kimsboy
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 8,987
- 17,861
Kuangusha kombora moja la wa- Palestina, kunaigharimu Israel Dola elfu 80
Mei 07, 2019 13:55 UTC
Gazeti la utawala wa Israel Hayom limeandika kwamba, utawala huo hauwezi kumudu gharama kubwa ya Kuongoza na kuangusha kila kombora linalovurumishwa kutoka Ukanda wa Gaza.
Kwa mujibu wa gazeti hilo, kuongoza na kuangusha kombora moja kwa kutumia ngao ya makombora ya utawala huo inayoitwa 'Kuba la Chuma' (iron dome) kwenye operesheni zake za kiulinzi kunagharimu kiasi cha Dola elfu 80.
Aidha limeongeza kwamba utumiaji wa ngao nyingine ya makombora inayoitwa 'David's Sling' una gharama mara dufu katika kukabiliana na makombora yanayovurumishwa na Hamas wa Palestina kuelekea miji ya Israel. Kwa mujibu wa gazeti la Israel Hayom, gharama ya kuzuia na kuangusha kombora moja, ni zaidi ya Dola milioni mbili kwa kutumia ngao hiyo ya David's Sling.
Itakumbukwa kufuatia kufeli ngao ya makombora ya 'Kuba la Chuma' mwaka jana utawala wa israel ulizindua ngao nyingine inayoitwa David's Sling.
Gazeti hilo limekiri kwamba kitendo cha Wapalestina kutumia makombora ya gharama nyepesi inawawea rahisi wanapalestina kuunda haraka makombora hayo.
Aidha limeongeza kuwa, suala la wapiganaji wa Gaza kuwa na akiba kubwa ya makombora, linawafanya waweze kuingia katika vita vya muda mrefu na Israel bila kuhitaji kuunda makombora mapya.
Jumatatu ya jana kanali ya 12 ya televisheni ya utawala wa israel ilikiri kufeli ngao ya makombora ya israel ya 'Kuba la Chuma' (iron dome) mbele ya mashambulizi ya Wapalestina na kuongeza kwamba katika mapigano ya hivi karibuni jumla ya makombora 650 yalivurumishwa kutoka Gaza kwenda miji ya utawala huo na kwamba ngao hiyo iliweza kuzuia makombora 170 pekee.
My take:Israel inazidi kupata hasira tu ndo maana siku hizi waisrael wana umasikini wa kutisha daaah
Mei 07, 2019 13:55 UTC
Gazeti la utawala wa Israel Hayom limeandika kwamba, utawala huo hauwezi kumudu gharama kubwa ya Kuongoza na kuangusha kila kombora linalovurumishwa kutoka Ukanda wa Gaza.
Kwa mujibu wa gazeti hilo, kuongoza na kuangusha kombora moja kwa kutumia ngao ya makombora ya utawala huo inayoitwa 'Kuba la Chuma' (iron dome) kwenye operesheni zake za kiulinzi kunagharimu kiasi cha Dola elfu 80.
Aidha limeongeza kwamba utumiaji wa ngao nyingine ya makombora inayoitwa 'David's Sling' una gharama mara dufu katika kukabiliana na makombora yanayovurumishwa na Hamas wa Palestina kuelekea miji ya Israel. Kwa mujibu wa gazeti la Israel Hayom, gharama ya kuzuia na kuangusha kombora moja, ni zaidi ya Dola milioni mbili kwa kutumia ngao hiyo ya David's Sling.
Itakumbukwa kufuatia kufeli ngao ya makombora ya 'Kuba la Chuma' mwaka jana utawala wa israel ulizindua ngao nyingine inayoitwa David's Sling.
Gazeti hilo limekiri kwamba kitendo cha Wapalestina kutumia makombora ya gharama nyepesi inawawea rahisi wanapalestina kuunda haraka makombora hayo.
Aidha limeongeza kuwa, suala la wapiganaji wa Gaza kuwa na akiba kubwa ya makombora, linawafanya waweze kuingia katika vita vya muda mrefu na Israel bila kuhitaji kuunda makombora mapya.
Jumatatu ya jana kanali ya 12 ya televisheni ya utawala wa israel ilikiri kufeli ngao ya makombora ya israel ya 'Kuba la Chuma' (iron dome) mbele ya mashambulizi ya Wapalestina na kuongeza kwamba katika mapigano ya hivi karibuni jumla ya makombora 650 yalivurumishwa kutoka Gaza kwenda miji ya utawala huo na kwamba ngao hiyo iliweza kuzuia makombora 170 pekee.
My take:Israel inazidi kupata hasira tu ndo maana siku hizi waisrael wana umasikini wa kutisha daaah