ya Madai kutokana na kubambikizwa kesi ya wizi?
Naomba msaada wa kisheria kuhusu hili.
Baadaye Mwajiri akaamua kunifukuza kazi nikiwa na mkataba wa kudumu. Niliamua kumburuza CMA Mwajiri wangu.
Swali langu ni kwamba " Nikishinda hii kesi huko CMA na kurudi kazini. Je, naweza kumfungulia Mwajiri wangu kesi ya Madai kutokana na kubambikizwa kesi ya wizi?
Naomba msaada wa kisheria kuhusu hili.