Kubadilisha Mfumo wa Elimu ili Kupata Shule Zinazojitegemea na Kujiendesha kwa Faida

Logikos

JF-Expert Member
Feb 26, 2014
12,434
19,452
Part One
Title: KUBADILISHA MFUMO WA ELIMU ILI KUPATA SHULE ZINAZOJITEGEMEA NA KUJIENDESHA KWA FAIDA BILA KUTEGEMEA KARO, VILEVILE KUZALISHA WAHITIMU WENYE UJUZI WA MAZINGIRA YAO NA UHAKIKA WA KIPATO

Utangulizi
Kuna jambo halipo sawa kwenye mukstabali wa Elimu yetu nchini pamoja na dunia kwa ujumla. Vijana wengi wanaohitimu wanakosa ajira hivyo kutokuwa msaada kwa jamii yao, kama hio haitoshi wastani wa mtu kuja kupata ajira au kuanza kazi kwa manufaa yake na ya jamii ni zaidi ya miaka 20. Hapo ni baada ya kusoma chekechea, kuanza la kwanza akiwa na miaka sita na kumaliza la saba akiwa na miaka 12, ukiongeza miaka minne ya sekondari na mingine miwili hapo utaona kwamba elimu ya sekondari
atamaliza akiwa na miaka 18 au zaidi na hapo chuo bado kinamsubiri.

Masomo yanayofundishwa sio tu hayaendi sambamba na uhitaji wa soko la ajira na uzalishaji bali kuna tasnia kama michezo na sanaa inaonekana kama ni burudani hivyo hayapewi kipaumbele katika mitaala.

Kama hio haitoshi elimu imekuwa ghali sana, na ni moja ya matumizi yenye gharama katika familia kuliko mahitaji mengine. Yaani familia inagharamika sana hata kuingia katika umasikini ili kuwatafutia ufunguo wa maisha watoto wao, ila mwisho wa siku kujikuta ufunguo huo hauna msaada katika maisha ya huyo kijana zaidi ya madeni kwa kijana na jamii kukosa nguvu kazi kwa kutokunufaika na ujuzi wa kijana huyo, manufaa ambayo yangepatikana iwapo huyo kijana angepatiwa mafunzo yanayohitajika katika jamii.

Kwenye andiko hili muandishi amejitahidi kuonyesha njia mbadala ambazo zitahakikisha yafuatayo: -
  1. Kuhakikisha gharama ya Elimu inakuwa rafiki kwa kila mzazi kuweza kumudu na wale wasio na uwezo wanapata ujuzi kwa manufaa ya Taifa la kesho.​
  2. Kuhakikisha Shule zinajiendesha zenyewe kwa kutokutegemea karo, ruzuku au michango ya wazazi.​
  3. Kuhakikisha shule sio tu zinafundisha bali zinazalisha na katika uzalishaji huo wanafunzi wanapata ujuzi unaoendena na mazingira yao.​
  4. Badala ya wanafunzi kulipa na kuondoka na madeni wakihitimu, kuwepo na mfumo ambao kijana akihitimu anakuwa na kianzio cha pesa cha kumuwezesha kupata elimu ya juu au kwa wale wanaoanza maisha kuweza kujikimu. Yaani kama vile mzee anavyopata kiinua mgongo akistaafu, kijana huyu anapata kilainisha mgongo kabla ya kuingia mtaani.​

Andiko hili linatambua fika umuhimu wa elimu kama nguzo ya jamii na badala ya elimu kuwa chanzo cha umasikini wa familia kwa kuingia kwenye madeni ili kusomesha watoto wao, tunahitaji kurudi kwenye reli ili Elimu ifanye kile kilichokusudiwa nacho ni kumuwezesha binadamu kupambana na kuyamudu mazingira yake.

Ni ukweli usiopingika ustawi wa jamii na ongezeko la uchumi halitegemei mali asili, mitaji na teknolojia pekee bali idadi na ubora wa nguvukazi pia.

Andiko hili lina sehemu kubwa mbili ya kwanza ni kuelezea jinsi ya kubadilisha mfumo wa shule uwe wa kujitegemea na kuzalisha wahimu wenye ujuzi na tija, na sehemu ya pili itaelezea jinsi ya kutatua changamoto zinazoikumba elimu ya sasa. Baadhi ya changamoto hizo
ni: -
  1. Ukosefu wa Mitaji kwa Mashule na Gharama Kubwa ya Kusomesha kwa Wazazi.
  2. Elimu kutoenda sambamba na mfumo wa ajira, au uzalishaji
  3. Mfumo wa Elimu unaochukua muda mrefu kabla ya Wahitimu kupata fursa ya kuanza kazi na kuzalisha.
  4. Mitaala kutotoa kipaumbele kwa baadhi ya mafunzo kama Sanaa na Michezo, hivyo taifa kupoteza vipaji.
  5. Kipimo cha ufaulu kinaangalia ufaulu wa mitihani na sio vigezo vingine jambo linalowatenga watu wenye Uwezo tofauti ambao hauwezi kupimwa kwa mitihani ya darasani.
  6. Wanafunzi kutokujifunza vitu wanavyopenda bali masomo ambayo watapata chuo kizuri au kazi yenye mshahara mkubwa.
  7. Elimu inahamasisha mashindano ya nani kapata maksi nzuri zaidi na sio uelewa.
  8. Ualimu sio Wito tena bali kazi ya kujipatia Kipato, wengi wanafundisha sio kwa mapenzi bali njia ya kujikimu kimaisha.
  9. Wanafunzi kujifunza ili kupata Kazi na sio Kujifunza ili kuongeza Uelewa, au Kujifunza wanachopenda ili kutimiza ndoto zao.
  10. Elimu inafundisha kukariri badala ya kukuza fikra na tabia ya kuhoji

ITAENDELEA...
 
PART TWO:
Kuzifanya Shule kuwa Nguzo Muhimu ya Jamii
Shule ni muhimu sana katika Jamii inatoa elimu, na angalau hata kinadharia ni ufunguo wa maisha kwa wanafunzi, shule zinatakiwa kuwapa nyenzo wanafunzi ya kuweza kupambana na mazingira yao na kuhakikisha maisha yao ya ukubwani yanakuwa bora. Shule ni viwanda vya nguvukazi ili kuhakikisha ustawi wa jamii

Ingawa kwa bahati mbaya au vinginevyo, uhalisia umegeuka, kwenda shule na kupata elimu hakumpi tena kijana uhakika wa ajira wala kipato bali shule zimekuwa mwanzo wa madeni kwake na familia yake kwa ujumla.

Moja ya pendekezo ni kubadilisha mashule na kuyafanya yajitegemee kwa kuzalisha na kuingiza kipato wakati huo huo kuhakikisha wanafunzi wanapata mafunzo kwa vitendo.

Pendekezo ni kubadilisha shule ili ziwe moyo wa jamii, kufanya mashule yawe kichocheo cha maendeleo kwa kutoa elimu na mahitaji ya wanajamii.

Kwa ufupi ni kupata shule zenye sifa zifuatazo:

  1. Zinafundisha kwa vitendo na kutenda.
  2. Zinazalisha na kuuza hivyo kupata faida.
  3. Zinazopata kipato na kujiendesha.
Pendekezo la Mfumo
Pendekezo la andiko hili ni kwa shule kugawanyika katika makundi matatu. Shule za Awali, Shule za Kati na Vyuo.

Shule za Awali inapendekezwa ziwe za wanafunzi watoto ambao bado ni wadogo na ziwe shule za kutwa. Shule hizi ziwe ni chekechea mpaka darasa la tatu, wanafunzi hawa watakuwa wana umri mdogo mpaka miaka tisa na inapendekezwa wawe wanasoma shule za kutwa, ili waendelee kuwa karibu na wazazi wao.

Shule za Kati zianzie darasa la nne miaka kumi na hizi ndio shule zinazoongelewa katika andiko hili. Shule hizi zitajumuisha Darasa la Nne mpaka kidato cha sita, (Yaani la nne mpaka la saba na kidato cha kwanza mpaka cha sita).

Baada ya hapo kijana huyu atakuwa ameiva kuweza kuingia mtaani kuendelea kuzalisha kwa kujiajiri au kuajiriwa au kama akipenda kuendelea na elimu ya juu ya chuo. Ingawa mpaka kuhitimu kwake atakuwa ana nyenzo zote za kumuwezesha kuishi kama raia mzalishaji anayeweza kupambana na mazingira ya nchi yake, ukizingatia atakachokifanya ndicho alichokuwa anafanya maisha yake yote.

Ingawa shule huwa zinaendeshwa kwa misimu na kunakuwa na wakati wa kupumzika, uzalishaji ni wa mwaka mzima, inapendekezwa shule hizi ziwe na wanafunzi wengi ambao wanasoma na kupata likizo muda tofauti ili kuhakikisha kwamba uzalishaji unafanyika mwaka mzima. Kwahio wanafunzi hawa watakuwa wanachukua likizo kwa zamu, masomo ya kinadharia kwa zamu na ya vitendo pia kwa kupeana zamu kadri inavyohitajika

Kijana huyu kama tukakavyoona hapo baadae akihitimu Sekondari sio tu ataondoka na ujuzi wa kufanya shughuli kwa manufaa yake na jamii bali pia ataondoka na kilainisha mgongo / kianzio cha kuanzia maisha kama vile mstaafu anavyopewa kiinua mgongo.
Itaendelea....
 
Title: KUBADILISHA MFUMO WA ELIMU ILI KUPATA SHULE ZINAZOJITEGEMEA NA KUJIENDESHA KWA FAIDA BILA KUTEGEMEA KARO, VILEVILE KUZALISHA WAHITIMU WENYE UJUZI WA MAZINGIRA YAO NA UHAKIKA WA KIPATO

Utangulizi
Kuna jambo halipo sawa kwenye mukstabali wa Elimu yetu nchini pamoja na dunia kwa ujumla. Vijana wengi wanaohitimu wanakosa ajira hivyo kutokuwa msaada kwa jamii yao, kama hio haitoshi wastani wa mtu kuja kupata ajira au kuanza kazi kwa manufaa yake na ya jamii ni zaidi ya miaka 20. Hapo ni baada ya kusoma chekechea, kuanza la kwanza akiwa na miaka sita na kumaliza la saba akiwa na miaka 12, ukiongeza miaka minne ya sekondari na mingine miwili hapo utaona kwamba elimu ya sekondari
atamaliza akiwa na miaka 18 au zaidi na hapo chuo bado kinamsubiri.

Masomo yanayofundishwa sio tu hayaendi sambamba na uhitaji wa soko la ajira na uzalishaji bali kuna tasnia kama michezo na sanaa inaonekana kama ni burudani hivyo hayapewi kipaumbele katika mitaala.

Kama hio haitoshi elimu imekuwa ghali sana, na ni moja ya matumizi yenye gharama katika familia kuliko mahitaji mengine. Yaani familia inagharamika sana hata kuingia katika umasikini ili kuwatafutia ufunguo wa maisha watoto wao, ila mwisho wa siku kujikuta ufunguo huo hauna msaada katika maisha ya huyo kijana zaidi ya madeni kwa kijana na jamii kukosa nguvu kazi kwa kutokunufaika na ujuzi wa kijana huyo, manufaa ambayo yangepatikana iwapo huyo kijana angepatiwa mafunzo yanayohitajika katika jamii.

Kwenye andiko hili muandishi amejitahidi kuonyesha njia mbadala ambazo zitahakikisha yafuatayo: -
  1. Kuhakikisha gharama ya Elimu inakuwa rafiki kwa kila mzazi kuweza kumudu na wale wasio na uwezo wanapata ujuzi kwa manufaa ya Taifa la kesho.​
  2. Kuhakikisha Shule zinajiendesha zenyewe kwa kutokutegemea karo, ruzuku au michango ya wazazi.​
  3. Kuhakikisha shule sio tu zinafundisha bali zinazalisha na katika uzalishaji huo wanafunzi wanapata ujuzi unaoendena na mazingira yao.​
  4. Badala ya wanafunzi kulipa na kuondoka na madeni wakihitimu, kuwepo na mfumo ambao kijana akihitimu anakuwa na kianzio cha pesa cha kumuwezesha kupata elimu ya juu au kwa wale wanaoanza maisha kuweza kujikimu. Yaani kama vile mzee anavyopata kiinua mgongo akistaafu, kijana huyu anapata kilainisha mgongo kabla ya kuingia mtaani.​

Andiko hili linatambua fika umuhimu wa elimu kama nguzo ya jamii na badala ya elimu kuwa chanzo cha umasikini wa familia kwa kuingia kwenye madeni ili kusomesha watoto wao, tunahitaji kurudi kwenye reli ili Elimu ifanye kile kilichokusudiwa nacho ni kumuwezesha binadamu kupambana na kuyamudu mazingira yake.

Ni ukweli usiopingika ustawi wa jamii na ongezeko la uchumi halitegemei mali asili, mitaji na teknolojia pekee bali idadi na ubora wa nguvukazi pia.

Andiko hili lina sehemu kubwa mbili ya kwanza ni kuelezea jinsi ya kubadilisha mfumo wa shule uwe wa kujitegemea na kuzalisha wahimu wenye ujuzi na tija, na sehemu ya pili itaelezea jinsi ya kutatua changamoto zinazoikumba elimu ya sasa. Baadhi ya changamoto hizo
ni: -
  1. Ukosefu wa Mitaji kwa Mashule na Gharama Kubwa ya Kusomesha kwa Wazazi.
  2. Elimu kutoenda sambamba na mfumo wa ajira, au uzalishaji
  3. Mfumo wa Elimu unaochukua muda mrefu kabla ya Wahitimu kupata fursa ya kuanza kazi na kuzalisha.
  4. Mitaala kutotoa kipaumbele kwa baadhi ya mafunzo kama Sanaa na Michezo, hivyo taifa kupoteza vipaji.
  5. Kipimo cha ufaulu kinaangalia ufaulu wa mitihani na sio vigezo vingine jambo linalowatenga watu wenye Uwezo tofauti ambao hauwezi kupimwa kwa mitihani ya darasani.
  6. Wanafunzi kutokujifunza vitu wanavyopenda bali masomo ambayo watapata chuo kizuri au kazi yenye mshahara mkubwa.
  7. Elimu inahamasisha mashindano ya nani kapata maksi nzuri zaidi na sio uelewa.
  8. Ualimu sio Wito tena bali kazi ya kujipatia Kipato, wengi wanafundisha sio kwa mapenzi bali njia ya kujikimu kimaisha.
  9. Wanafunzi kujifunza ili kupata Kazi na sio Kujifunza ili kuongeza Uelewa, au Kujifunza wanachopenda ili kutimiza ndoto zao.
  10. Elimu inafundisha kukariri badala ya kukuza fikra na tabia ya kuhoji

ITAENDELEA...
Unamaanisha elimu iwe biashara kama real estate Tanzania ina washaur wa hovyo
 
Title: KUBADILISHA MFUMO WA ELIMU ILI KUPATA SHULE ZINAZOJITEGEMEA NA KUJIENDESHA KWA FAIDA BILA KUTEGEMEA KARO, VILEVILE KUZALISHA WAHITIMU WENYE UJUZI WA MAZINGIRA YAO NA UHAKIKA WA KIPATO

Utangulizi
Kuna jambo halipo sawa kwenye mukstabali wa Elimu yetu nchini pamoja na dunia kwa ujumla. Vijana wengi wanaohitimu wanakosa ajira hivyo kutokuwa msaada kwa jamii yao, kama hio haitoshi wastani wa mtu kuja kupata ajira au kuanza kazi kwa manufaa yake na ya jamii ni zaidi ya miaka 20. Hapo ni baada ya kusoma chekechea, kuanza la kwanza akiwa na miaka sita na kumaliza la saba akiwa na miaka 12, ukiongeza miaka minne ya sekondari na mingine miwili hapo utaona kwamba elimu ya sekondari
atamaliza akiwa na miaka 18 au zaidi na hapo chuo bado kinamsubiri.

Masomo yanayofundishwa sio tu hayaendi sambamba na uhitaji wa soko la ajira na uzalishaji bali kuna tasnia kama michezo na sanaa inaonekana kama ni burudani hivyo hayapewi kipaumbele katika mitaala.

Kama hio haitoshi elimu imekuwa ghali sana, na ni moja ya matumizi yenye gharama katika familia kuliko mahitaji mengine. Yaani familia inagharamika sana hata kuingia katika umasikini ili kuwatafutia ufunguo wa maisha watoto wao, ila mwisho wa siku kujikuta ufunguo huo hauna msaada katika maisha ya huyo kijana zaidi ya madeni kwa kijana na jamii kukosa nguvu kazi kwa kutokunufaika na ujuzi wa kijana huyo, manufaa ambayo yangepatikana iwapo huyo kijana angepatiwa mafunzo yanayohitajika katika jamii.

Kwenye andiko hili muandishi amejitahidi kuonyesha njia mbadala ambazo zitahakikisha yafuatayo: -
  1. Kuhakikisha gharama ya Elimu inakuwa rafiki kwa kila mzazi kuweza kumudu na wale wasio na uwezo wanapata ujuzi kwa manufaa ya Taifa la kesho.​
  2. Kuhakikisha Shule zinajiendesha zenyewe kwa kutokutegemea karo, ruzuku au michango ya wazazi.​
  3. Kuhakikisha shule sio tu zinafundisha bali zinazalisha na katika uzalishaji huo wanafunzi wanapata ujuzi unaoendena na mazingira yao.​
  4. Badala ya wanafunzi kulipa na kuondoka na madeni wakihitimu, kuwepo na mfumo ambao kijana akihitimu anakuwa na kianzio cha pesa cha kumuwezesha kupata elimu ya juu au kwa wale wanaoanza maisha kuweza kujikimu. Yaani kama vile mzee anavyopata kiinua mgongo akistaafu, kijana huyu anapata kilainisha mgongo kabla ya kuingia mtaani.​

Andiko hili linatambua fika umuhimu wa elimu kama nguzo ya jamii na badala ya elimu kuwa chanzo cha umasikini wa familia kwa kuingia kwenye madeni ili kusomesha watoto wao, tunahitaji kurudi kwenye reli ili Elimu ifanye kile kilichokusudiwa nacho ni kumuwezesha binadamu kupambana na kuyamudu mazingira yake.

Ni ukweli usiopingika ustawi wa jamii na ongezeko la uchumi halitegemei mali asili, mitaji na teknolojia pekee bali idadi na ubora wa nguvukazi pia.

Andiko hili lina sehemu kubwa mbili ya kwanza ni kuelezea jinsi ya kubadilisha mfumo wa shule uwe wa kujitegemea na kuzalisha wahimu wenye ujuzi na tija, na sehemu ya pili itaelezea jinsi ya kutatua changamoto zinazoikumba elimu ya sasa. Baadhi ya changamoto hizo
ni: -
  1. Ukosefu wa Mitaji kwa Mashule na Gharama Kubwa ya Kusomesha kwa Wazazi.
  2. Elimu kutoenda sambamba na mfumo wa ajira, au uzalishaji
  3. Mfumo wa Elimu unaochukua muda mrefu kabla ya Wahitimu kupata fursa ya kuanza kazi na kuzalisha.
  4. Mitaala kutotoa kipaumbele kwa baadhi ya mafunzo kama Sanaa na Michezo, hivyo taifa kupoteza vipaji.
  5. Kipimo cha ufaulu kinaangalia ufaulu wa mitihani na sio vigezo vingine jambo linalowatenga watu wenye Uwezo tofauti ambao hauwezi kupimwa kwa mitihani ya darasani.
  6. Wanafunzi kutokujifunza vitu wanavyopenda bali masomo ambayo watapata chuo kizuri au kazi yenye mshahara mkubwa.
  7. Elimu inahamasisha mashindano ya nani kapata maksi nzuri zaidi na sio uelewa.
  8. Ualimu sio Wito tena bali kazi ya kujipatia Kipato, wengi wanafundisha sio kwa mapenzi bali njia ya kujikimu kimaisha.
  9. Wanafunzi kujifunza ili kupata Kazi na sio Kujifunza ili kuongeza Uelewa, au Kujifunza wanachopenda ili kutimiza ndoto zao.
  10. Elimu inafundisha kukariri badala ya kukuza fikra na tabia ya kuhoji

ITAENDELEA...
Kazi ya kuja PM kutuomba kura umeianza rasmi naona sasa
 
Unamaanisha elimu iwe biashara kama real estate Tanzania ina washaur wa hovyo
Moja elimu sasa hivi sio biashara ? Unadhani hizo Private Schools zinapewa ruzuku ?

Pili Namaanisha Shule / Taasisi ziweze kujiendesha kwa kuzalisha kila inachofundisha na kutoa products..., hivyo faida kwa shule ni kupata kipato na kwa wanafunzi ni kupata apprenticeship yaani mafunzo kazini.

Hapo kabla mfumo huu wa shule haujaanza watu walikuwa wanafundishwa kwa kutumia apprenticeship (baba yako ni mfua chuma na wewe utakuwa mfua chuma) kama ni muoka mikate na wewe utakuwa muoka mikate, kama ni mtengeneza viatu na wewe hali kadhalika....

By the way asante kwa comment..., naomba labda nikuulize nini faida ya elimu..., na ni upi mbadala wa elimu ya vitendo. Kufananisha elimu na real estate sio mfano mzuri ila kama shule inafundisha wood joinery na kutengeneza furniture kwanini hayo makochi yanayotengenezwa yasiuzwe, au shule kuwa na karakana ? Na kama hayauziki basi wanachofundisha hakina tija....
 
Kazi ya kuja PM kutuomba kura umeianza rasmi naona sasa
Mkuu hapa hakuna Kura ndio maana nimeweka Jukwaa la Elimu ili tuchangie Hoja / Issue at hand na sio mtoa hoja..., kwahio tashukuru sana kama ukitoa Pro and Cons na kwanini haiwezekani na sio motive behind.

Nadhani wote tunaweza tukakubaliana kwamba kilichopo sasa is not fit for purpose.... (By the way sijawahi maishani mwangu kuomba kura ya mtu, nataka chochote mtu atakachotoa ni with merit na sio vinginevyo); Mara zote huwa nakubaliana na maneno ya Magreth Thatcher...
"I love argument. I love debate. I don't expect anyone just to sit there and agree with me - that's not their job."
Kwahio I value constructive critisism more than kupakana mafuta kwa mgongo wa chupa

Unaona sasa tunatoka nje ya mjadala..... By the way tashukuru kama tukirudi kwenye Mada Husika, unadhani kwanini huu mfumo wa elimu uliopo unafaa zaidi na proposal hii haifai ?
 
Mkuu hapa hakuna Kura ndio maana nimeweka Jukwaa la Elimu ili tuchangie Hoja / Issue at hand na sio mtoa hoja..., kwahio tashukuru sana kama ukitoa Pro and Cons na kwanini haiwezekani na sio motive behind.

Nadhani wote tunaweza tukakubaliana kwamba kilichopo sasa is not fit for purpose.... (By the way sijawahi maishani mwangu kuomba kura ya mtu, nataka chochote mtu atakachotoa ni with merit na sio vinginevyo); Mara zote huwa nakubaliana na maneno ya Magreth Thatcher...
"I love argument. I love debate. I don't expect anyone just to sit there and agree with me - that's not their job."
Kwahio I value constructive critisism more than kupakana mafuta kwa mgongo wa chupa

Unaona sasa tunatoka nje ya mjadala..... By the way tashukuru kama tukirudi kwenye Mada Husika, unadhani kwanini huu mfumo wa elimu uliopo unafaa zaidi na proposal hii haifai ?
Hauwezi kutulazimisha kukubaliana na hoja zako, solve kwanz tatizo la Ajira
 
Hauwezi kutulazimisha kukubaliana na hoja zako, solve kwanz tatizo la Ajira
Mkuu nimekulazimisha wapi ukubaliane na mimi ?, Nimeleta wazo ambalo kwa upande wako linaweza likawa pumba (well its okay) ila hata kama kuleta kwangu wazo kumeleta huu mjadala huoni ni faida ?

Narudia maneno ya Thatcher..., "I love argument. I love debate. I don't expect anyone just to sit there and agree with me - that's not their job."

Pili tatizo la ajira huoni nimesema kwamba shule kuzalisha watu wenye ujuzi unaoendana na mazingira yao na soko la ajira..., kwa wanafunzi hawa maisha yao yote kusoma na kufanya vile vinavyotakiwa na soko..., hata wakitoka kwenye huko kusoma ni muendelezo wa kile walichokuwa wanafanya..., kumbuka hizi shule will also be industries....

By the way hauoni kwamba huenda tatizo la ajira lina correlation na elimu wanayopata hao wahitaji wa hizo ajira ? Sasa unaweza kutatua tatizo la hitimisho wakati kumbe kinachosababisha ni kilichotangulia ambacho hautaki kukibadilisha...
 
Yan anaund makal ili spate vote za pm

"You have to believe in facts," said Mr Obama, "without facts there is no basis for cooperation.
"If I say this is a podium and you say this is an elephant, it is going to be hard for us to cooperate."

Anyway kama mada inaongelea Elimu na arguments unazoleta hazihusiani na mada tajwa hapo juu..., huoni kwamba hatulitendei haki hili Jukwaa la Elimu ? Ingawa ingekuwa Chit Chat ningekuelewa....

Anyway to each his / her Own.... Back to the matter at hand una cha kuchangia chochote kuhusu mustakabali wa elimu yetu kwa sasa Duniani ?
 
huu ndio ushauri mbovu kuliko yote toka Chief Hangaya aingie kasirini.
Kwanini Mkuu twende kwa Hoja. Unadhani kwanini Shule zisiwe Self Sustainable ?

Sasa hivi shule zinategemea Karo na za Serikali Ruzuku toka Serikalini n.k., pamoja na hayo pesa hizo hazitoshi kwahio kupata kitu substandard....

Pia nadharia kwenye mashule ni nyingi hakuna vitendo...., kwahio unaona kuna ubaya gani wanafunzi hao kupata elimu ya nadharia na vitendo na kwa shule kufanya vitu kwa vitendo n.k. Ni aibu shule kukosa chakula wakati nchi ni ya Kilimo ina ardhi ya kutosha na kilimo cha sasa wala sio cha nguvu kazi kwamba wanafunzi watapata suluba..., kuna wanafunzi wana vipaji kwanini shule siziwe na timu ambazo zina-compete kwenye mashindano ? Kuna waimbaji na waigizaji kwanini wasitoe kazi za Kisanii ziingie sokoni...

Asante kwa mchango wako ila kwanini unadhani hili haliwezekani
 
Ushauri wake huwezi kuuweka kweny matendo ata chembe
Hivi nikikwambia Paraguay kuna mfumo wa Self Sustainable Schools utasemaje ?


Kwa kutumia mfumo wa Kilimo na Miradi biashara iliyowazunguka ili kuwapa elimu na elimu kazini wanafunzi hao....

Turudi kwenye mada husika kwanini haiwezekani ?, Kusema haiwezekani bila kuongea ni kwanini tena kwenye Jukwaa la Elimu sijui nikuweke kwenye kundi gani....
 
Hivi nikikwambia Paraguay kuna mfumo wa Self Sustainable Schools utasemaje ?


Kwa kutumia mfumo wa Kilimo na Miradi biashara iliyowazunguka ili kuwapa elimu na elimu kazini wanafunzi hao....

Turudi kwenye mada husika kwanini haiwezekani ?, Kusema haiwezekani bila kuongea ni kwanini tena kwenye Jukwaa la Elimu sijui nikuweke kwenye kundi gani....
Hiwezekani ni mpaka tupewe elimu jinsi gani mfumo utakuwa na structure kiupana zaidi ndipo tuamue kama Taifa
 
Hivi nikikwambia Paraguay kuna mfumo wa Self Sustainable Schools utasemaje ?


Kwa kutumia mfumo wa Kilimo na Miradi biashara iliyowazunguka ili kuwapa elimu na elimu kazini wanafunzi hao....

Turudi kwenye mada husika kwanini haiwezekani ?, Kusema haiwezekani bila kuongea ni kwanini tena kwenye Jukwaa la Elimu sijui nikuweke kwenye kundi gani....
Hiwezekani ni mpaka tupewe elimu jinsi gani mfumo utakuwa na structure kiupana zaidi ndipo tuamue kama Taifa,ASA Uzi upo jf kwa watu laki tano
 
Hiwezekani ni mpaka tupewe elimu jinsi gani mfumo utakuwa na structure kiupana zaidi ndipo tuamue kama Taifa,ASA Uzi upo jf kwa watu laki tano
Imebidi niangalie tupo Jukwaa gani mara mbili...., Mkuu tukiongelea Mbinu za Tanzania kuchukua Kombe la dunia haimaanishi tutachukua kombe lijalo au kama tutachukua maishani mwetu..., ni kuongelea mbinu theoretically... baada ya hapo watu wanaweza kuboresha, kubadilisha au kupuuzia ila haikatazi kuongelea suala...

Hii ni theory on paper ambayo inaweza ikawa au isiwe applied, kabla ya ku-move practically ni lazima kitu kiwepo on paper na watu kufanya due dilligence..., na katika huo upembuzi yakinifu ni lazima kuangalia faida na hasara za mfumo uliopo na kama unaushauriwa unawezekana au una mapungufu kiasi gani.... (we have a dialogue and we debate kwa hoja sio vioja).

Kumbuka hapa sisi sio watengeneza Sera ila kama Concerned Citizens ni wadau wa kuweza kusema au kuchangia pale tunapoona panaweza kurekebishwa..., kwahio badala ya kusema haiwezekani swali ni kuuliza mapana yake yapoje na kama ulivyoona hili andiko bado linaendelea kujibu hizo changamoto zitatatuliwa vipi...

Issue hapa sio kuwafanya watunga sera wabadilike bali ni kuonyesha mapungufu yaliyopo; wayachukue au wasiyachukue hilo ni suala lao mimi kama concerned citizen takuwa nimefanya wajibu wangu kwa kueleza kile ninachoona kinafaa (In my Humble Opinion)
 
Back
Top Bottom