OCC Doctors
Senior Member
- Jul 20, 2018
- 104
- 151
Uotaji wa meno hutofautiana kati ya mtoto wa kiume na wa kike. Mtoto wa kike anawahi kuota meno kuliko yule wa kiume. Kwa wastani watoto wengi huanza kuota meno wanapokuwa na umri wa miezi sita. Kwa kawaida meno mawili ya chini huanza (meno ya mbele). Kisha hufuatia meno ya juu. Baada ya hapo meno mengine huendelea kuota mara nyingi huota mawili mawili (moja moja kila upande).