Kuanzisha Vyama vipya misibani kama cha 'MboKa ' Alliance ni kujitafutia laana za lazima

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,548
108,859
Ifike muda sasa tujifunze kuheshimu misiba na hasa wale ambao tunawaomboleza ili kuonyesha kwamba kweli tumeumia na kuondoka Kwao hapa duniani na tuache hizi tabia za ' Kipuuzi ' za kila mara kupenda kutumia misiba kama sehemu yetu ya Kujiimarisha na kupata Sifa Kisiasa.

Chama kipya cha ' MboKa ' Alliance hakiwezi kuwa na baraka kama kimeanzishiwa Msibani sana sana tu kinaweza kikajikuta kinapata ' laana ' ambayo itakiangamiza zaidi.

Kwahiyo mnataka kutuambia kwamba bila Msiba huo kutokea huu Muungano wa ' Kinafiki ' wa ' MboKa ' Alliance usingetokea? Je tukisema labda kwa tamaa zenu za Kisiasa labda nyie ndiyo ' Wachawi ' wenyewe ambao ' mmemroga ' Marehemu ili afe halafu kupitia Msiba wake mjijenge Kisiasa tutakuwa tunakosea?

Siasa bora, njema na zenye mantiki na tija huwa hazianzishwi Misibani bali kuna ' mazingira ' maalum ambayo yanaweza yakachochea Watu kufanya Siasa ila kamwe na hata katika Mila za Kiafrika Misibani ni sehemu ya Kuomboleza tu na kumuombea Marehemu makazi mema huko aendako.

Nawasubiri kwa hamu sana niwaone hao Wanachama wa awali wa Chama kipya nchini Tanzania cha ' MboKa ' Alliance ili nami niweze kujua idadi kamili ya Watu ambao wanaenda kupata ' laana ' ya Kutukuka ya Marehemu Mwalimu ili pengine liwe fundisho kwa ' Wanafiki ' wengine wote wa Kisiasa nchini Tanzania.

Nawasilisha.
 
Hawa CHADEMA NA ACT wapo frustrated mno NA AWAMU HII...

Ukichunguza huu muungano wa AJABU NI UWOGA WAO na kuanza kujihami ili wasije poteza JIMBO... Na wameisha ona dalili tayari za kulipoteza HILI JIMBO na ndio maana wameanza kujihami mapema mno kwa kufanya mambo ya AJABU AJABU..

Na ukiangalia kwa JICHO LA TATU CHADEMA wajanja sana hapa wameamua kuunda URAFIKI NA ZITTO kwa sababu tu wanajua ZITTO mkoani KIGOMA kaushawishi kapo kapo hivyo ili kutolipopteza JIMBO lazima wawe karibu na huyu JAMAA.
 
Hivi kuunganisha vyama msibani in sahihi? Au walipaswa wamalize msiba kwanza wakirudi Dodoma ndo wakae kikao cha kuunganisha hivyo vyama na masharti ya kuungana yawekwe wazi. Kesho kutwa tu hapo Kakonko kutakuwa na Uchaguzi utashangaa kila Chama kitaweka Mgombea Ubunge.
 
Kama mnaungana Muwe tayari kugawana Ruzuku Pia , Mara nyingi Mchawi Wa Muungano Wa Vyama vya siasa ni Ruzuku ya vyama vya Siasa , kila chama kinataka Ruzuku
 
Kuungana na kutengana sijui ni jambo gani jema la kumpendeza mungu mpaka atoe laana. Kwani msibani kuna kipi cha kusababisha au kuzuia muungano wowote as long aliyekufa ni mwanasiasa na walioungana ni wanasiasa?

Hata mainjinia wanaweza kukutana kwenye msiba wa injinia mwenzao na wakaamua kuunganisha kampuni zao wazo walilolipata msibani wala hakuna tatizo. Kuungana ni baraka.

Usihukumu usije ukahukumiwa, laana hutoi wewe wala hupangi jinsi ya kupata laana. Wala Mungu hapangiwi!
 
Ahsante kwa Kuwasilisha Mkuu..Nikadhani umetoa hoja Ijadiliwe ...Kumbe Umehukumu..
Wengine huwa Tunaamini Katika Muungano haijalishi ni wapi au wakati gani Mtaungana..
Sikupingi ni Wazo langu.
 
Ifike muda sasa tujifunze kuheshimu misiba na hasa wale ambao tunawaomboleza ili kuonyesha kwamba kweli tumeumia na kuondoka Kwao hapa duniani na tuache hizi tabia za ' Kipuuzi ' za kila mara kupenda kutumia misiba kama sehemu yetu ya Kujiimarisha na kupata Sifa Kisiasa.

Chama kipya cha ' MboKa ' Alliance hakiwezi kuwa na baraka kama kimeanzishiwa Msibani sana sana tu kinaweza kikajikuta kinapata ' laana ' ambayo itakiangamiza zaidi.

Kwahiyo mnataka kutuambia kwamba bila Msiba huo kutokea huu Muungano wa ' Kinafiki ' wa ' MboKa ' Alliance usingetokea? Je tukisema labda kwa tamaa zenu za Kisiasa labda nyie ndiyo ' Wachawi ' wenyewe ambao ' mmemroga ' Marehemu ili afe halafu kupitia Msiba wake mjijenge Kisiasa tutakuwa tunakosea?

Siasa bora, njema na zenye mantiki na tija huwa hazianzishwi Misibani bali kuna ' mazingira ' maalum ambayo yanaweza yakachochea Watu kufanya Siasa ila kamwe na hata katika Mila za Kiafrika Misibani ni sehemu ya Kuomboleza tu na kumuombea Marehemu makazi mema huko aendako.

Nawasubiri kwa hamu sana niwaone hao Wanachama wa awali wa Chama kipya nchini Tanzania cha ' MboKa ' Alliance ili nami niweze kujua idadi kamili ya Watu ambao wanaenda kupata ' laana ' ya Kutukuka ya Marehemu Mwalimu ili pengine liwe fundisho kwa ' Wanafiki ' wengine wote wa Kisiasa nchini Tanzania.

Nawasilisha.

Umesoma gazeti gani chief

Kwani wamezungumza wapi huo muungano!?
 
Ifike muda sasa tujifunze kuheshimu misiba na hasa wale ambao tunawaomboleza ili kuonyesha kwamba kweli tumeumia na kuondoka Kwao hapa duniani na tuache hizi tabia za ' Kipuuzi ' za kila mara kupenda kutumia misiba kama sehemu yetu ya Kujiimarisha na kupata Sifa Kisiasa.

Chama kipya cha ' MboKa ' Alliance hakiwezi kuwa na baraka kama kimeanzishiwa Msibani sana sana tu kinaweza kikajikuta kinapata ' laana ' ambayo itakiangamiza zaidi.

Kwahiyo mnataka kutuambia kwamba bila Msiba huo kutokea huu Muungano wa ' Kinafiki ' wa ' MboKa ' Alliance usingetokea? Je tukisema labda kwa tamaa zenu za Kisiasa labda nyie ndiyo ' Wachawi ' wenyewe ambao ' mmemroga ' Marehemu ili afe halafu kupitia Msiba wake mjijenge Kisiasa tutakuwa tunakosea?

Siasa bora, njema na zenye mantiki na tija huwa hazianzishwi Misibani bali kuna ' mazingira ' maalum ambayo yanaweza yakachochea Watu kufanya Siasa ila kamwe na hata katika Mila za Kiafrika Misibani ni sehemu ya Kuomboleza tu na kumuombea Marehemu makazi mema huko aendako.

Nawasubiri kwa hamu sana niwaone hao Wanachama wa awali wa Chama kipya nchini Tanzania cha ' MboKa ' Alliance ili nami niweze kujua idadi kamili ya Watu ambao wanaenda kupata ' laana ' ya Kutukuka ya Marehemu Mwalimu ili pengine liwe fundisho kwa ' Wanafiki ' wengine wote wa Kisiasa nchini Tanzania.

Nawasilisha.
ndugu, nimesema na ninarudia kusema tena - na nyie CCM anzeni kwanza kuheshimu jeshi letu.
msitumie jeshi letu kama platform ya kufanya siasa.

CCM imechakaa. ukiangalia nje ya bunge, mtendaji mwenye nguvu kuliko wote (ukiachilia rais) ni yule dogo aliyekula mzinga form 4.

ukirudi mle bungeni, wabunge mnaowategemea kujenga hoja eti ni kina Kibaji (std 7) na Msukuma (std 7).

ndiyo maana tutaendelea kuwakumbusha where exactly you belong.... CCM bila polisi ni wepesi kama ile karatasi ya kuchambia!
 
Lumumba mnaweweseka kweli maana mlianza kulimezea mate Jimbo kwa ushirikiano huu hamtoki,wezi wakubwa nyie...
 
Sehemu yeyote yenye mkusanyiko inafaa kujadili mambo muhimu,kwa mfano issue ya msiba inajulikana, nanaliyefariki ni mwanasiasa, kuna ubaya gani kuzungumzia siasa kwenye msiba wa mwanasiasa?

Yeye ameshaenda zake,sisi tunaoendelea kuishi lazima mipango iendelee!
Unashangaa watu kuanzisha chama cha siasa msibani,mbona hushangai watu kutongozana au kutomban.@ msibani??))
 
ukawa walianza hivi na sasa wako wapi
Ruhusuni mikutano na makongamano ya vyama vyote na sio (chama chakavu) tu utajua ukawa wako wapi....unapigana na mtu uliyemfunga pingu mikononi unajisifu unanguvu....
 
Msiwalaumu wanasiasa wakati hii tabia ammeijenga kote. Ni kweli siku hizi msiba pamekuwa mahala pa malengo maalumu. Msibani watu wanaenda kuiba hela za michango ya msiba.

Ninachojua msiba ni ishara kwamba ulikuwa na mahusiano mazuri na marehemu au wafiwa. Kama hukuishi naye vizuri huna haja ya kwenda na hakuna wa kukushangaa.

Hivyo, zamani msibani watu walikuwa wanabubujikwa na machozi, siku hizi msibani ni suala la kuangalia nani kaja au nani hakuja. Msibani kuna watu wanatafuta wachumba. Msibani kuna watu wanataka kujionyesha wana mahusiano mazuri na jamii.

Mimi hadi leo ninakwenda msiba wa mtu ninayepatana naye tu, kwa sababu huyo akifa ninaona kuna pengo hivyo ninam-miss. Lakini kama hukujuana na mimi, au tulikorofishana, wala sioni aibu kukataa kuja msiba wako.

Wiki juzi tu sikwenda kwenye msiba wa binamu yangu kwa ambaye familia yao tuligombana na kuahidiana kutozikana.
 
Back
Top Bottom