Kuajiriwa ama kujiajiri

Kaka binafsi nakushauri ujiajiri,suala la kuajiriwa kwa nchi hii ni pasua kichwa,maana hata kama umesoma hakuna anayejali professional,haiingii akilini nchi ina uhaba wa madaktari halafu unamlipa daktari sh, 600,000 kwa mwezi mbuge ambaye pengine kabahatika kupata elimu ya msingi analipwa M 6-12 kwa mwezi kweli hii ni nchi inayothamini professional?huo ni mfano mmojawapo.Mimi kama huyo jamaa aliyetoa mfano hapo juu nilikuwa nimeajiriwa nikifanya kazi na consulting firm ya makaburu fulani hapa town mshahara wangu ulikuwa 1,100,000 take home ukiweka gross ni kama 1.6 million hivi ila mwajiri wangu alikuwa anacharge USD 50 kwa saa kwa uwepo wangu site (nina maana ninapokuwa nasimamia kazi yoyote ya site)You can imagine for a day of 8hrs uwepo wangu site unamtengenezea mwajiri USD 400 na muda mwingi wa kazi zangu ilikuwa site naweza kuwa ofisini kwa wiki moja tu katika mwezi mzima.Nikaanza ndogo ndogo ikiwepo kufungua kampuni,nilipoweza kufungua kampuni japo ilikuwa ya mfukoni sikuwa na ofisi,ofisi ilikuwa nyumbani kwangu nikatoa notice ya miezi miwili huku sijui nitafanyafanyaje mambo yasipokwenda vizuri lakini niliamua na mawazo yangu hayakuwahi kufikiri kufanya kazi za kuajiriwa siku zote nilijipa muda wa miaka mitatu baada ya kutoka chuo lakini haikuwezekana ilipofika mwaka wa nne nikaamua liwalo na liwe nikajitoa muhanga.Mwezi wa november 2009 ndo ilikuwa mwisho wa notice ya ajira yangu,baada ya hapo nikaanza kutafuna akiba huku nikipambana kupata mpenyo wa kazi kwa ajili ya kampuni yangu,sikuweza kufanikiwa mpaka April 2010 nilipopata kazi ya Million 6 ilinipa faida ya milion 2,nikapata tena dili la M 38,kuanzia hapo ikawa ni kazi juu ya kazi to date naongea na kazi ya M 158 mkononi mambo hayakuwa rahisi kwa kipindi ambacho sikuwa na kazi na sikuwa na akiba ya kutosha maana kwa mshahara wangu wa M 1.6 ulikuwa na majukumu mengi hasa familia tegemezi ilikuwa kubwa,lakini nilijitoa muhanga nikaamua kwa ajili ya maisha ya baadae na Mungu akanisimamia,kama una wazo la kujiajiri ni suala la kupongezwa maana najua ipo siku utachukua hatua japo itakuwa ya kuumiza kichwa ila itakusaidia,pia nakushauri usifanye biashara ya kuiga tafuta biashara ambayo hata kama ni ndogo lakini si yenye watu wengi kama profesional yako inaruhusu kujiajiri kupitia hiyo fanya hivyo,maana kwa nchi yetu utakuta PROFESSOR na LAYMAN hawana tofauti hata katika kufanya biashara,maana utakuta layman ana daladala na profesor ana daladala why akawa profesor?kuwa profesor ina maana hata namna ya kufikiri kwako lazima kuwe tofauti na watu wengine profesor anatakiwa kutumia elimu yake aandike maandiko watu wampe pesa aanzishe kiwanda,au ufugaji mkubwa au kilimo chenye tija lakini utakuta hatuna wasomi wa aina hiyo. Jiyoe muhanga kiongozi utaona mafanikio,hata kama utaanza kwa kununua jiko mahali ukaange chipsi lakini ni biashara yako usikaange chipsi kama wengine we ongeza manjonjo kidogo ili uibe wateja toka kwa jirani yako hivyo ndo tunatakiwa kuwa watanzania,ubunifu kidogo tu unakuuza. Nitakupa mfano mwimgime **** juice ngapi zinatengenezwa hapa Tanzania na za bei rahisi tu?lakini angalia DELMONTE ilivyoteka soko la juice hapa Tanzania japo ni juice ghali lakini packaging yake inaiuza bila mgogoro.Anza sasa kuchukua hatua.


Mkuu umenivukisha mahali maana naona kama napita kwenye hali kama ya kwako. Nilipotoka tu chuo nilichukia mno kuajiriwa. Ila nilijipa muda wa miaka minne tu wa kuandaa na kuendeleza biashara yangu. Miaka minne ilipoanza kukaribia kuisha mwaka jana 2011, nilikuwa bado sijaweza kuifikisha biashara yangu nilipokuwa nimeplan iwe. Kwa kuwa nilisha panga kuacha nikasema sitarudi nyuma lazima ni-terminate contract. So, mwaka jana nimeacha kazi, miezi miwili iliyopita ilikuwa migumu sana kwangu, ila naona hali ya ofisi yangu inaanza kuonyesha matunda mazuri.

Kabla ya kuacha kazi niliwashirikisha watu plan yangu, zaidi ya asilimia 90 hawakunielewa, ndipo nilipoamua kuchukua uamuzi binafsi, hata ndugu sikuwaambia kama nimeacha kazi maana lazima wangelikataa wazo langu.

Ninachoweza kushauri,kama upo kwenye ajira,
1. Fahamu nini unachotaka kufanya pindi utakapo kuwa nje ya ajira,
2. Anza kuweka mkakati wa kukifanyia kazi ukiwa ndani ya ajira.
3. Weka muda pia kwamba unataka kuajiriwa mpaka lini, let say, mwaka 1, 2 au 3..n.k, bila ku-set muda utajikuta una mawazo ya kujiajiri lakini lini hujui na utaendelea kubakia kwenye ajira maisha yako yote ukiwa na wazo la kujiajiri mwenyewe. Pia uwe strict katika muda ulio set, na hapa ndipo maamuzi magumu yanapojitokeza unapotaka kuendena na plan yako.
4. Tafuta ushauri kwa watu tofauti walioko kwenye biashara na haswa biashara unayotaka kufanya na ujifunze kutoka kwao..

All the best.
 
Mkuu umenivukisha mahali maana naona kama napita kwenye hali kama ya kwako. Nilipotoka tu chuo nilichukia mno kuajiriwa. Ila nilijipa muda wa miaka minne tu wa kuandaa na kuendeleza biashara yangu. Miaka minne ilipoanza kukaribia kuisha mwaka jana 2011, nilikuwa bado sijaweza kuifikisha biashara yangu nilipokuwa nimeplan iwe. Kwa kuwa nilisha panga kuacha nikasema sitarudi nyuma lazima ni-terminate contract. So, mwaka jana nimeacha kazi, miezi miwili iliyopita ilikuwa migumu sana kwangu, ila naona hali ya ofisi yangu inaanza kuonyesha matunda mazuri.

Kabla ya kuacha kazi niliwashirikisha watu plan yangu, zaidi ya asilimia 90 hawakunielewa, ndipo nilipoamua kuchukua uamuzi binafsi, hata ndugu sikuwaambia kama nimeacha kazi maana lazima wangelikataa wazo langu.

Ninachoweza kushauri,kama upo kwenye ajira,
1. Fahamu nini unachotaka kufanya pindi utakapo kuwa nje ya ajira,
2. Anza kuweka mkakati wa kukifanyia kazi ukiwa ndani ya ajira.
3. Weka muda pia kwamba unataka kuajiriwa mpaka lini, let say, mwaka 1, 2 au 3..n.k, bila ku-set muda utajikuta una mawazo ya kujiajiri lakini lini hujui na utaendelea kubakia kwenye ajira maisha yako yote ukiwa na wazo la kujiajiri mwenyewe. Pia uwe strict katika muda ulio set, na hapa ndipo maamuzi magumu yanapojitokeza unapotaka kuendena na plan yako.
4. Tafuta ushauri kwa watu tofauti walioko kwenye biashara na haswa biashara unayotaka kufanya na ujifunze kutoka kwao..

All the best.

wakuu tatizo la uoga wa watanzania kutake risk linachangiwa na na vitu viwili.
1.mfumo wa maisha tuliyolelewa-tangu tukiwa wadogo tunaambiwa soma uje kupata kazi nzuri,na sio soma uje kutengeneza ajira.sasa hii inatujenga hadi tunapomaliza chuo kuamini kazi nzuri ni ile tu unayoenda kuajiriwa na si vinginevyo.na hata hivi leo mtu akionekana asbuhi hajavaa shati na na tai na nakachomekea anaonekana hana future nzuri au shuguli maalumu
2.mfumo wa elimu,elimu yetu inatuandaa kukariri na kufaulu mitihani tu na sio kutufikirisha kutatua matatizo.pia kujiajiri kunahitaji kujituma na kufanya kazi kwa bidii amabalo hilo wataanzania wengi hawako tayari kwasababu kwenye ajira watu uwa mda wote wana feel proud kuwa na kazi lakini si utkelezaji wa majukumu kwa ufanisi.
Nb:kujiajiri kwa mazingira ya sasa ya ajira ni best option,maslahi ni kidog sana kwenye ajira.ni raha sana asubuhi unaamka unaelekea ofisini kwako.
 
Bora kufanya yote mawili na ndivyo wengi wanafanya.

Nakuelewa sana Husninyo ni kweli wengi wanafanya hivi na ndio sababu wengi wanashindwa ku-take off.Lazima kuchagua moja hapa na kuwa tayari ku-take risk ili kufikia malengo husika hakuna kitu kama kufanya vyote kwa pamoja(isipokuwa kwenye zile hatua za awali kabisa za kujiajiri) kwa sababu lazima kuna kimoja kitazorota au unaweza kuvipoteza vyote.
Ajira inahitaji kuwekeza umakini ma muda wa kutosha na kujiajiri kupo hivyohivyo.
 
Bora ujiajiri hata kwa kuuza sigara unatoka kimaisha kuliko kusubiri ajira ya mwisho mwezi
 
Nakuelewa sana Husninyo ni kweli wengi wanafanya hivi na ndio sababu wengi wanashindwa ku-take off.Lazima kuchagua moja hapa na kuwa tayari ku-take risk ili kufikia malengo husika hakuna kitu kama kufanya vyote kwa pamoja(isipokuwa kwenye zile hatua za awali kabisa za kujiajiri) kwa sababu lazima kuna kimoja kitazorota au unaweza kuvipoteza vyote.
Ajira inahitaji kuwekeza umakini ma muda wa kutosha na kujiajiri kupo hivyohivyo.

nimekusoma ila kujiajiri na kuajiriwa vyote vina faida na hasara zake. Naona humu imekuwa fashion kila anaekuja anasema bora kujiajiri wakati wao wenyewe ni waajiriwa hadi wanazeekea kazini. Mambo kama haya ni vizuri kumwelesha mtu kwa pande zote mbili.
 
We Husnino ukimaliza phD jiajiri hata kufuga kuku ni shwari tu imradi una ofc yako
 
Niliwahi kusoma kitabu kimoja cha mambo ya ujasiriamali ameandika mfilipino mmoja (sikikukmbuki title, nitajaribu kukitafuta nishee) anasema kama umeajiriwa si vema kuacha kazi kwenda kujiajiri. Unatakiwa ujiajiri wakati unaendelea na kazi mpaka huo mradi wako utakapoweza kukupatia mara mbili ya mshahara wako ndo uache kazi ukasimamie mwenyewe mradi wako ili kuongeza kipato zaidi.

Hii ni nzuri cuz unaweza ukayumba wakati biz ipo mwanzoni na ajira ikakusaidia kuisukuma.
 
Kujiajiri, ukiweza, ni jambo bora si kwako tu, bali kwa uchumi wa taifa pia. Ukijiajiri haiyumkini utapanuka hata kama ni polepole, na utaajiri wengine. Ndio maana mitaala ya vyuo siku hizi ina somo la ujasiriamali.

Kama walivyosema wengine, kutegemea kipato halali cha kuajiriwa kwa kawaida hakuwezi kukuletea utajiri. Lakini ukijiajiri - possibilities zinakuja.

umesema sawa mkuu,lakini hebu angalia serikali imeweka mikakat gani kumsaidia kijana huyu ambaye ana nia ya dhati kabisa ya kujiajiri?kwa sababu hana mtaji,kazi hana,na ana mahitaji ya kila siku yanamkabili,afanye nn? Au nini kifanyike? Asante mkuu kwa mchango.
 
mkuu thats what life is all about; HAPPINESS, ABUNDANCY, SERVING OTHERS, FREEDOM, LIFE STYLE OF YOUR DREAM........

TRAVELLING THE WORLD IMETULIA SANA.

hivi pesa za retirement hz hz za madafu zinaweza zikatupa hivyo vitu kweli? Na ukumbuke dependence ya wandugu with your amount fixed,hebu nijibu mkuu,otherwise thanks
 
naomba niwe tofauti na wengi katika hili..UJASIRIAMALI SIO SOMO LA KUFUNDISHWA KAMA KIINGEREZA AU HESABU...ITS AN ART..gifted from the one HIGH ABOVE....watu wanazaliwa wajasiriamali na HAWAINGIZWI DARASANI kuwa wajasiriamali...ndio maana kunatofauti kubwa kati ya MFANYABIASHARA NA MJASIRIAMALI....wafanyabiashara wanafundishwa lakini wajasiriamali wanazaliwa na pia ni "kipaji kinachorithiwa"

Kwa hiyo mkuu unataka kuniambia ile elimu ya ujasiriamali tuiite biashara? Mm ninaweza kusema kwa upeo wangu wa wastani kuwa kila kitu kinakwenda kwa elimu,without education the mission is blank,isipokuwa elimu haipatikani darasani tu,hata kitaa waweza pata elimu,au unasemaje bwana mkubwa? Thanks for your contribution
 
kuna fursa nyingi sana katika kujiajiri. ni wewe tu kuwa na moyo wa kijasiriamali na kujua wapi utapata mitaji ya kujiendesha, na mikakati ya kuendeleza biashara yako

Ni kweli mkuu,spirit ya entrepreneurship ni muhimu sana,hii itakusaidia kupenya pindi utanda wa changamoto utakapotokea.
 
Wakuu nime jitahidi kusearch hadi nimekutana na hili somo,very nice.kweli JF ni kiboko.

mkuu,hapa ndio mahali pake,ila usichukue haya materials kwa ajili ya kujibu mtihani,yachukue kwa ajili ya practical application ili ujikuomboe kiuchumi na uinjoy matunda kama freedom nk,shukrani mkuu.
 
Kujiajiri, ukiweza, ni jambo bora si kwako tu, bali kwa uchumi wa taifa pia. Ukijiajiri haiyumkini utapanuka hata kama ni polepole, na utaajiri wengine. Ndio maana mitaala ya vyuo siku hizi ina somo la ujasiriamali.

Kama walivyosema wengine, kutegemea kipato halali cha kuajiriwa kwa kawaida hakuwezi kukuletea utajiri. Lakini ukijiajiri - possibilities zinakuja.

Mkuu nilisahau kukupongeza kwa kuweka neno "ukiweza" bilashaka lina maana sana hapo.
 
Mkuu umenivukisha mahali maana naona kama napita kwenye hali kama ya kwako. Nilipotoka tu chuo nilichukia mno kuajiriwa. Ila nilijipa muda wa miaka minne tu wa kuandaa na kuendeleza biashara yangu. Miaka minne ilipoanza kukaribia kuisha mwaka jana 2011, nilikuwa bado sijaweza kuifikisha biashara yangu nilipokuwa nimeplan iwe. Kwa kuwa nilisha panga kuacha nikasema sitarudi nyuma lazima ni-terminate contract. So, mwaka jana nimeacha kazi, miezi miwili iliyopita ilikuwa migumu sana kwangu, ila naona hali ya ofisi yangu inaanza kuonyesha matunda mazuri.

Kabla ya kuacha kazi niliwashirikisha watu plan yangu, zaidi ya asilimia 90 hawakunielewa, ndipo nilipoamua kuchukua uamuzi binafsi, hata ndugu sikuwaambia kama nimeacha kazi maana lazima wangelikataa wazo langu.

Ninachoweza kushauri,kama upo kwenye ajira,
1. Fahamu nini unachotaka kufanya pindi utakapo kuwa nje ya ajira,
2. Anza kuweka mkakati wa kukifanyia kazi ukiwa ndani ya ajira.
3. Weka muda pia kwamba unataka kuajiriwa mpaka lini, let say, mwaka 1, 2 au 3..n.k, bila ku-set muda utajikuta una mawazo ya kujiajiri lakini lini hujui na utaendelea kubakia kwenye ajira maisha yako yote ukiwa na wazo la kujiajiri mwenyewe. Pia uwe strict katika muda ulio set, na hapa ndipo maamuzi magumu yanapojitokeza unapotaka kuendena na plan yako.
4. Tafuta ushauri kwa watu tofauti walioko kwenye biashara na haswa biashara unayotaka kufanya na ujifunze kutoka kwao..

All the best.

Nashukuru mkuu kwa mchango mzuri,kikubwa ni kuyaweka katika matendn ili tuweze kufanikiwa,
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom