okiwira
JF-Expert Member
- Jul 23, 2018
- 2,787
- 2,853
MweeeeeSikubaliani na wewe, baada ya 2015 kutakuwa na katiba mpaya ambayo haitampa raisi madaraka makubwa na kutakuwa na utawala wa sheria, pia kuwawajibisha wavivu siyo udikteta, swala la mashoga raisi hawezi kuwa na maamuzi nalo kwani litakuwa chini ya mahakama ya katiba kuamua, kumbuka wakati huo mahakama zitakuwa huru, tofauti na sasa.
Kuhusu kupola mali za mafisadi huenda hasifanye hivyo, badala yake akawasamehe, akaunda tume ya uwazi na ukweli ambayo itawahoji watakaohisiwa walikuwa mafisadi ili wasaidie kuzuia ufisadi usitokee kirahisi.
Rais ajae atakuwa na kazi ngumu sana, kwani kila idara ya nchi imeoza na hawezi kuwa na nguvu sana kisheria kama alivyo raisi wa sasa.