Kuangusha kombora moja la Hamas kunaigharimu israel dola 80,000

kimsboy

JF-Expert Member
Oct 17, 2016
8,987
17,861
Kuangusha kombora moja la wa- Palestina, kunaigharimu Israel Dola elfu 80
Mei 07, 2019 13:55 UTC
Gazeti la utawala wa Israel Hayom limeandika kwamba, utawala huo hauwezi kumudu gharama kubwa ya Kuongoza na kuangusha kila kombora linalovurumishwa kutoka Ukanda wa Gaza.

Kwa mujibu wa gazeti hilo, kuongoza na kuangusha kombora moja kwa kutumia ngao ya makombora ya utawala huo inayoitwa 'Kuba la Chuma' (iron dome) kwenye operesheni zake za kiulinzi kunagharimu kiasi cha Dola elfu 80.

Aidha limeongeza kwamba utumiaji wa ngao nyingine ya makombora inayoitwa 'David's Sling' una gharama mara dufu katika kukabiliana na makombora yanayovurumishwa na Hamas wa Palestina kuelekea miji ya Israel. Kwa mujibu wa gazeti la Israel Hayom, gharama ya kuzuia na kuangusha kombora moja, ni zaidi ya Dola milioni mbili kwa kutumia ngao hiyo ya David's Sling.

Itakumbukwa kufuatia kufeli ngao ya makombora ya 'Kuba la Chuma' mwaka jana utawala wa israel ulizindua ngao nyingine inayoitwa David's Sling.

Gazeti hilo limekiri kwamba kitendo cha Wapalestina kutumia makombora ya gharama nyepesi inawawea rahisi wanapalestina kuunda haraka makombora hayo.

Aidha limeongeza kuwa, suala la wapiganaji wa Gaza kuwa na akiba kubwa ya makombora, linawafanya waweze kuingia katika vita vya muda mrefu na Israel bila kuhitaji kuunda makombora mapya.

Jumatatu ya jana kanali ya 12 ya televisheni ya utawala wa israel ilikiri kufeli ngao ya makombora ya israel ya 'Kuba la Chuma' (iron dome) mbele ya mashambulizi ya Wapalestina na kuongeza kwamba katika mapigano ya hivi karibuni jumla ya makombora 650 yalivurumishwa kutoka Gaza kwenda miji ya utawala huo na kwamba ngao hiyo iliweza kuzuia makombora 170 pekee.

My take:Israel inazidi kupata hasira tu ndo maana siku hizi waisrael wana umasikini wa kutisha daaah
4bsf2e689ab61c1e0ls_800C450.jpg
 
Siku zote tangu ulipotokea mapinduzi ya viwanda, bajeti kubwa imekuwa ikielekezwa kwenye ulinzi hadi kupelekea watu kufa kwa njaa!
Sio Israel tu bali ni mataifa yote ya dunia.

Inakadiriwa kwamba kama isingelikuwa hivyo, wakaazi wote wa dunia wasingepata shida yoyote ya maji, vyakula, umeme na maisha mazuri ya uhakika.

Kuliweka taifa katika usalama kunahitaji gharama ambayo ni ya kutisha!

Kwanza kabisa wanajeshi wanahitaji mshahara mzuri pamoja na poshoposho ambazo zingine ni siri
 
Dini zimesha watawala hamanaga reasoning ya masuala ya dunia ndomaana Africa tutabaki hivi hivi siku zote......
Mkuu Mimi sija zungumzia Dini hapo Mimi simo humo unapofikiria Mimi ni bina Adam sawa na wengine tofauti rangi tu Mimi Sina mteule!! Tupo sawa wote hakuna binaadam malaika!! Awe mzungu awe mwarabu awe mwafraca wote sawa!!
 
Hakuna sehemu watu hawapati shida!
Hata na hao wapalestina wanapata shida vile vile
 
Kwa taarifa yako ISRAEL wana ustawi na maendeleo kuliko hao Palestine wanaotengeneza roketi kwa 5000
 
Waisraeli hawawezi baki salama milele. Kumkana Mesiya na kumuua na kutaka kufuta kabisa historia yake na nguvu na miujiza aliyofanya. Hilo hawa jamaa watateseka tu miaka yote. Mungu hawezi kunyamazia hilo la kumkana yule aliyemtuma ambaye ni njia, kweli na uzima.
Hao waliopo hapo Israel kwa sasa sio wale wayaudi waliomkataa yesu.. Hao waliopo ni ashkenaz kutoka ulaya.
 
Waisraeli hawawezi baki salama milele. Kumkana Mesiya na kumuua na kutaka kufuta kabisa historia yake na nguvu na miujiza aliyofanya. Hilo hawa jamaa watateseka tu miaka yote. Mungu hawezi kunyamazia hilo la kumkana yule aliyemtuma ambaye ni njia, kweli na uzima.
Mlaumu Mungu kwanza kwa kushindwa kumlinda alieyemtuma ,,mpaka viumbe dhaifu binadamu wakamuua,badala ya kulaumu mzizi(shina) wewe unalaumu matawi
 
Mlaumu Mungu kwanza kwa kushindwa kumlinda alieyemtuma ,,mpaka viumbe dhaifu binadamu wakamuua,badala ya kulaumu mzizi(shina) wewe unalaumu matawi

Mungu alijua kuwa angeweza kumfufua. Shida iko kwa wale ambao hadi leo wanamsubiri mesiya wao. Yule waliyemuua hawamtambui.
 
Back
Top Bottom