Mbase1970
JF-Expert Member
- Jun 11, 2015
- 6,053
- 4,595
Mkuu umenifanya nikatafute youtube hiyo Eulogy ya January Makamba, kijana katulia na nimekubali ulichokisema jamaa kakomaa si tu kisiasa naona katika kila nyanjaKama una akili timamu na umeweza kumfuatilia kwa umakini wako mkubwa kabisa akiwa anazungumza ' mahala fulani ' huwezi kukataa na kutokubaliana nami kwamba 99.9% ya Maelezo yake Mheshimiwa Waziri January Makamba yalikuwa ni Mafumbo ya ' Kimadongo ' kwa Kiongozi mmoja ( ambaye hata Yeye pia alikuwepo eneo la tukio na alikuwa anamsikiliza mno tu ) huku akiwa ametumia ujuzi wake mkubwa wa ' Fasihi ' katika Uwasilishaji mbele ya Hadhira.
Sasa naamini kwamba kumbe kuna Vita ya chinichini kati ya January Makamba na huyo Kiongozi ( ambaye namhifadhi ) ila nipende tu kuchukua muda huu sasa kumuomba huyo Kiongozi kuwa mara baada ya tukio la Jumatatu ijayo basi aanze Kujitafakari na ikibidi aweze Kubadilika upesi ili na Yeye Siku ikitokea Mwenyezi Mungu akimchukua basi nasi tutakaokuwepo tuweze Kumlilia na Kumkumbuka kwa mema kama Mpendwa wetu mmoja.
Hakika sijapata kuona Kijana Mjanja, Mwerevu na anayejua Kupima maneno yake vyema huku akijua azungumze nini na wapi huku akimpiga Mtu ' Madongo ' tena akiwa hapo hapo bila kujua ni Yeye na si ajabu nae akawa anacheka kama Mheshimiwa Waziri January Makamba na kuanzia leo nampa Cheo rasmi cha Rais wa Mafumbo na Fasihi Kali.
Baadhi ya maneno yake ni kama yafuatayo nikiyanukuu hapa chini...
" Marehemu hakupenda attention kama wengi wetu "
" Marehemu hakuwa Mtu wa Kinyongo "
" Marehemu hakupenda kabisa Sifa au Kusifiwa kitu ambacho kwa wengi Wetu ni Kigumu "
" Marehemu alichukia mno Kuwaonea wengine kwa Wadhifa wake / Ukubwa wake "
" Marehemu amenifundisha Kunyenyekea Kitu ambacho kwa Sisi wenye dhamana ni ngumu "
" Ukiona una Kigugumizi cha kushindwa Kumzungumzia Marehemu jua kuna maana mbili hapo kwamba ama huna Shukran na umejawa Unafiki ndani yako au umeumizwa Kiukweli kutokana na Mema yake yote aliyokuwa akikufanyia "
" Marehemu atufanye Sisi tuliobaki na hasa wenye dhamana hizi Kubadilika Kimatendo ili nasi Siku tukiondoka hapa duniani tuliliwe hivi kama Yeye "
Shikamoo sana na mno January Makamba. Leo nimekuvulia Kofia rasmi kwamba uko vizuri Kichwani na nina uhakika hata Mzee wako Yusuph Makamba kama kuna Mtoto ambaye anajivunia nae basi ni Wewe. Popote ulipo nakuomba endelea na aina hii ya Hekima na Busara uliyonayo na niseme leo hapa kwamba kama ' coming 2025 ' nikisia Chama changu cha CCM kime ' Shortlist ' majina Matatu na Wewe umo basi nina uhakika kwa Uwezo wako mkubwa, uwerevu wako, exposure yako na Malezi yako basi kwa 99% una uwezo wa kuja kuwa Rais wa Tanzania.
Mwenyezi Mungu akusaidie na akusimamie Kaka.
Nawasilisha.